Waraka wangu kwa ACT - WAZALENDO

Mkandara

JF-Expert Member
Mar 3, 2006
15,772
8,958
Siku ya leo imenipa mwanga mkubwa juu ya chama hiki baada ya kusoma tamko la chama ACT – Wazalendo juu ya maamuzi ya bodi ya wakurugenzi wa MCC kusitisha mahusiano na Tanzania. Kusema kweli imenishangaza sana chama kinachojinasibisha kama chama cha UJAMAA kimekiuka nguzo zake kuu kwa sababu tu ya mtazamo na maamuzi ya viongozi wake.


Kwanza lablda niseme hivi UJAMAA ni imani, imani ya kwamba Undugu na Umoja wetu ndio nguzo yetu ya maendeleo na kwamba hakuna mgeni anayeweza kutuletea maendeleo isipokuwa sisi wenyewe. Hii ni imani ambayo ndio haswa chimbuko la kudai UHURU wetu tusitawaliwe kiuchumi. Hatukuomba UHURU kwa sababu tulikuwa tumefungwa katika minyororo ama tulitengwa katika kupata haki za kibinadamu - Hapana. na haya ndio Castrol amekataa hadi jana akimwambia Obama kwamba - Hatuhitaji zawadi toka kwa MKOLONI. Maneno haya yanatokana na Imani sii swala la maskini jeuri!

Hivyo, hata sisi hatukuomba UHURU wa bendera, uhuru ambao kwamba mnajitawala wenyewe lakini bado mnatawaliwa Kiuchumi. Lengo kuu la Ujamaa ni kuondokana na kutawaliwa kiuchumi na ndio maana katika harakati za kujitawala kiuchumi ikazaliwa itikadi ya UJAMAA na KUJITEGEMEA inayokinzana na dhana ya kutawaliwa Kiuchumi na wakoloni, fikra hizo zikahamasisha wananchi wenyewe wachukue jukumu la kutaka kuendesha uchumi wa nchi zao kwa sababu wakoloni walikuja kukoloni nchi zetu sio kwa sababu walihitaji ardhi zaidi za kuishi wao, bali makoloni ya kuwekeza katika kukuza uchumi wa cnhi zao. Usipozingatia haya nawe ni msomi basi ndio katika maneno yale ya Nyerere alosema kwamba sio kila msomi ana akili wala sio kila mwenye akili ni msomi wengine ni wapuuzi tu!..WAPUUZI yaani IGNORANT! kama wale wanaohubiri Kuran na Biblia kumbe wanayoyafanya yao ni katika yale yaloharamishwa!

Sasa leo napo wasoma chama cha ACT –Wazalendo, chama ambacho kwamba nilidhani kweli ni WAJAMAA wamenipa mshtuko mkubwa sana kuona wapo tayari kukiuka principal zao kwa vipande vya rupia kutegemea misaada ambayo ndio msingi mkuu wa kutawaliwa kiuchumi. Sii Marekani, Jumuiya ya nchi za Ulaya wala Canada zinazoweza kutoa misaada pasipo kutazama kwanza interest zao na sidhani kama kuna mmoja wa viongozi wa ACT anafahamu interest za Marekani ama hiyo taasisi ya MCC zaidi ya kwamba wanatusaidia! Wanachokifahamu ni vitu gani wanavyotusaidia pasipo kujua, wao wananufaika na vitu gani toka kwetu? Hilo moja!

Pili, sidhani kama viongozi wa ACT wanafahamu undani wa itikadi hii inapofikia wao kutetea mashirika makubwa yanayoendesha uchumi wa nchi hizi kuwa msingi wa kujinufaisha wao kimaendeleo. Ujamaa (Socialism) kwa mapana yake ni falsafa inayopinga mapokezi ya mashirika makubwa kutawala uchumi wa nchi dhidi ya walio wengi. Nchi zetu bado zikipigana kuupata Uhuru wa kiuchumi, wakati nchi za magharibi ambazo tayari wamejitawala kiuchumi vyama vyao vya kijamaa vimejikita kupambana na wakoloni wa ndani ambayo ndio haya mashirka makubwa kutawala uchumi wa nchi zao yakiwaacha wananchi walio wengi maskini. Kwa hiyo ukoloni haukuwa nje tu hadi ndani mwao kuna Ukoloni. Leo unapotetea nchi kama marekani inayotujmia taasisi kama MCC kututawala kiuchumi wakatuletea makampuni kama Halliburton na Symbion nchini mnadhani hatutakuwa na matatizo ya kisiasa kwa kusimika vibaraka wake ili wanufaike kwa mafuta na gas!

Hivi kweli kwa akili zenu mnafikiri Marekani wanajali nani atakuwa rais wa Zanzibar kupitia kura za wananchi? Basi kama wangekuwa wazuri hivyo wa demokrasia wangekubali matokeo ya Misri, Palestina au hata Iraq katika uchaguzi mkuu ulopita! Kwa nini Marekani hao hao walikuwa against vyama vilivyoshinda na katika uchaguzi halali kabisa! It all comes to their Interest! Na Tanzania kwa utajiri tulokuwa nao lazima watatuchafua kama walivyoweza kuzibomoa nchi nyingine toka Russia, Somalia, Iraq, Libya, Sudan na sasa Syria! Utajiri wa Mafuta na gas tulokuwa nao kama hatutatumia AKILI zetu basi itakuwa laana kwetu.

