Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,215
- 10,283
Lowassa alikuwa mgombea wa Ukawa sio wa Chadema peke yake. Ndio maana Juma Duni Haji akajiunga na Chadema kutoka CUF ili awe mgombea mwenza. Lowassa aliisaidia Chadema kuvuna wabunge ( kitu ambacho wenzake katika Ukawa hawakufurahia) na kura za urais zilizopelekea kupata ruzuku ya maana na hivyo kuweza kuhimili mishale yote waliyorushiwa 2015 mpaka 2020.Mbowe kidogo aiuwe CHADEMA 2015 ni vile tu wanachama waliamua kwenda hivyo hivyo.
Sasa ni zamu ya uongozi upya kuonyesha kuwa wataweza kukiongoza na kukijenga chama chao katika wakati mgumu ulio mbele yao.
Amandla...