Waraka wa Shigongo kwa Ze Original Komedi

"Ametoa kwenye gazeti na kasema pia wiki ijao atatoa waraka kwa Seki. Kama kweli ana nia nzuri si ange watafuta privately awape ujumbe?"


Lakini ujumbe si umefika? kama wao wanavyotumia TBC1 kuwarushia watu makombora basi kwa style hiyo nao watajibiwa....

Maneno ya Busara Eric..Big up!!!!
 
Ila kiukwelii ni kwamba bila Shigongo kutumia mbinu zake chafu, leo Mashaka asingekuwa wa kubangaiza. Shigongo ndiye aliyehakikisha jamaa anakuwa bankrupt na kumfilisi kabisa.

Ndo maana ktk post yangu ya wali mwanzo wa thread hii nilisema tope limechafua vumbi...
mwenye akili afahamu
 
Sasa kama sekioni ni yatima tatizo ni nini ? Sekioni alikuwa anaishi kimara baruti na hakuwahi kulelewa na reginald mengi kama shigongo anavyotaka tuamini

Ili kumsaidia mtu sio lazima uishi nae; kuna yatima wengi duniani wanasaidiwa na watu wanaoishi Ulaya na Marekani kwa wafadhili wao kuwatumia pesa za karo pamoja na matumizi. Seki alifadhiliwa na Mengi na kwa utamaduni wa kiafrika mtu anayemtukana mfadhili wake hupatwa na laana; nadhani vijana hawa hawayajui haya! Shigongo amewapa darasa zuri sana hasa ule mfano wa kondomu kwani ni ukweli usiopingika kuwa Manji [kama walivyo wahindi wote] atawathamini hawa vijana pale tu watakapokidhi mahitaji yake baada ya hapo atawatupilia mbali. Ukweli ndio huo.
 
Last edited:
Wakasema Eddie Lunyamila wa Yanga eti choka mbaya, akiwashtaki watasemaje, eti alikuwa anamtegemea mkewe na alipokufa naye kwisha kazi, unaweza kumsimangia mtu kweli kifo cha mkewe?

Waraka wa Shigongo unatoa baraka kwa Orijino Komedi kuwakaanga ambao hawajawasaidia ila wasifanye hivyo kwa ambao hawajawasaidia. Ushauri ambao ni very unfair
 

nakubaliana na waraka huu kabisa, ni watu wachache sana wataelewa umuhimu wa waraka huu, na si kwa ze commedy wenyewe bali hata kwa maisha yetu ya kila siku, tunachanganyikiwa na mafanikio kidogo sana tunayopata tukumbuke ....if u dont raise your eyes eneough and see far you will think you are in the highest peak.....
 
Nafikikiri Shigongo ametoa ushauri mzuri tu kwa hao madogo, kwa sababu sio vizuri hata kidogo kufanyie mizaha kwenye TV hali za maisha za watu. This is a very sensitive issue which leaves other people embarrased and feeling down. Mtu kama mambo yake hayamwendei vizuri sio wa kumdhihaki hata kido, because that is just a destiny and anyone can be in that position. I think this guys need to find some other issues to make fun on rather than making a joke a other people's situations.

The other thing is, a good advice is a good advice and it does'nt matter where its coming from. The fact of the matter is that Shigongo has given these guys a very good advice, and whether Shigongo is not clean or not cannot trivialise the advice. Kama some of you wana JF mnataka kusuggest that mtu asitoe advive mpaka nae awe msafi, nani anaweza akaprove kweli kama yeye ni msafi sana. Kila mtu ana mapungufu yake, and thats why we are human beings, but that does not stop us from giving advice from our relatives, friends etc.

We need to create the habit of taking the advice as it is and trying to digest and see if its good advice rather than weighing it based on where it is coming from.
 

True Nguli ni sisi tu wachache! Finally I can see.
 
alichokifanya Shigongo ni hoja dhaifu, anaanza kumjadili mtu na si hoja.

Tukianza kumjadili na yeye humu kweli atabaki?mbona tunamwangalia namna alivyoandika makala zake za Napasua jipu pwaaa juu ya amina chifupa tena katika critical situation tukauchuna? anatafuta issue ya kuuzia gazeti i think..na ni mtu wa maslahi zaidi ya kitu anachokiamini.

Tuache kila mtu afane kazi yake, nakubali kukosoa uendeshaji wa kazi upo katika kuboresha lakini si kama shigongo alivyofanya.
 

Umesema ukweli mkuu. Tatizo huku kuna watu wana bisha bila kuangalia pande zote. Nadhani wengine ili mradi tu wawe wamebisha ndiyo wana ridhika.
 
Sijui kama nipo sahihi, but nilichomsoma mwandishi wa waraka ni kuwa "Abiola ndo kamlea Seki" Mengi kawapa kuonekana kama wachekeshaji wazuri via matukio.