Kama mnakumbuka Ufaransa waliiwekea vikwazo Rwanda miaka 14 ilopita baada ya uchaguzi wa Kagame ati anakiuka haki za binadamu na wala sio kwa sababu Kagame alikuwa dikteta mbaya sana kuliko kina Yahya Jammeh wa Gambia ama Obiang Mbasogo wa Equatorial Guinea ambao wamekubatiwa na Ufaransa miaka yote isipokuwa kwa sababu Kagame hakuna katika hesabu zao zakutawaliwa Kiuchumi. Na hata hawa Marekani miaka 7 ilopita nao wakamwekea vikwazo Utawala wa Kagame kwa kigezo kile kile cha haki za binadamu.

Nani leo anaweza kuinyooshea kidole Rwanda kwamba walipoteza mahusiano na nchi hizo! Rwanda imeteteleka kiuchumi ama ndio kwanza waliweza kutafuta mbinu zaidi ya kukuza umoja wao na kujitegemea wao wenyewe. Na hii ndio dhana ya vitisho wanayopenda sana kuitumia nchi za magharibi kutishia nchi maskini ambazo hadi leo wana Uhuru wa bendera tu hawajaweza kujitawala kiuchumi. Na hii ndio kazi kubwa ya wanasiasa wetu wanapotangaza siasa ya UJAMAA kwa maana pana zaidi ni kuikomboa nchi kutoka katika mizizi ya kutawaliwa kiuchumi.


Leo, ACT – Wazalendo kwa mapenzi yao ya Upinzani pasipo kujali misingi ya kiimani na kufuata kile wanachohubiri wamekuwa wa kwanza kupigania misaada ambayo kwanza binafsi sioni manufaa yake zaidi ya kuliweka taifa letu ktk lindi kubwa zaidi la Utegemezi. Hivi kweli tunashindwa kujenga barabara zetu hadi tutegemee misaada ya MCC ilihali usafiri ni miundombinu ya kwanza kabisa katika maandalizi ya kujitegemea kiuchumi.

Kuhusu Umeme, ni vyanzo vipi MCC wametuwezesha zaidi ya wao kutuletea Richmond na sasa Symbion ambayo inatukamua hadi tone la mwisho! Hata hiyo kusambaza Umeme vijijini hao MCC wapo Tanzania miaka mingapi ilopita kiasi kwamba leo ni asilimia chini ya 30 tu ndio wana umeme majumbani? Umeme wenyewe wa mgao na magenerata wakituuzia mafuta! Kweli tulihitaji na bado tunahitaji fedha za MCC tu kusambaza umeme nchini wakati hatuna vyanzo vyetu wenyewe vya kudumu! wao ndio wazalishaji umeme na wao ndio wanatusaidia kusambaza.. Mchumi yeyote ataiona faida inamlenga nani?

Nikirudi katika swala la Uchaguzi wa Zanzibar, ACT mnao ushahidi gani wamshindi zaidi ya kwamba mnafuata mkumbo? CUF wenyewe walitangaza kwa uhakika ushindi wa majimbo 20 kati ya 50, na hata kama projection ilionyesha wazi Maalim Seif kashinda bado tunatakiwa kutazama sharia inasemaje. Tuache makosa na mapungufu yote yalotajwa na Jecha ambayo sote hatuna ushahidi wa kutosha tunafahamu wazi Maalim Seif alijitangaza mshindi mapema kabla ya kutangazwa inyume cha sharia! Hili pekee ilitakiwa kufufuta Uchaguzina pengie ushindi apewe Shein, lakini Jecha na ZEC wakatafuta sababu nyingine za kufuta uchaguzi.

Sasa hatuwezi kupuuza sharia ambayo sote tunaijua kwamba Maalim Seif alikiuka tukamjengea hema la kutaka mshindi atangazwe kwa sababu tu tunaamini Maalim Seif alishinda na tunataka CCM itolewe madarakani. Na tunashindwa kujiuliza kwanini Maalim Seifalijitangaza wakati anajua sharia za uchaguzi? Kwa kuhofia CCM watachakachua? Sasa akijitangaza ndio ingeondoa uchakachuaji ama kupinga matokeo yoyote ambayo Jecha au ZEC ingetangaza. Binafsi yangu nitasema Jecha aliwashika mkono CUF kufuta matokeo ya uchaguzi laa sivyo kisheria Maalim Seif alitakiwa kuchukuliwa yeye hatua kali na iwe mfano kwa viongozi wengineo maaa Marekani na nchi zinazotumia mfumo wa wabunge wengi ndio hutangazwa mshindi kupitia hesabu ya kura zinavyohesabiwa na sii jukumu la Tume wala mwenyekiti kutangaza mshindi. Sisi tuna sharia zetu na tunafuata utaratibu wa Umaarufu kumpa mshindi na hakuna chombo chochote chenye mamlaka ya kutangaza wala kupinga matokeo yatakayo tangazwa na mwenyekiti. Sasa ikiwa mwenyekiti ana mamlka haya makubwa kabisa ambayo hata mahakama wala rais hana mamlaka ya kufuta matokeo aloyatangaza, ni nani mwenye mamlaka hayo kikatiba zaidi yake?

