KennedyMmari
JF-Expert Member
- Dec 12, 2012
- 979
- 183
Ndugu zangu maofisa,waasibu, mameneja na wakurugenzi wa bodi ya mikopo ya Elimu ya juu nchini Tanzania (HESLB), poleni sana kwa kazi nzito mnayoifanya maana nimeota ndoto kuwa mara baada ya timu ya taifa kushindwa kufanya vizuri mmeazimia kulisaidia taifa katika kitengo hicho na ndoto inaonesha kuwa wiki jana tu mlikuwa Arusha katika uwanja wa Sheikh Amri Abed kusakata kabumbu, kuvuta kamba na kukimbiza kuku.
Lakini naomba ieleweke wazi hapa kuwa tatizo kwetu sisi watoto wa mafukara si kutaka kuhoji juu ya jitihada zenu za kukuza na kuendeleza vipaji vyenu au juu ya nia yenu njema ya kukuza na kuendeleza soka nchini ili siku moja Tanzania iweze kushiriki walau kombe la dunia hata kwa nafasi ya viti maalum, lakini maswali yetu sisi tusojua ladha ya utamu wa maisha ni kuwa:-
Je wakati mkipanda mabasi au hata ndege kwenda Arusha kwa kutumia kodi za Baba na Mama zetu wauza maparachichi kule Santilya Umalila Mbeya mlikuwa mnajua kuwa vyuoni kuna watoto wa mafukara wa mwaka wa kwanza ambao mpaka sasa tunaishi vyuoni kama kinda aliyekosa mama kwani tumekosa mahali pa kulala na hata chakula cha uhakika huku ikikumbukwa wazi kuwa wengi wetu.
Tulitoka kwetu Tandahimba Mtwara na kwingineko tukiwa na matumaini makubwa kuwa tungepata pesa ya kujikimu kutoka serikalini kwani hata kile tunachosoma kwa sasa tulikichagua kwa kuwa ndio kilikuwa na uwezekano wa kutufanya kupata mkopo ukilinganisha na kile kilichokuwa ndoto zetu.
Lakini pamoja na haya yote mlitunyima hicho mnachokiita mkopo na mkatutaka kusubiri majina ya banchi la kumi ambayo mpaka ninapoandika waraka huu bado hayajatolewa na ndio kwanza ninyi mpo Arusha kuonesha vipaji ambavyo sisi hatukuviona kwenu hapo awali.
Naam labda ni kupitiwa tuu na kujisahau kutokana na kiyoyozi cha ofisini kwenu magari ya kifahari na maisha bora ya familia zenu lakini naomba kuhoji, kwani mlipita njia gani kusafiri mpaka Arusha? njia ambayo hamkuona hata kijiji kimoja cha Tanzania na kuona huko mnapo paita bushi ambapo kiuhaalisia ndipo tulipo toka sisi watoto wa mafukara tulioomba mkopo kwa kutumia pesa za mahindi ya kuikimu.
Familia ambayo bibi yangu Shogoo aliamua kuyauzaa ili mimi nikanunue fomu yenu ya shilingi 30,000, nikahangaika sana kupata kibali cha kifo cha baba na mama yangu lakini nakumbuka nilishirikiana na rafiki yangu Tabu ambaye alikuwa amefiwa na Baba yake na kubakiwa na mama yake ambaye kwa sasa ni mgonjwa sana lakini bado mkanipa mimi asilimia 0% na yeye mmempaa TSH3,800 katika 1800,000 anayopaswa kulipa kwa mwaka mmoja wa masomo.
Tulipohoji juu ya kukata rufaa ili tuongezewe pesa mkatujibu kuwa tusubiri mpaka mtakapo kamilisha taratibu lakini kumbe taratibu zenyewe tunazosubiri mpaka sasa ni ninyi kurudi kutoka michezoni?
