VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Tangu kadhia ya kupitishwa 'kimagumashi' na 'kuchomekwa' kwa vifungu katika Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Katiba Bungeni Dodoma,wapinzani hawakulala.Hawakushindwa. Waliendelea kupigania ustawi wa nchi kupitia Katiba mpya bora nje ya Bunge.Wakaitisha mikutano miwili mikubwa: Jangwani na Kibanda Maiti. Wakaungwa mkono. Wakasikika.
Wapinzani walilenga mambo makubwa mawili. Kwanza, kumtaka Rais awe makini katika mchakato huu wa Katiba mpya kwakuwa unabeba mustakabali wa Taifa. Hapa, wakamuomba Rais asisaini Muswada husika.Pia, walitaka kusikilizwa na Rais katika kuwasilisha hoja zao. Walitaka majadiliano na maridhiano ya kitaifa na Rais. Lengo hili limefanikiwa.Mosi, taarifa rasmi za Ikulu zinaonesha kuwa Rais hakusaini Muswada husika. Pili,wapinzani jana wamekutana na Rais Ikulu kusikilizana na kuelewana. Lengo limetimia.
Pia, wapinzani walilenga kurejeshwa Bungeni kwa Muswada huo ili uweze kujadiliwa tena kwa maboresho yalengayo afya ya Taifa.Tayari,Rais 'ameshaamuru' Muswada urejeshwe Bungeni kwa marejesho.Waweza kurejeshwa ukiwa umeshasainiwa au la. Haijalishi. Lengo la pili limetimia pia.
Ingawa wapinzani walibezwa sana hasa na Waandamizi wa CCM yetu, muda si muda mantiki yao itaonekana kwa wengi au wote. Kupigania Katiba bora ni kupigania Taifa bora. Katiba ndiyo msingi wetu wa kwanza. Vingine vyote vinaifuata Katiba. Vingine vyote ndiyo.
Hongereni sana wapinzani: Mbowe,Lipumba na Mbatia na vyama vyenu kwa kufanikiwa hata kwa haya. CCM yetu ijifunze kuendana na wakati na mabadiliko yake.Watanzania si wale jamani,wamebadilika sana.Tusije tukabadilishwa kwa kura!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Wapinzani walilenga mambo makubwa mawili. Kwanza, kumtaka Rais awe makini katika mchakato huu wa Katiba mpya kwakuwa unabeba mustakabali wa Taifa. Hapa, wakamuomba Rais asisaini Muswada husika.Pia, walitaka kusikilizwa na Rais katika kuwasilisha hoja zao. Walitaka majadiliano na maridhiano ya kitaifa na Rais. Lengo hili limefanikiwa.Mosi, taarifa rasmi za Ikulu zinaonesha kuwa Rais hakusaini Muswada husika. Pili,wapinzani jana wamekutana na Rais Ikulu kusikilizana na kuelewana. Lengo limetimia.
Pia, wapinzani walilenga kurejeshwa Bungeni kwa Muswada huo ili uweze kujadiliwa tena kwa maboresho yalengayo afya ya Taifa.Tayari,Rais 'ameshaamuru' Muswada urejeshwe Bungeni kwa marejesho.Waweza kurejeshwa ukiwa umeshasainiwa au la. Haijalishi. Lengo la pili limetimia pia.
Ingawa wapinzani walibezwa sana hasa na Waandamizi wa CCM yetu, muda si muda mantiki yao itaonekana kwa wengi au wote. Kupigania Katiba bora ni kupigania Taifa bora. Katiba ndiyo msingi wetu wa kwanza. Vingine vyote vinaifuata Katiba. Vingine vyote ndiyo.
Hongereni sana wapinzani: Mbowe,Lipumba na Mbatia na vyama vyenu kwa kufanikiwa hata kwa haya. CCM yetu ijifunze kuendana na wakati na mabadiliko yake.Watanzania si wale jamani,wamebadilika sana.Tusije tukabadilishwa kwa kura!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam