Ngaliba Dume
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,710
- 3,669
Jana I.G.P S.Mwema alisambaza waraka kwa ma-RPC wote Tz nzima kuwataka waitishe "MABARAZA YA ASKARI" ktk mikoa yote,lengo likiwa ni kutathimini mwenendo wa Jesh la polisi dhidi ya raia. Katika Mabaraza hayo Askari walipewa nafasi kujadili,kutoa mawazo na kupendekeza nini kifanyike baada ya Jesh kupoteza imani kwa raia na jamii. Katika waraka huo wa siri I.G.P aliwataka makamanda wawatie moyo vijana wasikate tamaa,kwan kwa tukio la Iringa imeonekana askari wote wamerudi nyuma na kupunguza hari ya kazi,hii imefanya viongozi wa juu kupata hofu ya utayali wa askari ktk kulitumikia jeshi... Katika maoni,askar wengi wamependkeza RPC Iringa aunganishwe ktk kesi,kwani kumwacha Cleophas Simon peke yake n uonevu,pia wameomba serikali iwakemee viongozi wa CCM wanaoshndkza polisi kuwatandka vyama vya upinzani..ktk kikao cha mkoa wa Iringa askari wengi wameonekana kukata tamaa na kutaka kuacha kazi...hali ya askari wa chini wanaotumika ktk Operation za riots imeshuka sana kwa kutishika na tukio la Iringa. Vijana wengi wameonekana kuchukizwa na hali ya kulazimishwa kutumia nguvu kwa maslahi ya kisiasa,kwa kugundua hilo makamanda wamewatia moyo vijana wengi kuwa wasikate tamaa,kwani swala la Iringa n sehemu ya ajali za kazini ambazo wao kama askari wanatakiwa wakabiliane nazo! Kiukweli vijana wengi wamekata tamaa baada ya kuona panapotokea tatizo ni askari wa vyeo vya chini ndo wanatolewa kafara bila kufuata uwajibikaji wa pamoja na Seniority ya jeshi la polisi ambapo mdogo hafanyi kitu bila mkubwa kutoa amri.