Warioba, the last credible PM

Na wewe ukitumaini kwamba itabidi tuamini hayo ya jikoni unayotuletea basi wataleta wengi kama walivyoleta zile porojo kwamba kifimbo cha Nyerere kilisahauliwa mahala wakashindwa kukibeba.

Tutaamini hadi zile porojo kwamba Kawawa hakuwa anajua English akawa anaongezewa chai hadi Nyerere akamwambia "Kawawa funika Kikombe".

Na wote wanaoelta porojo hizo base yao ni hiihii kama wewe kwamba tusubiri yaandikwe vitabuni kama wataandika.

Porojo tupu.

Mkuu hizo nyekundu ni porojo za shule ya vidudu! Kama ulisoma shule ya vidudu utakuwa ulizisikia lakini kama umesoma kindergarten utakuwa hujazisikia.

Nilichosema si porojo wala ni hali halisi na mambo ndivyo yalivyo. Wewe unategemea hotuba ya Nyerere na bahati mbaya humjui ama hukupata kumjua vizuri Mwalimu Nyerere. Pia nadhani hukujua jinsi Nyerere alivyomwachia madaraka Mwinyi na yeye kubaki kwenye Chama ambacho kilikuwa kinashika hatamu!

Nakuambia tena kwa nia nzuru kwamba kama una hoja zitoe bila matusi utapata tunu. Suala la Nyerere kumweka pale Warioba linajulikana hata kwa watoto waliokuwa chekechea enzi hizo.
 
Crucifix
Nikupateje
Kimbunga

Naomba niwakumbushe ya kuwa yawezekana Mwinyi alimpiga chini Warioba kutokana na utendaji duni wake lakini sababu kuu ya kupigwa chini ni kutokana na katiba yetu. Kama mnakumbuka ni kuwa mwaka 1990 Warioba alipoteza Jimbo la Bunda kwenye uchaguzi mkuu na inadaiwa Nyerere alichangia Warioba kukosa ubunge na kama sikosei ubunge ulienda kwa Stephen Wassira. Sasa kwa mujibu wa Katiba yetu ni kuwa Waziri MKuu lazima ateuliwe miongoni mwa wabunge wa kuchaguliwa majimboni na Warioba alishashindwa jimboni kwake, automatically akakosa sifa kikatiba kuwa waziri mkuu, isipokuwa alichaguliwa kuwa mbunge wa taifa na kuteuliwa kuwa waziri wa TAMISEMI.

Kuhusu uadilifu, hilo sina uhakika nao ila wote twajua stori kuwa jamaa alikuwa mlevi sana hivyo yaweza kuwa hakuwa mwizi ila alikuwa mzembe sana
 
Crucifix
Nikupateje
Kimbunga

Naomba niwakumbushe ya kuwa yawezekana Mwinyi alimpiga chini Warioba kutokana na utendaji duni wake lakini sababu kuu ya kupigwa chini ni kutokana na katiba yetu. Kama mnakumbuka ni kuwa mwaka 1990 Warioba alipoteza Jimbo la Bunda kwenye uchaguzi mkuu na inadaiwa Nyerere alichangia Warioba kukosa ubunge na kama sikosei ubunge ulienda kwa Stephen Wassira. Sasa kwa mujibu wa Katiba yetu ni kuwa Waziri MKuu lazima ateuliwe miongoni mwa wabunge wa kuchaguliwa majimboni na Warioba alishashindwa jimboni kwake, automatically akakosa sifa kikatiba kuwa waziri mkuu, isipokuwa alichaguliwa kuwa mbunge wa taifa na kuteuliwa kuwa waziri wa TAMISEMI.

Kuhusu uadilifu, hilo sina uhakika nao ila wote twajua stori kuwa jamaa alikuwa mlevi sana hivyo yaweza kuwa hakuwa mwizi ila alikuwa mzembe sana
chamakh,

..kifungo kinacholazimisha waziri mkuu ateuliwe toka miongoni mwa wabunge waliochaguliwa majimboni kiliingizwa kwenye katiba baada ya John Malecela kuteuliwa kuwa waziri mkuu.

..kumbuka kwamba Malecela alishindwa ubunge halafu akateuliwa mkuu wa mkoa, baadaye balozi/high commisioner Uingereza, halafu waziri mkuu na makamu wa kwanza wa raisi.
 
