Wasanii 13 wa taarab wafa ajalini

Wasanii 13 wa taarab wafa ajalini

Chimemena

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2011
Posts
1,376
Reaction score
453
Kuna tetesi kwamba kundi la 5 * taarabu wamepata ajali huko kibaha na inasadikika robo ya watu wamekufa..!!

Source: clouds fm
 
Wadau,

Taarifa za hivi punde kutoka Chalinze ni kuwa kikundi maarufu cha Taarab cha Five Stars kimepata ajali mbaya maeneo ya Chalinze na kisababisha vifo vya takribani robo tatu ya wanamuziki wote.

Ajali hii imetokea usiku huu. Idadi kamili ya waliokufa ama kujeruhiwa haijawekwa wazi kinagaubaga. Tunaendelea kufuatilia.

Pia haijajulikana walikuwa wanatokea wapi, ila inaaminika walikwa wanarudi jijini Dar baada ya Show ya weekend katika mikoa ya jirani.

Pole kwa ndugu, jamaa, marafiki wa marehemu na majeruhuu, pia na wadau wote wa muziki wa taarabu.

Mwenye taarifa kamili tafadi atujuje. RIP all.

Source: Clouds FM Sports Etra usiku huu
 
inna lilah wa ina ilayhi raaiun,tunaomba habari zaidi bac mkuu
:hatari:
 
Kuna taarifa zisizo rasmi kwamba kundi la taarabu la five star wamepata ajali mbaya ya gari maeneno ya kibaha na robo tatu ya wanamuziki wamepoteza maisha.

Kama kuna mtu alipita maeneo hayo au kuwa na taarifa rasmi tunaomba atujuze.

Naomba kuwasilisha.
 
Ni vizuri ume2pa habari, na amini umesikiliza clouds na wao hawana uhakika ni watu wangapi wamefariki.
Hebu tupe data kamili sasa wewe?
 
watu wamekufa, unaweza kuacha huo ulevi wako wa siasa za chuki, uzandiki na unafiki kwanza watu waomboleze? shame on you

RIP Marehemu wote

Hapo hakuna siasa ila ukweli ni kuwa serikali inayo simamia miundo mbinu ndiyo inapaswa kubeba lawama zote kwani ajali Tz ni nyingi sana na zinasababishwa na miundombinu mibaya
 
Mungu awasamehe, azilaze roho za marehemu mahala pema,wapumzike kwa amani!
 
We nduka, naanza kupata wasiwasi juu yako humu jamvin ni nani hasa! Kama sio Ma................bac ni El......
 
Huu ni utani au ni kweli?? Maana naona badala ya kuomboleza wengine wanapigana vijembe!
 
Nini wa taarabu, roho za watanzania wasiojuilikana zinatoka hakuna anayeleta ufukunyuku hapa, ila hawa waimba taarabu na wauza sura ndiyo mtulazimishe tupay attention kuangalia na kusikiliza. Its not fair, kila mtu ana haki ya kujadili anachojisikia.
 
Huu ni utani au ni kweli?? Maana naona badala ya kuomboleza wengine wanapigana vijembe!



Ni kweli ila watu wanaleta utani kwenye issue za msingi, inasikitisha sana, Mwenyezi Mungu na mwingi wa Rehema azilaze roho za marehemu mahali pema peponi, Amen!
 
Hawa clouds, yaan badala ya kuweka habari za msingi kuhusu huo msiba, wao wanaleta malumbano ya kimapenzi kati ya diamondi ,diva na wema sepetu, Usupa star kazi kwelikweli,,,
 
Sio Udaku ni habari za uhakika kabisa, 5 star modren taarab bas lao karibu robo tatu wamefariki.
 
Back
Top Bottom