Samahani sana naomba kuuliza wakuu mlipofika Arusha hakuna hata mmoja wenu aliyezinduka na kukumbuka kuwa kuna watoto wa wakulima wa ndizi kutoka Matombo Morogoro Vijijini na sehemu kama hizo nchini ambao wapo mwaka wa pili na watatu sasa lakini waliomba mkopo miaka ya hapo nyuma na mliwanyima wakasoma kwa kuombaomba kama wakimbizi ndani ya nchi yetu na kwa mwaka wa masomo 2015/2016 imetugharimu TSH 30,000 nyingine tuliyokopa kwa mzee Msemwa na kuweka rehani kijumba chetu cha mbavu za mbwa kilichopo kijijini ili kuweza kuomba upya mkopo.
Na mpaka sasa mmetuambia tusubiri ili muweze kutupa mkopo katika kile mnachokiita banchi ya kumi lakini cha kusikitisha kumbe sisi tunasubiri kwa matumaini lakini ninyi mpo Arusha kwenye michezo ama kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaa.
MASWALI KUNTU YA KUJIULIZA HAPA NI JE?
Kulikuwa na umuhimu gani wa kufanya bonanza la michezo kwa kipindi hiki ambacho majina ya wanafunzi wanaonufaika na mkopo kwa mwaka wa kwanza yamechelewa kutolewa ikilinganishwa na miaka mingine ya masomo na mpaka sasa mchakato wa majina yao bado haujakamilika?
Kama michezo ni starehe, furaha na kufahamiana kulikuwa na umuhimu gani wa kuyafanya hayo katika kipindi hiki ambacho maisha ya maelfu ya watanzania kubaki ama kuondoka vyuoni yapo katika mikono yenu iliyo na mamlakaa juu ya hatima ya watanzania hawa?
MWISHO.
Sisi kama watoto wa mafukara ambao kimsingi ndio walipa kodi wa Tanzania tunaomba kupewa majibu ya wazi katika vyombo vyaa habari kuwa.
NI KWANINI MSICHUKULIWE HATUA KALI ZA KIUTENDAJI HASA KATIKA ZAMA HIZI ZA ?HAPA KAZI TUU?
PILI NAOMBA MUELEZE WAZI NI KWANINI MUHESHIMIWA RAIS DR. JOHN POMBE MAGUFULI ASIFANYE ZIARA YA GHAFLA KATIKA OFISI ZENU KESHO ASUBUHI?
?PAMBANA NA HOJA USIPAMBANE NA MTOA HOJA?
SHITINDI VENANCE ROLANDI, MWENYEKITI WA KAMATI YA MAWAZIRI WA MIKOPO TANZANIA. 0759704444.
Lakini naomba ieleweke wazi hapa kuwa tatizo kwetu sisi watoto wa mafukara si kutaka kuhoji juu ya jitihada zenu za kukuza na kuendeleza vipaji vyenu au juu ya nia yenu njema ya kukuza na kuendeleza soka nchini ili siku moja Tanzania iweze kushiriki walau kombe la dunia hata kwa nafasi ya viti maalum, lakini maswali yetu sisi tusojua ladha ya utamu wa maisha ni kuwa:-
Je wakati mkipanda mabasi au hata ndege kwenda Arusha kwa kutumia kodi za Baba na Mama zetu wauza maparachichi kule Santilya Umalila Mbeya mlikuwa mnajua kuwa vyuoni kuna watoto wa mafukara wa mwaka wa kwanza ambao mpaka sasa tunaishi vyuoni kama kinda aliyekosa mama kwani tumekosa mahali pa kulala na hata chakula cha uhakika huku ikikumbukwa wazi kuwa wengi wetu.
Tulitoka kwetu Tandahimba Mtwara na kwingineko tukiwa na matumaini makubwa kuwa tungepata pesa ya kujikimu kutoka serikalini kwani hata kile tunachosoma kwa sasa tulikichagua kwa kuwa ndio kilikuwa na uwezekano wa kutufanya kupata mkopo ukilinganisha na kile kilichokuwa ndoto zetu.
Lakini pamoja na haya yote mlitunyima hicho mnachokiita mkopo na mkatutaka kusubiri majina ya banchi la kumi ambayo mpaka ninapoandika waraka huu bado hayajatolewa na ndio kwanza ninyi mpo Arusha kuonesha vipaji ambavyo sisi hatukuviona kwenu hapo awali.
