WARAIBU WENGI HAWAPENDI HUACHE VILEO

WARAIBU WENGI HAWAPENDI HUACHE VILEO

Papillon 1906

Senior Member
Joined
Jun 19, 2025
Posts
117
Reaction score
387
Waraibu wengi hawapendi kumuona mraibu mwenzao anafanya jitihada za kujitoa katika matumizi ya vilevi kama kuvuta bangi, madawa ya kulevya na kutumia pombe.

Ikitokea unafanya jitihada kama kupunguza kuhudhuria maskani au vilabuni au baa wanakuona snitch, kama ulikuwa mlevi ukaanza kunywa juisi watakubeza na kukutolea maneno ya dhihaka.

Wanataka uendele kushinda maskani kula bangi na kunywa vichungu asubuhi mbaka jioni.

Waraibu mpeni moyo na kumuunga mkono mmoja miongoni mwenu aliyechoka kuishi maisha ya utegemezi. Huyo inaezekana akawa chachu ya wewe kutoka kwenye uraibu.
 
Me mbona napenda watu waache JAPO na me vinanitesa ila hope Niko kwenye plan nzuri ya kuacha..ila kabla sijaacha sass kuna kampani yangu hio mwanangu hiyo sitaki aache kabla yangu nitakosa Vibe
 
katika taifa ambalo pombe inauzwa bei rahisi kuliko maji ya KUNYWA?
TWAFA
Katika taifa ambalo mgombea ananunua POMBE ili achaguliwe kuwa mtatua matatizo wa walevi
 
Back
Top Bottom