Wapinga kuharamishwa Miraa Uingereza

Wapinga kuharamishwa Miraa Uingereza

Herbalist Dr MziziMkavu

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,067
Reaction score
34,829
120501134610_khat_304x171_q_nocredit.jpg

Miraa imepigwa marufuku nchini Marekani na katika baadhi ya nchi za Ulaya


Baraza la serikali la ushauri kuhusu madawa ya kulevya, limekataa wito wa serikali kupiga marufuku Miraa au Khat.
Baraza hilo kuhusu utumiaji mbaya wa madawa ya kulvya, linasema kuwa hakuna ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa miraa inasabbisha athari za kiafya.

Taarifa zinazohusiana


Miraa hutumiwa sana na watu wa jamii ya wasomali, Yemeni na wa Ethiopia na imepigwa marufuku nchini Marekani, katika baadhi ya nchi za Ulaya na Netherlands.
Wizara ya mambo ya ndani ndiyo ilipendekeza kufanywa kwa uchunguzi huo.

Baraza hilo lilisema kuwa hakuna ushaidi kuonyesha kuwa Miraa ambayo ina kemikali 'cathinone 'inayochangamsha ,ilihusishwa na visa vya uhalifu wa kupangwa.


Lilisema kuwa khat, ambayo inatafunwa na wengi ili kujichangamsha ingawa athari hiyo sio kubwa ikilinganishwa na madawa mengine ya kulevya kama Amphetamine".


Elimu ya kuzuia matumizi


Makundi ya jamii ya kisomali, yaliambia baraza hilo nchini Uingereza kuwa , utafunaji wa Khat ni tatizo kubwa la kijamii
091218161601_khat_yemen_ap_386.jpg

Na nchini Yemen pia watu hutumia sana Miraa


Wanaharakati walisema kuwa mmea huo unasababisha matatizo ya kiafya pamoja na kuchangia kuvunjika kwa familia.
Mmea huo hata hivyo, pia una athari zake kubwa ambazo hujitokeza baada ya matumizi ikiwemo shinikizo la mawazo, ndoto mbaya na mengineyo, ingawa haya yote sio thibitisho kuwa watu wanaweza kuwa waraibu.
Lakini mwenyekiti wa baraza hilo, Profesa Les Iversen alisema kuwa waligundua kuwa hakuna matatizo yoyote ya kiafya yanahusishwa na utumiaji wa miraa.
 
Back
Top Bottom