Last edited by a moderator:
Kuna thread moja inayohusu mpaka wa Malawi ambayo nimeshauri watanzania wanaokurupuka kama wewe waache umbumbumbu wajikite kusoma vitabu vinavyoozea makatba bila msomaji (Bionyeza hapa).

Sijui kwa nini nisikuite mbumbumbu mkurupukaji. Kwa sababu hapo kwenye RED unaropoka kwamba Rais Mwinyi alimpiga chini Warioba yaani akam-demote kwa kumpa Uwaziri mwingine mbali na Uwaziri Mkuu.Ni mbumbumbu tu anayweze kukurupuka kama wewe kwa sababu Warioba hakuwa demoted kama unavyosema.

Kilichotokea ni kwamba Rais Julius Nyerere ali-resign na kustaafu November 04, 1985 yaani siku Rais Ali Hassan Mwinyi alipoapishwa kuwa Rais wa Tanzani. hadi siku ya kuapishwa Waziri Mkuu alikuwa Salim Ahmed Salim.

Kesho yake Joseph Sinde Warioba akateuliwa kuwa Waziri Mkuu. Kumbuka serikali ya Mwinyi na cabineta yake ilikuwa na uhalali wa miaka mitano na si milele. Hivyo, ilitakiwa kutawala kwa miaka mitano na uje uchaguzi mwingine ili ije serikali nyingine.

Serikali ikafanya kazi yake hadi uchaguzi wa mwaka 1990 uliofanyika October 28, 1990. Mwinyi akashinda uchaguzi huo na akaapishwa upya kuwa Rais wa Tanzania November 08, 1990. Kesho yake yaani siku moja baada ya kuapishwa akamteua John Malecela kuwa Waziri Mkuu wa serikali mpya. Warioba akapewa Wizara ya TAMISEMI kweny ehii serikali mpya iliyoanza November 1990.

Hivyo, kama kichwa chako kinafanya kazi yake badala ya kufunga nywele, huwezi kamwe kusema Warioba alipata demotion au hata kuhamishwa. Serikalini au kwenye taasisi yoyote unapohamishwa toka post moja kwenda nyingine lazima kuna barua inayoonyesha hivyo. Kama Warioba angekuwa amehamishwa toka Uwaziri Mkuu na akapewa Uwaziri mwingine ndani ya kipindi cha miaka mitano ya uchaguzi basi ningekubali kwamba ni demotion.

Lakini hakuna barua ya uhamisho aliyowahi kupewa Warioba. Kama ni barua basi ni ya kumaliza kutumikia Uwaziri katika Serikali ya 1985 hadi Nov. 1990. Kwa kifupi anatakiwa kusifiwa kumaliza kipndi hiki salama.

Nadhani maelezo haya yanakutosha kwa ufafanuzi. Sasa tuje kwa msimamo wa Warioba kama humfahamu.

Kama ni suala la kumpiga chini mwenzake basi Warioba ndiye alimpiga chini Rais wake Ali Hassan Mwinyi mwaka huo 1990. Kwa sababu hujui unatakiwa ufundishwe kwamba NEC-CCM ilikaa chini ya Mwenyekiti Julius Nyerera kuanzia February 07 hadi 12, 1990.

Kwenye hiyo NEC ililetwa report ya jinsi rushwa ilivyoenea serikalini. Mwenyekiti yaani Julius Nyerere akakemea vibaya rushwa ile na kama unakumbuka speech yake kwenye mkutano wa kumchagua Mkapa kuwa mgombea wa CCM, Nyerere alikumbusha wajumbe hili kwamba kemeo lake mle NEC lilifanya Waziri Mkuu aandike barua ya kujiuzuru.

Ingawa kujiuzuru kwa Warioba haukutangaziwa bali tulitangaziwa tu kwamba Rais Mwinyi kavunja baraza la mawaziri (click here). Hata ukisoma habari hiyo utaona kwamba Mwinyi alivunja cabinet March 12, 1990. Ilileta utata hadi ikadhaniwa labda ziara ya Mandela iliyomkuza sana Nyerere badala ya Mwinyi Rais wa nchi ilichangia maana ilikuwa ni siku mbili tu baada ya Mandela kumaliza ziara yake hapa nchini.