ACT – Wazalendo, achene hizi siasa za kutafuta umaarufu kupitia uchaguzi wa Zanzibar kwa sababu kuna makubwa zaidi ya kura unapoona nchi za magharibi zikijitwika mzigo! Wana lao jambo na hakika kesho yakijatokea ya kutokea mtajificha mbali kabisa na balaa litakalo wakumba wananchi na sii wa Zanzibar pekee bali balaa hilo lazima litavuka bahari na kuingia bara!
 
WanaJF,

Jana taifa limepata pigo kwa kukosa fedha za MCC takriban TZS 1.05Trillion ambazo zinatosheleza kujenga zahanati kata zote nchini, kuongeza kasi ya upatikanaji wa umeme hadi kufikia 57% ya kaya zote, kuweka maji kwenye vijiji vyote visivyo na maji nchini.

Kwanza kabisa masharti ya MCC hayakutolewa katikati ya mkataba bali yalikuwepo tangu awali wakati wa kupitishwa kwa MCC 1 kwamba serikali itapewa fedha hizo endapo itadumisha demokrasi, haki za binadamu, utawala bora, Utawala wa Kisheria, uwazi, nk. Hivyo MCC walivyoona baadhi ya vipengele (utawala wa sheria na Haki za binadamu) MCC waliwakumbusha serikali ya CCM kuhusu ukiukwaji huo unaoweza kuikosesha sifa ya kupewa msaada huo na wakapewa muda wa kufanya marekebisho.

swali nimejiuliza kwa nini tumekosa fedha hizo? majibu Yake????????

SUALA LA ZANZIBAR
Tume ya uchaguzi Znz ni huru kama inavyosemekana maamuzi yake hayaingiliwi na mamlaka yoyote (URT ama SMZ).

Lakini pili tume ni taasisi na maamuzi yake lazima yafuate utaratibu wa kitaasisi yaani Board/committee ikae na kufikia maamuzi yake kwa wajumbe wote kuafiki ama kutoafiki jambo hilo. Maajabu ni pale tume haikukaa kama taasisi badala yake familia moja ilifanya maamumuzi na kuyaita ya tume.

baada ya maamuzi hayo tulitegemea mamla za juu kumchukulia sheria mtendaji huyo. Hata hivyo tulitegemea mamlaka za juu zingechukua hatua kwa ukiukaji huo mkubwa wa kisheria aidha kwa kumwajibisha mhusika na kuendelea na mchakato ama kumuondoa kwenye nafasi hiyo na kuitisha uchaguzi mpya, badala yake yote hayakufanyika

Kwa mujibu wa Tume mtu yeyote atakayezuia mchakato wa uchaguzi kabla, wakati ama baada ya upigaji kura lazima sheria ichukue mkondo wake kama ilivyokua kwenye sheria ya Mita 100+. Tulitegemea Tume ya Zanzibar ingechukua hatua kwa wale wote aliyehujumu uchaguzi wa Zanzibar na kufanya uchaguzi huo ufutwe na tuambiwe jinsi walivyoharibu uchaguzi huo hadi leo hakuna wala mamlaka za juu hazijachukua hatua.

Leo MCC wamesema hawatupi hela tunasema wametupa masharti magumu, Kweli kuna ugumu wowote kwenye sheria tulizojitungia wenyewe? Hivyo basi:

Kwa nini Jecha Salum Jecha asiwaombe watanzania wote radhi kwa maamumuzi yake yaliyopelekea familia zaidi ya million 3 kuendelea kuteseka kwa maamuzi aliyoyafanya bila kushirikisha tume nzima?

Kwa nini Jecha Salum Jecha asijiuzulu sasa hata kama alishinikizwa iwe ni uwajibikaji kwa maamuzi yake (bila kujali yalikua sahihi ama la)?


Sheria ya Makosa ya Mtandao


Wakati wa upitishaji wa sheria hii mengi yalisemwa na wadau wengi hasa ule utaratibu wa kupelekea kwa dharura, maudhui ya mswaada na utaratibu uliotumika kuupitisha. sio tu ulilalamikiwa na wabunge wa upinzani bali vyombo vya habari, mashirika ya haki za binadamu, wanasheria n.k lakini bado wanaccm walipitisha kwa kauli moja Ndiooooooooo

Kama hiyo haitoshi mwenyekiti wa CCM ambaye wakati huo alikua Rais wa Jamhuri alisaini mswaada huo na kuwa sheria ambayo leo hii imeusababishia umma wa Tanzania kukosa fedha kiasi cha familia zaidi ya 3miilion zitateseka kwa maamuzi hayo. Hivyo basi

Je kwa nini Mwenyekiti wa CCM asijiuzulu kwa maamuzi yake hayo aliyoyafanya akiwa Rais bila kujalisha alikua na nia njema au la maana hizi kaya zaidi ya 3million ni pamoja na wanachama wa vyama mbalimbali na hata ccm na wasio na vyama. watu hao ndio waliopigia CCM kura leo hii wameambulia kunyimwa haki yao

Kwa nini wanaccm hasa wale wabunge waliopitisha mswaada huo wakiongozwa na aliyekuwa spika wa Bunge wasiombe radhi watanzania kwa maamuzi yao hayo?

