Tatizo Waislam wamekuwa watu wakutumiwa sana...kama Toilet paper vile ndo maana kila kitu huwa kinaelekezwa kwao.
NiKWELI kabisa, waislam wametumiwa saana kwa maslahi ya kisiasa na CCM. Kumbukumbu zinaonesha kwamba udini ulianza kutumiwa na CCM kupitia serikali yake na makada wake tangu mfumo wa vyama vingi uingie nchini. mathalan, chama cha CUF kilipakaziwa sana kuhusu udini. CCM wakafanikiwa katika hilo.
Waislam wamebaki kulewa kasumba hizo za udini toka CCM. Katika kampeni za udini wanamagamba wanajifanya wanajali sana maslahi ya waislam na haki zao.
CHA AJABu, waislam wanapoipelekea serikali ya CCM madai yao,
wakidhani CCM wameokoka, wacha Mungu wenye kujali uislam na waislam,hugeuziwa kibao na kusimangwa wakaonekana kuwa ni wachochezi, wasioridhika, washari, mazuzu wa kuigaiga uhafidhina wa kiislam, wasiojua dini yao na vitabu vyao, kwa maana nyingine huonekana maamuma.
Waislam wajue kuwa wanatumiwa tu. Udini, ukabila, ufisadi ni sera rasmi za CCM. Ufisadi umewaathiri watanzania wote. Ila waislam wameathirika zaidi.
Hembu tafiti, watuhumiwa wakuu wa ufisadi, waislam wako wangapi na wakristo wako wangapi. Jiulize walionunua viwanda vyetu na kuvichukua kuwa mali za familia zao. waislam ni wangapi. Wenye hisa Voda, Tigo wangapi ni waislam? TUAMKE, tusitumiwe kama toilet paper!!