Baada ya kuvunja cabinet yake Mwinyi akamtangaza tena Warioba kuwa Waziri Mkuu wake. Ingekuwa ni kumpiga chini basi Mwinyi angetumia nafasi hii kumpiga chini Warioba kama alivyotumia nafasi hii kumuingiza serikalini kwa mara ya kwanza waziri kijana yaani Jakaya Kikwete kuwa Waziri wa Nishati, Maji na Madini.

Hivyo, aliyekuwa ameonyesha nia ya kuondoka serikalini ni Warioba mwenyewe lakini Mwinyi akamrudisha. Na kama nilvyofafanua hapo juu, serikali hii ilipomaliza muda wake, alitakiwa kuja Waziri Mkuu mpya na akaja John Malecela.

Kusoma ni kazi rahisi sana kuliko kukurupuka, kuropoka na kupayuka.

Jazba hazijengi, maelezo yako yanajitosheleza kiasi cha kumshawishi mtu kuwa we ni muelewa, lakin mambo ya kukurupuka, kuropoka na mengine, nahisi una kitu kingine cha ziada kilichokusukuma kuandika maoni yako hasa kumsafisha mzee ruksa! jua hii ni Tanzania na wote tuwe na lengo la kuijenga!
 
Na mimi nasubiri kumwaga sifa zangu baada ya kuona rasimu ya katiba mpya. Lakini before then, naomba nifunge mdomo wangu kwani sipendi kuja kulazimika kumeza maneno yangu kwa aibu huko baadae.

Namuombea Mungu amwongoze Warioba ajue jukumu kubwa alilokabidhiwa na wananchi wa Tanzania na asikubali kuchakachuliwa na wale wasioipendea mema nchi yetu na watu wake.

Mh Warioba, tunaomba katiba kwa ajili yetu na kwa manufaa ya vizazi vijavyo miaka mia kadhaa. Sisi tutakupa yetu maoni na tunaomba uyazingatie.
 
Jazba hazijengi, maelezo yako yanajitosheleza kiasi cha kumshawishi mtu kuwa we ni muelewa, lakin mambo ya kukurupuka, kuropoka na mengine, nahisi una kitu kingine cha ziada kilichokusukuma kuandika maoni yako hasa kumsafisha mzee ruksa! jua hii ni Tanzania na wote tuwe na lengo la kuijenga!

Ni kweli kabisa kuna kitu kingine kwa mimi kuandika hivyo na hicho kitu kingine ni ukweli kwamba jamaa mleta hoja alikrupuka. Kama si kukurupuka utasemaje Warioba alipigwa chini wakati serikali iliyochaguliwa ilikuwa ni mpya na si kwamba aliondolewa kwenye serikali ya kwanza iliyomaliza muda wake.

Hata kindergarten ambaye hajui kilimtokea nini Warioba ukishamfafanulia hivi basi anakuwa na uhakika kwamba serikali ilikuja mpya na mawaziri wengi tu.

Political appointment inaisha pale muda wa political cabinet unapo-expire. Ikishakuwa hivyo tutarajie sura mpya kabisa. Fungua kitabu cha Nyerere kiitwacho UONGOZI WETU NA HATIMA YA TANZANIA. Nyerere amefafanua jinsi alivyomueleza Kawa nia ya kumleta Waziri Mkuu mpya. Kawawa mwenyewe akashiriki kumpendekeza Sokoine.

Nimelipinga kwa nguvu hili kwa sababu watu wanataka kupindisha historia kwa jazaba au ujinga wao. Hili halitokei kwa Warioba tu. Bali hata kuondoka kwa Sokoine ni kwamba baada ya uchaguzi wa November 1980, Nyerere hakumteua tena Sokoine bali alimteua Cleopa Msuya.

Hivyo, hakuna tofauti na kilichotokea kwa Sokoine ile November 07, 1980 na kilichotokea kwa Joseph Warioba November 07, 1990 yaani miaka kumi kamili baadaye.

Kwa kifupi kilicholeta Premiers wapya bada ya Sokoine (1980) na Warioba (1990) ni uchaguzi na si utendaji.

