Wapinzani mna kazi kubwa ya kuwaelimisha watanzania

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,371
Wapinzani nawashauri katika mikutano ya kampeni ya chaguzi ndogo za madiwani katika kata 21 kwa upande wa bara na kwa ubunge wa Jimbo la Dimani huko Zanzibar, waelimisha wapiga kura kuhusu siasa za chama tawala.

Ni tabia ya chama tawala kulegeza mambo pale uchaguzi unapokaribia kwa lengo la kuwahadaa wapiga kura jambo ambalo baadhi ya watanzania hawalielewi.

Kwa mfano,hivi sasa kuna huo uchaguzi wa madiwani 22 kwa upande wa Tanzania bara unakuja na huenda hii ndii ikawa sababu ya wamachinga na wachimbaji wa dogo kuruhusiwa kufanya shughuli zao katika maeneo ambayo waliokuwa wameondolewa.

Mbali na wamachinga na wachimbaji wadogo,sitashangaa kipindi hiki kikatumika kutangaza neema kwa wafanyakazi kama vile kulipwa malimbikizo yao, kupandishwa vyeo na hata tukasikia ahadi za watu kuajiriwa,n.k.

Wapinzani ni wajibu wenu kuwaelimisha wapiga kuwa juu ya jambo hili kwa kulifanya kuwa ni moja ya agenda yenu kuu kwenye mikutano ya kampeni itakayoonza tarehe 22 mwezi huu mpaka tarehe 21 mwezi January mwakani.

Baada ya uchaguzi huu wa madiwani kukamilika, nawashauri elimu hii iwe endelevu kwasababu watanzania hawa ni wepesi mno wa kusahau ingawa ni wazuri kwenye kulalamika.

Ni ushauri wa bure hasa katika awamu hii ambapo mwanamchi wa kawaida ni kama amesahaulika huku kipaumbele kikiwa ni ndege na mambo mengine ya aina hiyo..

Kipindi hiki huwezi sikia zile kauli kuwa wanaolalamika ni wapiga dili,n.k bali ni kipindi cha lugha tamu tamu za kutia matumaini ila uchaguzi ukipita tu lugha hizi zitarejea kwa kasi hivyo ni wajibu wenu wapinzani kutoa elimu na msisitizo kwa wapiga kura.

Msishangae pia hata kikao cha CCM kinachotarajiwa kuketi leo hii kikaja na maazimio au kauli tamu kuhusu mwananchi kumbe lengo ni huu uchaguzi mdogo tu na si vinginevyo.

Miko itakayoshiriki kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani imetajwa katika hii post hapa chini ikiwemo Mwanza,Shinyanga na Mara.

Kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge na udiwani kuanza December 22
 
Wapinzani nawashauri katika mikutano ya kampeni ya chaguzi ndogo za madiwani katika kata 21 kwa upande wa bara na kwa ubunge wa Jimbo la Dimani huko Zanzibar, waelimisha wapiga kura kuhusu siasa za chama tawala.

Ni tabia ya chama tawala kulegeza mambo pale uchaguzi unapokaribia kwa lengo la kuwadaa wapiga kura jambo ambalo baadhi ya watanzania hawalielewi.

Kwa mfano,hivi sasa kuna huo uchaguzi wa madiwani 22 kwa upande wa Tanzania unakuja na huenda hii ndii ikawa sababu ya wamachinga na wachimbaji wa dogo kuruhusiwa kufanya shughuli zao katika maeneo ambayo waliokuwa wameondolewa.

Mbali na wamachinga na wachimbaji wadogo,sitashangaa kipindi hiki kikatumika kutangaza neema kwa wafanyakazi kama vile kulipwa malimbikizo yao, kupandishwa vyeo na hata tukasikia ahadi za watu kuajiriwa,n.k.

Wapinzani ni wajibu wenu kuwaelimisha wapiga kuwa juu ya jambo hili kwa kulifanya kuwa ni moja ya agenda yenu kuu kwenye mikutano ya kampeni itakayoonza tarehe 22 mwezi huu mpaka tarehe 21 mwezi January mwakani.

Baada ya uchaguzi huu wa madiwani kukamilika,nawashauri elimu hii iwe endelevu kwasababu watanzania hawa ni wepesi mno wa kujisahau ingawa ni wazuri kwenye kulalamika.

Ni ushauri wa bure hasa katika awamu hii ambapo mwanamchi wa kawaida ni kama amesahaulika huku kipaumbele kikiwa ni ndege na mambo mengine ya aina hiyo..

Kipindi hiki huwezi sikia zile kauli kuwa wanaolalamika ni wapiga dili,n.k bali ni kipindi cha lugha tamu tamu za kutia matumaini ila uchaguzi ukipita tu lugha hizi zitarejea kwa kasi hivyo ni wajibu wenu wapinzani kutoa elimu na msisitizo kwa wapiga kura.

Msishangae pia hata kikao cha CCM kinachotarajiwa kuketi leo hii kikaja na maazimio au kauli tamu kuhusu mwananchi kumbe lengo ni huu uchaguzi mdogo tu na si vinginevyo.
ndege JOHN sababu hii ndio sababu ya hilo tamko la kuwatetea wamachinga na wachimbaji wadogo.
 