Kwa nini uongozi mzima wa CCM Taifa wasiombe radhi watanzania kwa kuwa na serikali isiyo sikivu na ikiwezekana wajiuzulu nafasi zao kwa serikali yao kushindwa kutimizia matakwa ya wananchi

Kuwajibika kisiasa sio dhambi wala aibu ni ukomavu wa kisiasa, ni utu, ni heshima kwa wale uliokuwa unawatumikia na kuonyesha kuwajali. Lakini kubwa zaidi ni uwajibikaji kwa unaonesha kwa hali ya juu kabisa kuwajibika kwa maamuzi mtu aliyoyafanya wakati akiwa kiongozi
 
Mkandara si urudi huku ufanye hizo siasa za Ujamaa na Kujitegemea. Canada unafanya nini?
Mkuu nimejifunza zaidi Ujamaa huku baada ya kujiunga na NDP, Nimeshiriki sana katika kampeni zao niki volunteer kumpitisha mbunge wetu wa Jimbo la Spadina mama Olivia Chow toka mwaka 2000, hivyo nachoweza kusema imani yangu katika Ujamaa haina mahala wala nchi bali nitaendelea kuitetea mahala popote..
 
Tuache makosa na mapungufu yote yalotajwa na Jecha ambayo sote hatuna ushahidi wa kutosha tunafahamu wazi Maalim Seif alijitangaza mshindi mapema kabla ya kutangazwa kinyume cha sharia! Hili pekee ilitakiwa kufufuta Uchaguzi na pengie ushindi apewe Shein, lakini Jecha na ZEC wakatafuta sababu nyingine za kufuta uchaguzi.
Mkandara, soma vitu vyako kabla ya kuandika.
 
Mkandara kabla hatujafika mbali unaweza kutuwekea hiyo sharia inayompa madaraka ya Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi kufuta matokeo yote pale mgombea urais iwapo atajitangaza?

Pia kama Seif alijitangaza iweje
na matokeo ya wawakilishi yafutwe kwa kosa gani na kwa sharia ipi?
 
Mkandara kabla hatujafika mbali unaweza kutuwekea hiyo sharia inayompa madaraka ya Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi kufuta matokeo yote pale mgombea urais iwapo atajitangaza?

Pia kama Seif alijitangaza iweje
na matokeo ya wawakilishi yafutwe kwa kosa gani na kwa sharia ipi?
Nimesema hivyo au nilisema CUF imebebwa? maana kisheria Maalim Seif alitakiwa kuhukumiwa yeye kwa kosa hilo na hili lingeleta madhara zaidi badala yake kapewa nafasi nyingine ya kugombea upya!.. Sasa wewe niwekee ibara ya sheria inayomkataza Jecha kufuta matokeo halafu tuendelee!
 
Siku ya leo imenipa mwanga mkubwa juu ya chama hiki baada ya kusoma tamko la chama ACT – Wazalendo juu ya maamuzi ya bodi ya wakurugenzi wa MCC kusitisha mahusiano na Tanzania. Kusema kweli imenishangaza sana chama kinachojinasibisha kama chama cha UJAMAA kimekiuka nguzo zake kuu kwa sababu tu ya mtazamo na maamuzi ya viongozi wake.


Kwanza lablda niseme hivi UJAMAA ni imani, imani ya kwamba Undugu na Umoja wetu ndio nguzo yetu ya maendeleo na kwamba hakuna mgeni anayeweza kutuletea maendeleo isipokuwa sisi wenyewe. Hii ni imani ambayo ndio haswa chimbuko la kudai UHURU wetu tusitawaliwe kiuchumi. Hatukuomba UHURU kwa sababu tulikuwa tumefungwa katika minyororo ama tulitengwa katika kupata haki za kibinadamu - Hapana. na haya ndio Castrol amekataa hadi jana akimwambia Obama kwamba - Hatuhitaji zawadi toka kwa MKOLONI. Maneno haya yanatokana na Imani sii swala la maskini jeuri!

Hivyo, hata sisi hatukuomba UHURU wa bendera, uhuru ambao kwamba mnajitawala wenyewe lakini bado mnatawaliwa Kiuchumi. Lengo kuu la Ujamaa ni kuondokana na kutawaliwa kiuchumi na ndio maana katika harakati za kujitawala kiuchumi ikazaliwa itikadi ya UJAMAA na KUJITEGEMEA inayokinzana na dhana ya kutawaliwa Kiuchumi na wakoloni, fikra hizo zikahamasisha wananchi wenyewe wachukue jukumu la kutaka kuendesha uchumi wa nchi zao kwa sababu wakoloni walikuja kukoloni nchi zetu sio kwa sababu walihitaji ardhi zaidi za kuishi wao, bali makoloni ya kuwekeza katika kukuza uchumi wa cnhi zao. Usipozingatia haya nawe ni msomi basi ndio katika maneno yale ya Nyerere alosema kwamba sio kila msomi ana akili wala sio kila mwenye akili ni msomi wengine ni wapuuzi tu!..WAPUUZI yaani IGNORANT! kama wale wanaohubiri Kuran na Biblia kumbe wanayoyafanya yao ni katika yale yaloharamishwa!

