Heshima mkuu
Nimevutiwa na hoja yako. Sielewi unasema nini unapotuambia kuwa tuangalie Ghana wanafanya nini kuhusu sekta ya madini. Una maana kuwa kitu watakachofanya wenzetu tuige tu hata kama ni kibaya? Una maana Mramba na Yona hawawezi kutumia udhaifu wa sheria zetu kufanya uhalifu wa kujinufaisha na kuliingizia hasara taifa? Una maana gani unaposema serikali imelamba galasa kwa kuwafikisha kina Yona na Mramba kwenye mikono ya sheria. Unaweza kueleza ni vipi mtumishi wa umma anaweza kuwa na mali za zaidi ya shilingi bilioni tano, na mjukuu wake ambaye hata hajafikisha miaka 10 anakuwa na hela za kweza kumbail babu yake, Au hizi ni porojo tu?
Unajua kuwa issue kubwa inayotukabili sasa ni EPA, kina Mramba wamefikishwa mahakamani kwa kuliingizia hasara taifa kama kuwafumba macho watanzania, na mii naona ni njia ya kuwafanya wakwepe EPA kiujanja, the game being played is fooling international community so as they can keep on pumping money in, not really rooting out graft. Mimi niko pessmistic sana na mwenendo mzima wa EPA naona kama kuna mchezo unachezwa, lakini this does not mean that jamaa hawana la kuwajibika nalo. Hata Ben ana mengi ya kuwajibika nayo, he oversaw the masacre in Zanzibar hiyo ni kesi tosha tu, kuna uhalifu mwingine unafanyiika huku ukiwa covered na sheria, lakini hili halina maana kuwa huo si uhalifu. Sema tatizo letu ni kuwa hatuna uwezo na ubavu wa kumfikisha mahakamani mpaka walio madarakani waamue.
Yes. Hakuna anayebariki ufisadi. Ila baadhi ya msingi ya kiutawala inaweza kuwafanya mjikute kwenye huo ufisadi. Hivyo ndivyo ilivyo. Kwa mfano madaraka aliyopewa DPP ni makubwa sana. Anaweza yeye kwa matakwa yake akaifuta kesi yoyote bila kuulizwa na mtu yoyote. Na imo kwenye sheria za nchi. Sasa inapotokea kuna corrupt leaders na yeye akawa corrupt unategemea nini hapa?
Kwa hiyo issue siyo kupiga kelele kuhusu Mafisadi au matumizi mabaya ya ofisi. Ni lazima kwanza tupige kelele hizi kanuni/sheria ziondolewa au zibadilishwe then the rest can be easily tackled.
It is very hard/impossible to incriminate Mramba/Yona.