Ila pia kama kuzidisha wanazidisha basi wanaweza kupunguza, ila kama hawazidishi sidhani kama hiyo nayo kuwa ni P.

Pia sisi ndani jamvini si tunatakiwa kuchukua mazuri kadri ya lengo????? N akama maneno yana uzuri basi tuyapimie hapo hata kam aliyesema kawa naye ni walewale.
 
Nakubaliana na shigongo katika mtizamo mmoja tu....ushauri wake ni muhimu kwa macelebrity wa bongo. Hiyo ya orijin komedi mmh wanajuana wenyewe...waswahili husema nyani haoni kundule. Nani asiyejua shigongo ni bingwa wa kuwachafua watu tena hasa wakina dada wanaomnyima uroda...mi ningemshauri abadilishe kichwa cha habari na aseme....Waraka maalum kwa vijana wenye umaarufu Tanzania.

Kama kufulia ndio kafulia watu wengine wakumbushwe the hard way. Hiyo inakubalika kabisa bwana, hata wenyewe komedi wanajua watakuja kusemwa na yeye huyo huyo wakifulia. Aende zake kule, mbona kadhamini the utamu watu hatumgusa au amesahau alimia 60 ya habari zake alikuwa akizotoa the utamu, si yeye aliyeitangaza ile blog kwa nguvu ili asiishiwe na story. Nashangaa kwanini hajaguswa na watu wa usalama. Hii nchi bwana.
 
Alichosema Shigongo ni sahihi kabisa, ametoa ushauri kwa hawa vijana ambao ni mzuri sasa haya mengine yanayomhusu yeye sio issue yaje kwa wakati wake, kama naye ana matatizo ina maana haruhusiwi kumshauri mtu? Tuwe wakweli jamani sio sahihi hata kidogo kumcheka mtu aliyeanguka kimaisha kwani hakuna apendaye; jana tena nimeone wakimcheka Saida Karoli kwamba amekuwa muuza chipsi, jamani wasaidieni hawa vijana kwa ushauri.
 
I find a lot of hyprocracy in this 'waraka'......his udaku newspapers are full of gossip and dirty pictures....then who is clean btn Eric and the orog..co...ur udaki newspapers are spoiling so many Tanzanians..
Shigongo please try to practice what u preach!!!
 
Mwe!!
huyu nae kafulia kweli.
Sasa kama walimsema Mashaka yeye imeuma nini?
"Iso kuwasha hujailamba"-Mjomba Mpoto.
 
Fasihi ilivyo ina tafsiri nyingi na mara nyingi tafsiri yoyote inaweza kukubalika kulingana na inavyojengewa hoja. kwa upande wa mwandika waraka naona ile sehemu ya aliyee....... imemboa sana na kwa mtazamo wake anaona jamaa kama vile wanajiona wao sasa ndo wako matawi ya juu na kwasababu hiyo wanawapuuza waliojichokea (waliofulia)- (Vema kabisa ndo mawazo yake hayo). Lakini angeweza kufikiria kwamba jamaa wanataka kila mtu akaze buti mahali alipo ili asije fulia. Kimsingi kila mtu hapendi kuporomoka kimafanikio lakini wakati fulani baadhi ya watu wanalewa mafanikio na kujisahau kuweka misingi imara ya kuendelea kuwa katika hali hiyo ya mafanikio na mwisho wake ni kufulia.
 
Huyo Mengi kama katukanwa si aende mahakamani?

Seki $ ITV na EATV walikuwa wanategemeana, sio kweli kwamba Seki alikuwa anamtegemea Mengi bali ktk vipindi vyake na Mengi alikuwa anaweka matangazo yake anapata pesa.
 
Huyu asitupoteze muda mjinga wa kwimba hana mpya angelijuwa ni kiasi gani mamia kwa mamia ya watanzania wamejipiga vitanzi na kuimia vibaya nafsi zao kwa ajili ya magazeti yake ya udaku wala asingefikia hatua ya kutaka kujikosha kwa mashaka huyu ni mjinga na mpenda sifa kuliko anavyojaribu ku-pretend kasha jaribu kushindana na clouds na primie time akajiona hana uwezo yote ilikuwa ni kutafuta umaarufu na sifa za kijinga leo anasema hatafuti umaarufu isipokuwa uanatafuta nini? mdanganye rafiki yako tippoh athumani si wajanja wa mjini uliowakuta hapa mjini
Sasa huyo Dudu baya unaweza kumuelezea nani akakuelewa status yake hata mwendawazimu anamjuwa kuwa ni mwendawazimu ndio maana anaimba kisukuma mpaka leo zaidi ya hapo jina lake DUDU BAYA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…