PreGE2025 Wapinzani 200 akiwemo diwani wa ACT Wazalendo wahamia CCM

PreGE2025 Wapinzani 200 akiwemo diwani wa ACT Wazalendo wahamia CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
2,439
Reaction score
6,692
Wanachama wa vyama vya upinzani 200 wa wilaya ya Tunduru akiwemo diwani wa kata ya Mchoteka kupitia tiketi ya Chama Cha Act Wazalendo Seif Dauda, katibu wa wilaya ya Tunduru wa Chama Cha Act Wazalendo Said Mponda, wamejiunga na Chama Cha Mapinduzi 2/4/2025 baada ya kumkabidhi kadi za uwanachama wa vyama walivyotoka katibu wa CCM, Balozi Dkt Emanuel Nchimbi akiwa katika ziara yake siku 5 katika mkoa wa Ruvuma.

Wakieleza sababu ya kuhama vyama vyao diwani pamoja na katibu wa Chama Cha Act Wazalendo wamesema wamevutiwa na utekekezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika wilaya ya Tunduru ambapo wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DKT Samia Suluhuu Hassan kwa kuleta miradi mikubwa katika kata ya Mchoteka na wilaya ya Tunduru kwa ujumla.

 
Alikuwepo Polepole kwa hiyo hizo ngonjera mbona beti zake tunazo
 
Nn maana ya kumkabidhi katibu wa ccm kadi za chama walipotoka?
Huyo katibu hizo kadi anakwenda kuzitumia kwenye nn?
 
Kamwe usimwamini mtu mwenye njaa...anawezaaa kugeuka kuwa kitu chochote mda wowote
 
Back
Top Bottom