Waraka wa wazi kwa Freeman Mbowe

Waraka wa wazi kwa Freeman Mbowe

Joined
Jul 3, 2020
Posts
6
Reaction score
97
WARAKA WA WAZI KWA MWENYEKITI WA CHADEMA TAIFA
MH.FREEMAN A. MBOWE

Mh. Mwenyekiti pole na majukumu ya ujenzi wa demokrasia nchini, Zaidi pole sana na shughuli za uchaguzi zilizokoma takribani wiki nne zilizopita huku majeraha ya ukiukwaji mkubwa wa demokrasia, uvunjwaji wa haki za raia, ndugu zetu kuuwawa, kufungwa na viongozi wetu wakuu ikiwemo Mh. Lissu na Mh. Lema kuomba hifadhi za kisiasa ili kujinusuru wao na familia zao kutokana na utawala wa mkono wa chuma yakiwa bado hayajapona.

Mh Mwenyekiti umekuwa nguzo imara na kinara wa kuongoza mapambano ya kudai haki, demokrasia na maendeleo ya watu kwenye Taifa letu, navutiwa sana na umahiri, ujasiri, uvumilivu, utu, upendo, moyo wa kusaidia wengine na uongozi wako bora uliotukuka tangu kuasisiwa kwa misingi ya CHAMA chetu mwaka 1992.

Ukiwa kijana mdogo kabisa haikukuzia kuongoza kurugenzi ya vijana kwa ufanisi
kubwa chini ya mwenyekiti wa kipindi hicho mzee wetu Mh. Edwin Mtei ambae alikulea katika misingi imara ambayo vizazi vya leo na vijavyo vina chakujifunza na kujivunia.

Mh. Mwenyekiti nakuandika waraka huu nikiwa na huzuni isiyokoma tangu nisome taarifa za viongozi wa BAWACHA wakiongozwa na Mh. Halima Mdee kufanya maamuzi ya kwenda Bungeni kuapa kama Wabunge wa viti maalumu watokanao na CHADEMA huku nikiwa kwenye wimbi kubwa la sintofahamu kama maamuzi hayo yanabarka za chama au laa.

Kamati kuu ya Chama chetu mara zote imekuwa ikifanya maamuzi sahihi na muhimu kwa mustakabali wa Kuhami Demokrasia ya Taifa letu na Kamwe sijawahi kutilia shaka maamuzi ya kamati kuu iliojaa viongozi makini na wenye weledi, na hata mlipokutana na kuyakataa matokeo ya Uchaguzi mkuu wa mwaka huu ilikuwa ni sehemu ya maamuzi sahihi na muhimu sana kwani wananchi na wapenda mabadiliko walifurahishwa na maamuzi yale. Je! ni nini kimetokea?

Maamuzi yamebadilika? Kama hayajabadilika kuna viongozi ndani ya Chama wamekuwa
wakubwa kuliko Chama? Natumai hakuna na kamwe hatakuja kutokea.

Mh. Mwenyekiti ni kweli katibu wetu wa vijana Mh. Nusrat Hanje ametoka gerezani kutokana na juhudi zetu, na wingi wa kelele zetu? Hashaa! Mtawala alimuweka gerezani kinyume na utaratibu, kamtoa kinyume na utaratibu na kisha kamzawadia Ubunge kinyume na utaratibu. Sisi tuliojitofautisha kwa sera na itikadi natumaini tutafuata utaratibu kwa mujibu wa katiba kwa manufaa ya kesho ya Chama chetu

Mh mwenyekiti mwisho kabisa nimalize kwa kutoa ushauri wangu kwako na kwa CHAMA;

1. Natambua chama chetu ni miongoni mwa vyama vyenye intelijensia imara hivyo niombe hatua za haraka ziwe zinachukuliwa dhidi ya wale wote wanaopanga kuasi,kuhujumu,au kuzorotesha maamuzi ya chama kabla wao hawajachukua hatua
zitugharimuzo, kutukatisha tamaa na kuturudisha nyuma.

2. Wote walio kwenda kinyume na makubaliano ya KAMATI KUU wafutwe uanachama mara moja ili ku restore Imani ya wananchi kwa chama chetu, na pia maamuzi hayo. yataheshimisha dhamira ya mamia ya ndugu zetu waliouwawa, kuteswa na kutupwa
magerezani.

3. Chama kiunde mfumo wa kuchangia gharama za uendeshaji wa shughuli zake kwani wananchi kwa mapenzi mema wameonyesha wako pamoja na sisi na katu hawatakubali fedha zitokanazo na dhuluma,uonevu na damu za ndugu zetu.