Sasa leo napo wasoma chama cha ACT –Wazalendo, chama ambacho kwamba nilidhani kweli ni WAJAMAA wamenipa mshtuko mkubwa sana kuona wapo tayari kukiuka principal zao kwa vipande vya rupia kutegemea misaada ambayo ndio msingi mkuu wa kutawaliwa kiuchumi. Sii Marekani, Jumuiya ya nchi za Ulaya wala Canada zinazoweza kutoa misaada pasipo kutazama kwanza interest zao na sidhani kama kuna mmoja wa viongozi wa ACT anafahamu interest za Marekani ama hiyo taasisi ya MCC zaidi ya kwamba wanatusaidia! Wanachokifahamu ni vitu gani wanavyotusaidia pasipo kujua, wao wananufaika na vitu gani toka kwetu? Hilo moja!

Pili, sidhani kama viongozi wa ACT wanafahamu undani wa itikadi hii inapofikia wao kutetea mashirika makubwa yanayoendesha uchumi wa nchi hizi kuwa msingi wa kujinufaisha wao kimaendeleo. Ujamaa (Socialism) kwa mapana yake ni falsafa inayopinga mapokezi ya mashirika makubwa kutawala uchumi wa nchi dhidi ya walio wengi. Nchi zetu bado zikipigana kuupata Uhuru wa kiuchumi, wakati nchi za magharibi ambazo tayari wamejitawala kiuchumi vyama vyao vya kijamaa vimejikita kupambana na wakoloni wa ndani ambayo ndio haya mashirka makubwa kutawala uchumi wa nchi zao yakiwaacha wananchi walio wengi maskini. Kwa hiyo ukoloni haukuwa nje tu hadi ndani mwao kuna Ukoloni. Leo unapotetea nchi kama marekani inayotujmia taasisi kama MCC kututawala kiuchumi wakatuletea makampuni kama Halliburton na Symbion nchini mnadhani hatutakuwa na matatizo ya kisiasa kwa kusimika vibaraka wake ili wanufaike kwa mafuta na gas!

Hivi kweli kwa akili zenu mnafikiri Marekani wanajali nani atakuwa rais wa Zanzibar kupitia kura za wananchi? Basi kama wangekuwa wazuri hivyo wa demokrasia wangekubali matokeo ya Misri, Palestina au hata Iraq katika uchaguzi mkuu ulopita! Kwa nini Marekani hao hao walikuwa against vyama vilivyoshinda na katika uchaguzi halali kabisa! It all comes to their Interest! Na Tanzania kwa utajiri tulokuwa nao lazima watatuchafua kama walivyoweza kuzibomoa nchi nyingine toka Russia, Somalia, Iraq, Libya, Sudan na sasa Syria! Utajiri wa Mafuta na gas tulokuwa nao kama hatutatumia AKILI zetu basi itakuwa laana kwetu.

Kama mnakumbuka Ufaransa waliiwekea vikwazo Rwanda miaka 14 ilopita baada ya uchaguzi wa Kagame ati anakiuka haki za binadamu na wala sio kwa sababu Kagame alikuwa dikteta mbaya sana kuliko kina Yahya Jammeh wa Gambia ama Obiang Mbasogo wa Equatorial Guinea ambao wamekubatiwa na Ufaransa miaka yote isipokuwa kwa sababu Kagame hakuna katika hesabu zao zakutawaliwa Kiuchumi. Na hata hawa Marekani miaka 7 ilopita nao wakamwekea vikwazo Utawala wa Kagame kwa kigezo kile kile cha haki za binadamu.

Nani leo anaweza kuinyooshea kidole Rwanda kwamba walipoteza mahusiano na nchi hizo! Rwanda imeteteleka kiuchumi ama ndio kwanza waliweza kutafuta mbinu zaidi ya kukuza umoja wao na kujitegemea wao wenyewe. Na hii ndio dhana ya vitisho wanayopenda sana kuitumia nchi za magharibi kutishia nchi maskini ambazo hadi leo wana Uhuru wa bendera tu hawajaweza kujitawala kiuchumi. Na hii ndio kazi kubwa ya wanasiasa wetu wanapotangaza siasa ya UJAMAA kwa maana pana zaidi ni kuikomboa nchi kutoka katika mizizi ya kutawaliwa kiuchumi.


Leo, ACT – Wazalendo kwa mapenzi yao ya Upinzani pasipo kujali misingi ya kiimani na kufuata kile wanachohubiri wamekuwa wa kwanza kupigania misaada ambayo kwanza binafsi sioni manufaa yake zaidi ya kuliweka taifa letu ktk lindi kubwa zaidi la Utegemezi. Hivi kweli tunashindwa kujenga barabara zetu hadi tutegemee misaada ya MCC ilihali usafiri ni miundombinu ya kwanza kabisa katika maandalizi ya kujitegemea kiuchumi.

Kuhusu Umeme, ni vyanzo vipi MCC wametuwezesha zaidi ya wao kutuletea Richmond na sasa Symbion ambayo inatukamua hadi tone la mwisho! Hata hiyo kusambaza Umeme vijijini hao MCC wapo Tanzania miaka mingapi ilopita kiasi kwamba leo ni asilimia chini ya 30 tu ndio wana umeme majumbani? Umeme wenyewe wa mgao na magenerata wakituuzia mafuta! Kweli tulihitaji na bado tunahitaji fedha za MCC tu kusambaza umeme nchini wakati hatuna vyanzo vyetu wenyewe vya kudumu! wao ndio wazalishaji umeme na wao ndio wanatusaidia kusambaza.. Mchumi yeyote ataiona faida inamlenga nani?

