Toggle navigation
Advertised Posts
RITA (September 6, 2016)
View All
Call for Interview
View All
Placements
View All
Publications
Procurement
Press Releases
News
Circulars
Hoja za Wadau
Visitors Counter
»Online 15
»Today 1737
»Yesterday 5443
»Week 11681
»Month 27505
==================
»Total 20404088
MAJIBU YA MASWALI NA HOJA ZA WADAU KWA MWEZI AGOSTI, 2016.
September 6, 2016
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, inapenda kuwashukuru wadau na wananchi wote waliotuandikia maoni pamoja na kuuliza maswali mbalimbali kwa kipindi cha mwezi Agosti, 2016. Tunapenda kuwajulisha wale wote waliotuandikia maoni na maswali na hawajafungua baruapepe zao (Emails) na kurasa zao za Facebook wazifungue kwani tumejibu kila swali na kuwatumia katika anwani husika na baadae kuyaunganisha maswali na maoni yanayofanana na kuyatolea majibu ya jumla kwa faida ya wasomaji wetu wengine ili kuendelea kuelimishana kuhusu masuala yanayohusu Uendeshaji wa Mchakato wa Ajira Serikalini.
1. Swali
Nawapongeza kwa kufanya kazi nzuri ya kuendesha mchakato wa ajira Tanzania, pili napenda kuuliza maswali mawili kama ifuatavyo, A. Napenda kujua ni vigezo vipi na ni kada gani ambayo huajiriwa kuwa Maafisa Mipango? B. je ni muda gani umebaki ili kuanza kutangaza Ajira?
Jibu
Swali la kipengele B. ambalo umeuliza ni muda gani umebaki ili kuanza kutangaza ajira, Kwa kuwa Serikali bado inaendelea kukamilisha zoezi la uhakiki wa Watumishi hewa ni vyema tukaendelea kuvuta subira hadi pale zoezi hilo litakapokamilika na kama mlivyoarifiwa awali juu ya kusitishwa kwa Ajira, vivyohivyo mtapewa taarifa rasmi na mamlaka zinazohusika za kuendelea kutoa nafasi za Ajira.
4. Swali
Habari Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, poleni na kazi ya kujenga Taifa. Mimi ni kijana wa kiume na mkazi wa Mwanjelwa Mbeya na pia ni muhitimu Chuo Kikuu cha Jordan.
Kuhusu kusitishwa kwa ajira mpya, kwanza naweza sema Rais wetu alikuwa sahihi kusitisha Ajira kutokana na uwepo wa watumishi hewa, nilikuwa nataka niwambie kuwa muda unazidi kwenda na atujapata taarifa yoyote nini kinaendelea japo mlisema zoezi la kuhakiki watumishi hewa bado linaendelea lakini bado hamjasema mtamaliza lini, nikimaanisha tarehe na siku, ilihali vijana asilimia kubwa waliohitimu wameanza kukata tamaa wakiamni Ajira zaweza zisiwepo sababu hawajui kesho yao na kuna baadhi walishindwa kusaini mikataba kwenye Taasisi binafsi wakiwa na uhakika wa Ajira sasa muda unaenda wengi wao wapo nyumbani na wakiwa njia panda bila kujua pakwenda.
Maoni yangu ningewaomba mjitahidi kabla ya mwezi huu kuisha muwe mmesha toa taarifa kamili kuhusu ajira mpya, na kama zoezi la kuhakiki watumishi hewa limekua bado linahitaji muda mwingi mwambieni Mhe. Rais John Pombe Magufuli aruhusu Ajira hata kama ishu ya watumishi hewa bado, kwa hawa wahitimu mliopanga kuwaajiri waajirini kwa kuwatengea (folder) lao ambalo alita ingiliana na waliopo kazini na Rais alisema hata toa ajira mpya akimaanisha zoezi litakuwa gumu zaidi kwa kuongeza watumishi wapya waunganishwe na wazamani, na sina imani kama nyie wenye dhamana ya kuajiri kwamba hamuwezi teknologia ya kutenganisha waajiri wa zamani na wapya ilihali sasa hivi teknolojia imekua, jamani nchi kama Rwanda watushinde? najua Rais wetu yupo siliazi mpelekeni hata proposal jinsi ya kufanya namna gani mtatenga watumishi waliopo na wa zamani ili operation ya kucheki watumishi hewa iendelee na waajiriwa wapya waanze kazi.
Na sera ya Rais wetu ni hapa kazi tu na sasa hivi nikiangalia kuna upungufu wa watumishi kama Madaktari, Walimu na sekta nyingine zenye uhaba wa wafanyakazi na muda unazidi kwenda je sera ya hapa kazi tu itaendana wakati mahospitalini hakuna wafanyakazi wa kutosha, vijijini hakuna walimu wa kutosha, tena gepu la watumishi walio hewa bado lipo wazi, jamani jitahidini nimeandika haya kwa maendeleo ya nchi pamoja na kupunguza idadi ya wahitimu waliopo nyumbani kwa mwaka na miezi sasa huku tegemeo na walichosomea kinahuishwa kuajiriwa serikalini na ofisi ya TAMISEMI Naibu Waziri Suleiman Jafo alisema wametenga budget ya kuajiri Watumishi wapya 71,000, kwa niaba ya wahitimu wanaosubiri Ajira nategemea mawazo yangu yatafanyiwa kazi na kupata majibu sahihi kabla ya mwezi huu kuisha. Asanteni sana na kazi njema.
Jibu
Tunashukuru kwa swali lako pamoja na maelezo marefu tumeyaopokea, yataendelea kufanyiwa kazi kadri inavyowezekana. Aidha, Serikali imejitahidi kutoa taarifa ya hatua iliyofikia katika uhakiki wa watumishi hewa mara kwa mara hata wiki iliyopita Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora alizungumza na Waandishi wa habari na kuelezea kuwa zoezi hilo liko katika hatua nzuri na kuzitaka baadhi ya taasisi ambazo bado hazijawasilisha taarifa zao za watumishi hewa ziwasilishe kabla ya tarehe 26 Agosti, 2016 ili taarifa hiyo iweze kuwasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua zaidi.
Hivyo, ni vyema tukaendelea kuvuta subira ili kupisha mamlaka husika kuweza kuratibu zoezi hilo kwa ufanisi kutokana na unyeti wake kwa mustakabali wa Taifa hili. Mwisho, nimalizie kwa kukuelewesha kuwa Sekretarieti ya Ajira ina dhamana ya kuendesha mchakato wa ajira kwa niaba ya waajiri katika Utumishi wa Umma ila siyo inayosimamia zoezi la uhakiki wala haiwezi kuendesha mchakato wa ajira bila ya kupata kibali cha kufanya hivyo kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, kwa kuwa suala la Ajira lina miongozo yake, linahitaji bajeti, kutengwa nafasi kwa mujibu wa ikama. Hivyo tusubiri zoezi hilo likamilike na baada ya hapo taarifa rasmi kuhusu mchakato wa Ajira Serikalini itatolewa na Mamlaka zinazohusika.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma. 06 Septemba, 2016.
Public Service Recruitment Secretariat.

2016. Tel: +255(22) 2153517 | Fax: +255(22) 2153518