4. Uhusiano mzuri wa wanachama ni ule tu unaoweka maslahi ya Taifa mbele na sio maslahi binafsi, na

5. Chama kiondoke katika fikra za mikakati na kisha kigeukie harakati za vuguvugu la kudai Katiba Mpya bila kuchoka hadi ipatikane, kwani ni wazi Demokrasia ya Vyama vingi haiwezi kutekelezeka chini ya KATIBA iliyoandaliwa mahususi kwa mfumo wa Chama
kimoja. Mh. Mwenyekiti mimi sio sehemu ya maamuzi kwenye chama lakini nilijifunza busara ni kutokunyamaza wala kutulia pale uyapendayo ukihisi yaenda mrama yapasa kusimama na kushauri, kama ulivyofanya mwaka 1995 pindi Mh. Edwin Mtei na Mh. Bob Makani walipogombea urais ndani ya CHAMA na baadae kuonekana kukubalika kwao na uimara wao watakipasua na kukigawanya CHAMA uliandika waraka kushauri kwamba WOTE wasigombee bali wamuunge mkono mgombea wa NCCR, ushauri ambao ulikuwa na tija na unatujenga mpaka leo hii. Mungu ibariki CHADEMA, Mungu Ibariki Tanzania.

Nakutakia Kheri na Maisha marefu yenye Furaha.

FREDRICK M. JUSTINE
 
Mwenyekiti sasahivi yupo busy kupiga mahesabu ya 1.5m zitakazokuwa zinaingia kila mwezi kwa hivyo vichwa 19 na 1m ya kichwa kimoja + Ruzuku.

Sidhani kama atapata muda wa kusoma huu Waraka wako.
 
Makamanda mtaandika sana hizo nyaraka ila ndio mjue kwenye ulingo wa kisiasa CCM ndio inaamua nani aingie bungeni na nani atoke !
 
Mwenyekiti sasahivi yupo busy kupiga mahesabu ya 1.5m zitakazokuwa zinaingia kila mwezi kwa hivyo vichwa 19 na 1m ya kichwa kimoja + Ruzuku.

Sidhani kama atapata muda wa kusoma huu Waraka wako.
Hivi ruzuku anaweza kuwa anakusanya kama ngapi kwa mwezi
 
Kijana unapoteza muda wako, nguvu zako na maarifa yako bure kumuandikia kiongozi ambae anaweka masilahi ya tumbo lake na familia yake mbele badala ya kutumikia wananchi. Ni afadhali muda huu, nguvu hizi na maarifa haya uliyotumia kuandikia uzi huu ungevitumia kuwafunza watoto wako kufanya homework hapo nyumban.

Tanzania hakuna chama cha upinzan au kiongozi wa upinzan ambaye yupo kwa ajili ya masilahi ya nchi au wananchi, wote wapo kwa ajili ya masilahi ya matumbo yao mfano michango ya wabunge iliyochangwa kwa takriban miaka 5 mpaka leo haijulikan ilipo na kwenye kampeni walichangisha zingine. Nimalize kwa kukupa pole mleta mada kwa kumuona mpiga dili ni mkombozi wako
 
Nawaonea huruma sana vijana wenzangu wanaosota jela/ rumande kwa makosa ya kujitoa kwao kusimamia harakati mbalimbali za CHADEMA.

rest in peace Alfonce Mawazo, Ben Saanane et al.
 
Mtoa mada anachelewa sana kuona mambo, anatakiwe afikirie nje ya box ili kuona na kupata majawabu .
 
Dhambi ya usaliti ni dhambi mbaya sana.

Sumu ni zile noti za Edo, halafu sasa mnyaturu kaja na mafaranga hataki mgawo na mzee wa sakosi, mzee akaanza mambo meusi zito akamwambia utang'ata mchanga, tembea na biti hilo, mzee wa sakosi akubali kupauka?

Usaliti ni mbaya sana.
 
Mkuu uchaguzi ulikuwa huru na wa haki. Hivi kwa andiko lako refu Hivi unataka kusema Lissu angemshinda JPM.? Kwani wewe maendeleo kwako Ni Nini. Unadhani Rais kazi yake Ni Nini hasa.

Je, umeshaishi nchi hizi zilizoendelea kuona maisha yalivyo. Unamwangalia JPM kama mwanachama wa CCM tu. Au Mtanzania anayebaki Ndani ya Chama kufanya mabadiliko Chanya kwa ajili ya Mtanzania.

Wakati wa kufikiria nchi yako, anza na mahitaji ya Mtanzania wa kawaida, Sio maslahi yako ya kiushabiki as if Tansania Ina Timu za simba na yanga tu.
 
Waraka mzuri kabisa. Naupeleka jwa Makene na Mnyika.
 
Back
Top Bottom