Nikirudi katika swala la Uchaguzi wa Zanzibar, ACT mnao ushahidi gani wamshindi zaidi ya kwamba mnafuata mkumbo? CUF wenyewe walitangaza kwa uhakika ushindi wa majimbo 20 kati ya 50, na hata kama projection ilionyesha wazi Maalim Seif kashinda bado tunatakiwa kutazama sharia inasemaje. Tuache makosa na mapungufu yote yalotajwa na Jecha ambayo sote hatuna ushahidi wa kutosha tunafahamu wazi Maalim Seif alijitangaza mshindi mapema kabla ya kutangazwa inyume cha sharia! Hili pekee ilitakiwa kufufuta Uchaguzina pengie ushindi apewe Shein, lakini Jecha na ZEC wakatafuta sababu nyingine za kufuta uchaguzi.

Sasa hatuwezi kupuuza sharia ambayo sote tunaijua kwamba Maalim Seif alikiuka tukamjengea hema la kutaka mshindi atangazwe kwa sababu tu tunaamini Maalim Seif alishinda na tunataka CCM itolewe madarakani. Na tunashindwa kujiuliza kwanini Maalim Seifalijitangaza wakati anajua sharia za uchaguzi? Kwa kuhofia CCM watachakachua? Sasa akijitangaza ndio ingeondoa uchakachuaji ama kupinga matokeo yoyote ambayo Jecha au ZEC ingetangaza. Binafsi yangu nitasema Jecha aliwashika mkono CUF kufuta matokeo ya uchaguzi laa sivyo kisheria Maalim Seif alitakiwa kuchukuliwa yeye hatua kali na iwe mfano kwa viongozi wengineo maaa Marekani na nchi zinazotumia mfumo wa wabunge wengi ndio hutangazwa mshindi kupitia hesabu ya kura zinavyohesabiwa na sii jukumu la Tume wala mwenyekiti kutangaza mshindi. Sisi tuna sharia zetu na tunafuata utaratibu wa Umaarufu kumpa mshindi na hakuna chombo chochote chenye mamlaka ya kutangaza wala kupinga matokeo yatakayo tangazwa na mwenyekiti. Sasa ikiwa mwenyekiti ana mamlka haya makubwa kabisa ambayo hata mahakama wala rais hana mamlaka ya kufuta matokeo aloyatangaza, ni nani mwenye mamlaka hayo kikatiba zaidi yake?

ACT – Wazalendo, achene hizi siasa za kutafuta umaarufu kupitia uchaguzi wa Zanzibar kwa sababu kuna makubwa zaidi ya kura unapoona nchi za magharibi zikijitwika mzigo! Wana lao jambo na hakika kesho yakijatokea ya kutokea mtajificha mbali kabisa na balaa litakalo wakumba wananchi na sii wa Zanzibar pekee bali balaa hilo lazima litavuka bahari na kuingia bara!
Mkuu upo?
 
Mkandara, soma vitu vyako kabla ya kuandika.
Mkuu wangu unanijua mimi vizuri kuliko wengine humu huwa naandika yalokuwa kichwani na hufanya makosa mengi ya uandishi. Mimi sii mtaalam wa kuandika bado najifunza maana huwa na papara za kuweka mawazo yangu haraka najisahau hata kupitia nilichoandika kwanza hadi nikisha yatuma.

Hii ilitokana na mazoea ya kukuta tovuti inataka ni log in tena upya baada ya kuchukua muda mrefu na hivyo hupoteza kila kitu. Kwa hiyo kama kuna mahala unataka nikufahamishe vizuri nidokeze nitaiweka sawa ila sintofanya marekebisho kwa sasa.
 
Mkandara eti anaamini kwa kuwa Maalim Seif alijitangaza, basi ni halali kwa uchaguzi kufutwa, Hii uliiona wapi mzee?

Kilichotakiwa kufanyika ni kwa Maalim kufunguliwa mashitaka ya kujitangaza, akini wakati huohuo Tume iwe inaendelea kutangaza matokeo, siyo kuyafuta.

Na kuhusu Ujamaa, Hata Nyerere ambaye ndiye Muasisi wa Ujamaa nchini alikuwa akitafuta misaada kwa nchi rafiki kama vile Urusi, China hata Marekani yenyewe.

Kuhusu MCC tulisaini wenyewe masharti yake likiwemo Demokrasia, Sasa tusianze kuwaona eti ni wakoloni kwa wao kusimamia masharti yale.

Nimkumbushe Mkandara, Hata Dawa za Ukimwi za ARV nazo ni msaada wa wamarekani, Je Mkandara unataka na msaada huo ACT wazalendo waupinge ili kuthibitisha imani yao ya Ujamaa?

Mkandara anachanganya vitu viwili, UJAMAA na KUJITEGEMEA, hizi ni concepts mbili tofauti!. Unaweza kuwa mjamaa na bado ukawa hujafikia level ya kujitegemea, Unaweza kuwa Bepari na Ukawa level ya kujitegemea mfano Uingereza, Marekani, Ujerumani etc
 
Mkuu upo?
Nipo sana tu hupitia mara kwa mara ila sichangii sana baada ya kuona watu vigeugeu sana humu na hutafuta wachawi maana mengi niliwaasa humu kabla ya Uchaguzi mkuu na yametokea, sasa wameshapata mchawi ilihali kimazingira yanayokukuta mara zote hutokana na wewe mwenyewe hakuna mchawi!
 