Huchelewi kusikia KAMATI KUU YA CCM IMEMKEMEA RAIS KUTOKANA NA HALI MBAYA YA UCHUMI NA KUMPA ONYO KALI WAZIRI WA FEDHA !

CCM kwa ulaghai ni hatari sana !
Nimegundua watu wengi hata humu ndani hawaelewi ni nini kinaendelea.Mwanza na Shinyanga ni moja ya mikoa ambayo itakuwa na uchaguzi mdogo wa madiwani pamoja na Mara ukiwa ni mkoa wenye shughuli za wachimbaji wagogo.
 
Nimegundua watu wengi hata humu ndani hawaelewi ni nini kinaendelea.Mwanza na Shinyanga ni moja ya mikoa ambayo itakuwa na uchaguzi mdogo wa madiwani pamoja na Mara ukiwa ni mkoa wenye shughuli za wachimbaji wagogo.
Mkuu usihofu , manyanyaso waliyofanyiwa watu wa kanda ya ziwa kwa mwaka mmoja uliopita , pamoja na kudanganywa sana startv , wenyewe wamekoma .

Wanachinjwa kila siku huko geita utadhani hakuna serikali , uchunguzi wangu umebaini kwamba Mwanza ndio sehemu inayoongoza kwa kunyanyasa wafanyabiashara duniani .

Wasipojifunza kwa hili basi ni heri tufundishe mawe .
 
Nimegundua watu wengi hata humu ndani hawaelewi ni nini kinaendelea.Mwanza na Shinyanga ni moja ya mikoa ambayo itakuwa na uchaguzi mdogo wa madiwani pamoja na Mara ukiwa ni mkoa wenye shughuli za wachimbaji wagogo.
Aisee wanajua Sana propaganda.. Michezo ya kuigiza na KUTAFUTA kick.. SERIKALI ya Ndege John ni ya mihemko +mizuka.. 2020 sio mbali
 
Mkuu usihofu , manyanyaso waliyofanyiwa watu wa kanda ya ziwa kwa mwaka mmoja uliopita , pamoja na kudanganywa sana startv , wenyewe wamekoma .

Wanachinjwa kila siku huko geita utadhani hakuna serikali , uchunguzi wangu umebaini kwamba Mwanza ndio sehemu inayoongoza kwa kunyanyasa wafanyabiashara duniani .

Wasipojifunza kwa hili basi ni heri tufundishe mawe .
Watu wameshakula hasara alafu saa hizi ndio anaingilia kati.

Kero za wachimbaji wadogo karibu kila siku huzikosi kwenye taarifa ya habari ila leo ndio mkuu anatoa kauli kukuzia agizo lake.Cha kujiluza siku zote alikuwa wapi?

Msitarajie CCM wako tayari kupokea aibu ya kushindwa kwenye hizi chaguzi hivyo watatumia kila mbinu kutaka kushinda viti hivi 22 vya udiwani
 
Inahitajika nguvu ya ziada sana , cjui watanzania tupo brainwashed, celewi aiseee, yan kwa mateso wanayopitia sasa ila wakienda kupiga kura bado hali ni ile ile, cc labda ashuke malaika kutoka mbinguni aisee

Uchaguz 2015 kuna bibi kina mama walikua vibaraka wa ccm , nikawauliza kuhusu sera za ccm na upinzani wakang'ang'ani oooh ikuchukua CHADEMA kutakua na vita! Ukiwauliza vita gan au itatokeaje hawajui ila wamekomaa wanaogopa vita..
Mwisho wa siku nakuja kukutana nao mwezi ulopita wanadai maisha magumu, biashara hazitoki, gharama za maisha zimepanda,
Sasa na mimi kwa jeuri nikawaimbia kale kawimbo ka tumeipenda wenyeweee ngi ngii, chaguo letu wenyeweee ngingi.. Wacha waisome namba eeenhhh
 
Umesahau moja mkuu huku Arusha tumeletewa bodaboda ila ajira kwa fani tulizozisomea amekatalia ama kweli huyu ndiye mkoloni mweusi halisi.... Tatizo la CCM wanajisifu wanambio pasipo kumsifu anayewakimbiza wamesahau bila upinzani pasingekuwepo watumishi hewa, kutumbua mafisadi,kuwakumbuka waajiriwa walau kwa nyongeza kidogo hata kuumbua hasara tuliyoipata.............

Haya Pombe walete walete....wasisahau kale kawimbo..........Hatunywi sumu hatujinyongi...CCM MBELE KWA MBELEEEEEEEEE...
 
Watu wameshakula hasara alafu saa hizi ndio anaingilia kati.

Kero za wachimbaji wadogo karibu kila siku huzikosi kwenye taarifa ya habari ila leo ndio mkuu anatoa kauli kukuzia agizo lake.Cha kujiluza siku zote alikuwa wapi?

Msitarajie CCM wako tayari kupokea aibu ya kushindwa kwenye hizi chaguzi hivyo watatumia kila mbinu kutaka kushinda viti hivi 22 vya udiwani
Na watashindwa vibaya sana ! Juzi Upendo Peneza amemwaga sumu mbaya sana chato , hatukutarajia ule umati , kumbe tarakimu zinasomwa sana huko mkuu .
 
Back
Top Bottom