Naam labda ni kupitiwa tuu na kujisahau kutokana na kiyoyozi cha ofisini kwenu magari ya kifahari na maisha bora ya familia zenu lakini naomba kuhoji, kwani mlipita njia gani kusafiri mpaka Arusha? njia ambayo hamkuona hata kijiji kimoja cha Tanzania na kuona huko mnapo paita bushi ambapo kiuhaalisia ndipo tulipo toka sisi watoto wa mafukara tulioomba mkopo kwa kutumia pesa za mahindi ya kuikimu.
Familia ambayo bibi yangu Shogoo aliamua kuyauzaa ili mimi nikanunue fomu yenu ya shilingi 30,000, nikahangaika sana kupata kibali cha kifo cha baba na mama yangu lakini nakumbuka nilishirikiana na rafiki yangu Tabu ambaye alikuwa amefiwa na Baba yake na kubakiwa na mama yake ambaye kwa sasa ni mgonjwa sana lakini bado mkanipa mimi asilimia 0% na yeye mmempaa TSH3,800 katika 1800,000 anayopaswa kulipa kwa mwaka mmoja wa masomo.
Tulipohoji juu ya kukata rufaa ili tuongezewe pesa mkatujibu kuwa tusubiri mpaka mtakapo kamilisha taratibu lakini kumbe taratibu zenyewe tunazosubiri mpaka sasa ni ninyi kurudi kutoka michezoni?
Samahani sana naomba kuuliza wakuu mlipofika Arusha hakuna hata mmoja wenu aliyezinduka na kukumbuka kuwa kuna watoto wa wakulima wa ndizi kutoka Matombo Morogoro Vijijini na sehemu kama hizo nchini ambao wapo mwaka wa pili na watatu sasa lakini waliomba mkopo miaka ya hapo nyuma na mliwanyima wakasoma kwa kuombaomba kama wakimbizi ndani ya nchi yetu na kwa mwaka wa masomo 2015/2016 imetugharimu TSH 30,000 nyingine tuliyokopa kwa mzee Msemwa na kuweka rehani kijumba chetu cha mbavu za mbwa kilichopo kijijini ili kuweza kuomba upya mkopo.
Na mpaka sasa mmetuambia tusubiri ili muweze kutupa mkopo katika kile mnachokiita banchi ya kumi lakini cha kusikitisha kumbe sisi tunasubiri kwa matumaini lakini ninyi mpo Arusha kwenye michezo ama kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaa.
MASWALI KUNTU YA KUJIULIZA HAPA NI JE?
Kulikuwa na umuhimu gani wa kufanya bonanza la michezo kwa kipindi hiki ambacho majina ya wanafunzi wanaonufaika na mkopo kwa mwaka wa kwanza yamechelewa kutolewa ikilinganishwa na miaka mingine ya masomo na mpaka sasa mchakato wa majina yao bado haujakamilika?
Kama michezo ni starehe, furaha na kufahamiana kulikuwa na umuhimu gani wa kuyafanya hayo katika kipindi hiki ambacho maisha ya maelfu ya watanzania kubaki ama kuondoka vyuoni yapo katika mikono yenu iliyo na mamlakaa juu ya hatima ya watanzania hawa?
MWISHO.
Sisi kama watoto wa mafukara ambao kimsingi ndio walipa kodi wa Tanzania tunaomba kupewa majibu ya wazi katika vyombo vyaa habari kuwa.
NI KWANINI MSICHUKULIWE HATUA KALI ZA KIUTENDAJI HASA KATIKA ZAMA HIZI ZA ?HAPA KAZI TUU?
PILI NAOMBA MUELEZE WAZI NI KWANINI MUHESHIMIWA RAIS DR. JOHN POMBE MAGUFULI ASIFANYE ZIARA YA GHAFLA KATIKA OFISI ZENU KESHO ASUBUHI?
?PAMBANA NA HOJA USIPAMBANE NA MTOA HOJA?
SHITINDI VENANCE ROLANDI, MWENYEKITI WA KAMATI YA MAWAZIRI WA MIKOPO TANZANIA. 0759704444.