Hatuhitaji tetesi za uchochoroni anazopenda Kimbunga maana Kimbunga anadhani tetesi ni zake tu anazotuletea na anazotaka tuamini kumbe unaweza hata kuanzisha thread mia za mashindano ya tetesi.

Kukurupuka ni kukurupuka tu. Kuropoka ni kuropka tu. Kila mtu anahaki ya kutumia neno kukurupuka au kuropoka maadamu tu yanaelekezwa kwa mtu aliyekurupuka au kuropoka kweli kama Nyerere alivyokuwa akitumia neno mpumbavu kwa mtu aliyekuwa ameonyesha upumbavu kweli. Ni maneno yaliyomo kwenye dictionary za lugha zote na hivyo yanajenga na wala si kubomoa!
 
chamakh,

..kifungo kinacholazimisha waziri mkuu ateuliwe toka miongoni mwa wabunge waliochaguliwa majimboni kiliingizwa kwenye katiba baada ya John Malecela kuteuliwa kuwa waziri mkuu.

Ni kweli kabisa. Hata kifungu cha Waziri Mkuu kuthibitishwa na Bunge kiliingizwa wakati tayari Malecela ni PM. Cleopa Msuya akawa Waziri Mkuu wa kwanza kupatikana kwa njia hii November 05, 1994. Siku ambayo pia cheo cha Unaibu Waziri Mkuu kilifutwa (deposed) baada ya Lyatonga Mrema kuhamishiwa Ministry of Youth and Labour.

Labda kwa kukumbusha ni kwamba yote haya yalitokea wakati wa Malecela ni kwa sababu miaka miwili baada ya premiership ya Malecela yaani 1992, ikaja Sheria ya vyama vingi. Hivyo mabadiliko hayo yalikuwa kujiandaa kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi.

..kumbuka kwamba Malecela alishindwa ubunge halafu akateuliwa mkuu wa mkoa, baadaye balozi/high commisioner Uingereza, halafu waziri mkuu na makamu wa kwanza wa raisi.

Ubunge alioshindwa ni ule wa mwaka 1985 yaani miaka mitatu baada ya kuwaambia wananchi kwamba wanaodai usafiri wa reli ni mbovu yeye kama Waziri wa Masiliano anawaambia "they can go to hell".

Hivyo, dakika anachaguliwa kuwa Prime Minister alikuwa ni High Commisioner London kama ulivyoeleza na hakuwa mbunge.
 
Crucifix
Nikupateje
Kimbunga

Naomba niwakumbushe ya kuwa yawezekana Mwinyi alimpiga chini Warioba kutokana na utendaji duni wake lakini sababu kuu ya kupigwa chini ni kutokana na katiba yetu. Kama mnakumbuka ni kuwa 1.mwaka 1990 Warioba alipoteza Jimbo la Bunda kwenye uchaguzi mkuu na inadaiwa Nyerere alichangia Warioba kukosa ubunge na kama sikosei ubunge ulienda kwa Stephen Wassira. Sasa kwa mujibu wa Katiba yetu ni kuwa Waziri MKuu lazima ateuliwe miongoni mwa wabunge wa kuchaguliwa majimboni na Warioba alishashindwa jimboni kwake, automatically akakosa sifa kikatiba kuwa waziri mkuu, isipokuwa alichaguliwa kuwa mbunge wa taifa na kuteuliwa kuwa waziri wa TAMISEMI.

Kuhusu uadilifu, hilo sina uhakika nao ila wote twajua stori kuwa jamaa alikuwa mlevi sana hivyo yaweza kuwa 2.hakuwa mwizi ila alikuwa mzembe sana

1. Jimbo alipoteza 1995
2. Heri ya hayo.........kuliko mwizi (we hunywi?)
 
credibility kivipi.... effectiveness nayo imo kwenye credibility?

Credibility inaweza kutafsriwa kama ushawishi chanya kwa umma kuamini unachokisema au kufanya; ushawishi huu hujengwa kwa maneno na matendo yanayozingatia maadili katika jamii husika. Sasa kwa kuwa hakuna mtu asiye na kasoro zake, mengine kama ya kunywa gongo tunayapotezea. Tunakazia kwenye wizi na uongo. Warioba is credible katika muktadha huu.
 
Back
Top Bottom