Nipo sana tu hupitia mara kwa mara ila sichangii sana baada ya kuona watu vigeugeu sana humu na hutafuta wachawi maana mengi niliwaasa humu kabla ya Uchaguzi mkuu na yametokea, sasa wameshapata mchawi ilihali kimazingira yanayokukuta mara zote hutokana na wewe mwenyewe hakuna mchawi!
Kwahiyo nani mchawi?
 
Nimesema hivyo au nilisema CUF imebebwa? maana kisheria Maalim Seif alitakiwa kuhukumiwa yeye kwa kosa hilo na hili lingeleta madhara zaidi badala yake kapewa nafasi nyingine ya kugombea upya!.. Sasa wewe niwekee ibara ya sheria inayomkataza Jecha kufuta matokeo halafu tuendelee!
Siwezi quote andishi lako kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu.
Lakini kuna sehemu umeandika ..lakini Jecha na ZEC wajatafuta sababu nyingine za kufuta uchaguzi...swali hizo sababu ni zipi na sharia inasemaje kuhusu hizo sababu?

Pia nimekuuliza vp kuhusu wawakilishi wao kosa lao ni lipi?
 
Mkandara eti anaamini kwa kuwa Maalim Seif alijitangaza, basi ni halali kwa uchaguzi kufutwa, Hii uliiona wapi mzee?

Kilichotakiwa kufanyika ni kwa Maalim kufunguliwa mashitaka ya kujitangaza, akini wakati huohuo Tume iwe inaendelea kutangaza matokeo, siyo kuyafuta.

Na kuhusu Ujamaa, Hata Nyerere ambaye ndiye Muasisi wa Ujamaa nchini alikuwa akitafuta misaada kwa nchi rafiki kama vile Urusi, China hata Marekani yenyewe.

Kuhusu MCC tulisaini wenyewe masharti yake likiwemo Demokrasia, Sasa tusianze kuwaona eti ni wakoloni kwa wao kusimamia masharti yale.

Nimkumbushe Mkandara, Hata Dawa za Ukimwi za ARV nazo ni msaada wa wamarekani, Je Mkandara unataka na msaada huo ACT wazalendo waupinge ili kuthibitisha imani yao ya Ujamaa?

Mkandara anachanganya vitu viwili, UJAMAA na KUJITEGEMEA, hizi ni concepts mbili tofauti!. Unaweza kuwa mjamaa na bado ukawa hujafikia level ya kujitegemea, Unaweza kuwa Bepari na Ukawa level ya kujitegemea mfano Uingereza, Marekani, Ujerumani etc
Mkuu sijasema Kujitangaza kwa maalim Seif ndio sababu ya kufuta matokeo bali nimesema Jecha kambeba Maalim Seif pasipo yeye kujijua kwa sababu ilitakiwa Maalim Seif aadhibiwe yeye na pengine kufutwa ama kuzuiwa kabisa kugombea Urais. majuzi Uganda yule mgombea wa Upinzani aliswekwa ndani kwa sababu tayari alikuwa ameshaanza kutaka kujitangaza mshindi asisubiri Tume.

Maadam sheria yetu imewapa Tume mamlaka ya kutangaza mshindi na hakuna mtu wala chombo kingine kinachoweza kutangaza ni jukumu letu kufuata sheria laa sivyo mnajiondoa mapema kabla hata ya uchaguzi kwa sababu mnajua Tume itatangaza tu wanayemtaka ashinde!
Kama unakumbuka niliwaambia humu kuhusu Upinzani kutaka Uchaguzi kabla ya kuipata Katiba Mpya ni kosa mkasema hapana sio kosa CCM lazima waondoke. katiba mpya itapatikana baada ya UKAWA kuingia madarakani - Mmmmh! Nikasema tena kukazania serikali 3ni kosa kwa sababu kuna ibara zaidi ya 200 zinazotakiwa kupitishwa na muhimu zaidi mkasema hapana serikali 3 ni muhimu tunataka Zanzibar huru na Tanganyika Huru..Hayakuwa, haya sasa mnacholia lia nini?
 
Siwezi quote andishi lako kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu.
Lakini kuna sehemu umeandika ..lakini Jecha na ZEC wajatafuta sababu nyingine za kufuta uchaguzi...swali hizo sababu ni zipi na sharia inasemaje kuhusu hizo sababu?

Pia nimekuuliza vp kuhusu wawakilishi wao kosa lao ni lipi?
Unaniuiza mimi tena kumbe wakati wote unampinga Jecha hujui sababu alizozitaja? Bibie kweli tutaweza kujadili ya Jecha ikiwa wewe mwenyewe hujui alichosema Jecha kama sababu!

Na nimesema wazi huko nyuma tuache hizo sababu zao ambazo CUF wamedai ama Jecha kwa sababu hatuna ushahidi nazo mkononi isipokuwa kwa maneno yao tu. Nikawapeni sababu ambayo sote tunaijua na tulimuona Seif akijitangaza kabla ya tume na kwamba hii pekee ingemwondoa Maalim Seif ktk uchaguzi lakini Jecha akapotezea akatoa sababu nyinginezo ili uchaguzi urudiwe badala ya Maalim Seif kufutwa yeye!
 
