Elections 2010 Wapinzani tumieni kiamilifu kauli za mwalimu nyerere kipindi hiki

Jatropha

JF-Expert Member
Apr 9, 2009
1,151
199
kabla ya kifo chake mwalimu nyerere alipata kuamka baadahi ya mamabo ambayo hivi sasa ynajitokeza wazi wazi mathalani:-

1) wakati wote wa maisha yake mwalimu nyerere alisistiza kuhus umuhimu wa serikali yoyte kukusanya kodi ipasavyo na akawa kutamka "serikali yoyete isiyokusanya kodi ni ya wala rushwa"

2) katika mchujo wa wagombea urais ndani ya ccm mwaka 1995, mwalimu nyerere alitumia madaraka yake kukata jina la edward lowassa katika kinyang'anyiro hicho kutokana na tuhuma za kutumia madaraka yake kujilimbikizia mali kupita uwezo wake. Viongozi wa ccm wakapuuza usia wake kumhusu lowassa na tabia ya viongozi kutumia nydhifa zao kujilimbikizia mali na wakampatia madaraka ya uwaziri mkuu; sote ni mashuhuda ya nini kilitokea ndani ya miezi sita ya lowassa katika uwziri mkuu.

Mwalimu nyerere ni miongoni mwa watanzania wa awali kuwapigia kura wagombea wa upinzani katia uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi, kwa kumchagua mgombe kutoka chama cha upinzani cha nccr mageuzi aitwaye balozi paul ndobo katika nafasi ya ubunge wa jimbo la musoma vijijini. Hii ni baada ya chama alichokiasisi mwalimu nyerere cha ccm kumsimamisha mgombea mwenye tuhuma za kufilisi ushirika.
mwalimu nyerere alipata kutamka hadharani kuwa "ccm sio baba wala mama yangu mzazi", hivyo kwa kuwa ccm haikusimamisha mtu mwenye rekodi ya uadilifu nimetumia haki yangu yab kikatiba kuchagua mtu muadiulifu kutoka kambi ya upinzani.

leo hii sote tunashuhudia idadi kubwa ya watuhumiwa wenye tuhuma mbali mbali na kubwa za ufisadi wakipitishwa na ccm kugombea ubunge; na kisha kunadiwa na viongozi wa kitaifa wa ccm pasipo aibu yoyote.

3) mwalimu nyerere pia aliwahi kunukuliwa aktamka kuwa "chadema ni chama makini" na katika miaka hii mitano 2005-2010 sote tumeshuhudia ni kwa jinsi gani chadema imefanikiwa kuhakikisha raslimali za taifa zinatumika kuwanufaisha watanzania na sio wawekezaji kutoka nje tuu.

Hivyo wagombe a wa upinzani mwaka huu wawakumbushe watanzania kauili hizi muhimu za mwalimu nyerere, ikiwezekana walipie hotuba za mwalimu nyerere alipotamka kauli hizi katika vyombo vya habari ili kuwafanya watanzania walio wengi waondokane na matongotongo ya mfumo wa chama kimoja.

























 
Back
Top Bottom