Unaniuiza mimi tena kumbe wakati wote unampinga Jecha hujui sababu alizozitaja? Bibie kweli tutaweza kujadili ya Jecha ikiwa wewe mwenyewe hujui alichosema Jecha kama sababu!

Na nimesema wazi huko nyuma tuache hizo sababu zao ambazo CUF wamedai ama Jecha kwa sababu hatuna ushahidi nazo mkononi isipokuwa kwa maneno yao tu. Nikawapeni sababu ambayo sote tunaijua na tulimuona Seif akijitangaza kabla ya tume na kwamba hii pekee ingemwondoa Maalim Seif ktk uchaguzi lakini Jecha akapotezea akatoa sababu nyinginezo ili uchaguzi urudiwe badala ya Maalim Seif kufutwa yeye!

Sababu nyingi zipi hizo? Mie ninachofahamu Jecha alifuta uchaguzi kwa vile Maalim Seif alisema mwelekeo wa matokeo ulivyo..Sasa wewe unasema sababu nyingine nami nakuuliza ni zipi hizo?

Na je vp wawakilishi wao kosa lao ni lipi?
 
Sababu nyingi zipi hizo?
Well hatuwezi kujadili hili ikiwa wewe hujui sababu alizozisema Jecha kumbe unafuata mkumbo tu. hakuna sheria inayomkataza Jecha kufuta matokeo na hakuna sheria inayompa madaraka mtu yeyote hata rais aliyepo madarakani kutoa matokeo isipokuwa yeye. Hivyo ana mamlaka makubwa ambayo lazima uyatazame ktk sheria na kanuni za ZEC na sio katiba ya nchi.
 
Kuishi canada, haina maana ndo unajua kila kitu, nataka nikukumbushe kidgo sana labda umesahau ,nakumbuka wakati wa nyerere tulikua na mfumo wa ujamaa jee Niambie ni maendeleo gani tuliyapata, kama ckosei ilifika wakati ikawa tunakula chakula cha farasi (dona la njano ) je nchi Ukilianua kuingia katika mfumo wa kibepari tumeshawahi kula chakula cha farasi ?jibu bado, pili kama ckosei ni nchi 1 tu duniani ilotumia mfumo wa kijamaa ikapata maendeleo (China) kwa hyo ndugu yangu Nadhani siasa za ujamaa Tanzania hazitufai ukija TZ hizo siasa zako ziache canada
 
Kuishi canada, haina maana ndo unajua kila kitu, nataka nikukumbushe kidgo sana labda umesahau ,nakumbuka wakati wa nyerere tulikua na mfumo wa ujamaa jee Niambie ni maendeleo gani tuliyapata, kama ckosei ilifika wakati ikawa tunakula chakula cha farasi (dona la njano ) je nchi Ukilianua kuingia katika mfumo wa kibepari tumeshawahi kula chakula cha farasi ?jibu bado, pili kama ckosei ni nchi 1 tu duniani ilotumia mfumo wa kijamaa ikapata maendeleo (China) kwa hyo ndugu yangu Nadhani siasa za ujamaa Tanzania hazitufai ukija TZ hizo siasa zako ziache canada
sasa ikiwa wananchi wenyewe hamkujua UJAMAA ni wenu wenyewe kujiletea maendeleo unawezaje kumlaumu Nyerere ilihali wewe bado hujajikomboa kiakili bado mtumwa unayetaka kuletewa na Mzungu!..

Na hii imedhihirika hadi katika Ubepari bado watu mnataka kuletewa. sasa wewe nambie toka mmeingia Ubepari mmefaidika sana kutokula Ugali wa njano, mbona huku ndio Unapendwa zaidi! Labda nikuonyesha najua zaidi yako ni kwamba kile unachokiita chakula cha farasi ndio Dona la njano!

Nasikia siku hizi mmegundua Dona ndio mpango mzima au nasema uongo! Yaani ulichokuwa ukila ni unga wa mahindi ya njano ambayo hayakukobolewa. Pengine hujawahi kuona mahindi ya njano. na hakuna mfugaji yeyote Ulaya na Canada anayelisha farasi wake unga wa njano!

Pili, Nyerere alijenga reli ya Tazara, tulikuwa na viwanda vya nguo, ngozi hadi viatu, kiwanda cha kusafisha mafuta, viwanda vya kutengeneza matairi kifupi zaidi ya viwanda 3,000 leo viko wapi? JP Magufuli anaanza kazi upya kuvirudisha baadhi vilivyopo, leo hii sukari hadi mayai mnaagiza nje kutajirisha kina Manji, kama sio uvivu ni laana gani imewakuta!
 
Mkuu nimejifunza zaidi Ujamaa huku baada ya kujiunga na NDP, Nimeshiriki sana katika kampeni zao niki volunteer kumpitisha mbunge wetu wa Jimbo la Spadina mama Olivia Chow toka mwaka 2000, hivyo nachoweza kusema imani yangu katika Ujamaa haina mahala wala nchi bali nitaendelea kuitetea mahala popote..

Really ............. Siyo huo Ujamaa ndiyo uliokukimbiza Tanzania!!?
 
Back
Top Bottom