Wapiga kura jimbo la Iringa Mjini wamshangaa mbunge wao, Msigwa ana kazi kubwa kutetea kiti chake

Chilisosi

JF-Expert Member
Oct 19, 2008
3,051
747
WAPIGA KURA JIMBO LA IRINGA MJINI WAMSHANGAA MBUNGE WAO



WAKATI mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (pichani )na viongozi wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) leo walijitolea kufanya usafi katika eneo la kitanzani mjini Iringa kama njia ya kuhamasisha usafi, wapiga kura wa jimbo hilo wameonyesha kutofautiana na uamuzi huo wa mbunge kufanya usafi huku baadhi yao wakidai kuwa jimbo hilo limemsinda kuongoza na ndio sababu ya uchafu kuzagaa kila kona ya mji .


" Mbunge wetu leo anajitolea kufanya usafi siku zote alikuwa wapi hadi uchafu unazangaa kiasi hiki mitaani .....tunamtaka Msigwa kufanya kazi kama wabunge wengine na kuachana na siasa za kuunga unga na kutafuta umaarufu kwa watu "


Wakizungumza l;eo kwa nyakati tofauti wananchi wa jimbo la Iringa mjini walisema kuwa mji wa Iringa umeendelea kuzidiwa na uchafu na kuwa mbali ya mbunge kujitolea kufanya usafi pamoja na wanachama wa Chadema ila bado hatua hiyo haiwezi kutatua tatizo la uchafu na badala yake uchafu wa Manispaa ya Iringa utaendelea kuwepo .


Juma Husein mkazi wa Kitanzini katika Manispaa ya Iringa alisema kuwa mbunge wao anatafuta umaarufu wa kisiasa na kusahau kuwa yeye ni mbunge wa jimbo la Iringa mjini na mwakilishi wa wananchi hao bungeni hivyo alipaswa kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa uchafu katika jimbo lake badala ya kufanya usafi kwa misingi ya kisiasa huku akitambua kufanya hivyo ni kujichongea mwenyewe kwa wananchi kuwa kumbe ameonyesha kushindwa kuongoza jimbo hilo na ndio sababu ya taka kuzagaa kila kona.


Husein alisema ni vema mbunge Msigwa kwenda kujifunza katika jimbo la Moshi mjini ambalo pia linaongozwa na mbunge wa Chadema na kuona kama mbunge huyo ametumia mbinu kama hiyo kusafisha mji ama kuna mbinu nyingine inatumika badala ya hiyo ya zima moto inayotumiwa na mbunge Msigwa sasa ya kukodi magari ya usafi.


Aidha alisema kuwa kwa kuwa Manispaa ya Iringa inakabiliwa na tatizo la magari ya kusomba takataka na uhaba wa vyombo vya kuhifadhia takataka mbunge Msigwa kwa kutumia mfuko wa jimbo alipaswa kuanza kushughulikia kero hiyo badala ya kukodi magari kwa siku moja ili kutaka kuonekana kuwa ni mchapakazi wakati siku zote yupo mjini Iringa na uchafu huo upo.


Kwa upande wake mbunge Msigwa alipoulizwa na mwandishi wa habari hizi kuhusiana na utaratibu huo alisema kuwa kazi ya mfuko wa jimbo si kwa ajili ya kusafisha mji na kuwa yeye ataendelea kusafisha mji kwa muda wa siku mbili hizi kabla ya kwenda bungeni .


Msigwa alisema kuwa kupitia ofisi yake tayari amekwisha changisha kiasi cha shilingi milioni 16 kwa ajili ya kununua gari ya kubeba taka katika Manispaa ya Iringa ili kupunguza tatizo la uchafu katika mji huo.


Afisa afya wa Manispaa ya Iringa Severin Tarimo alipotafutwa na mwandishi wa habari hizi ili kueleza mikakati ya Manispaa ya Iringa juu ya hali ya uchafu inayoendelea kuukumba mji huo alidai kuwa kwa sasa yupo likizo hivyo anayeweza kujibia hilo ni yule aliyemwachia ofisi.


"Nazungumza na nani ....sasa mimi nipo likizo bwana naomba uongee na mtu mwingine" alikata simu


MWISHO
Source FRANCIS GODWIN BLOG

My take,
Msigwa kuna mtu anaitwa Chilisosi anakuja hapo hivyo jiandae vyema
CHILISOSI FOR IRINGA 2015

 
hee nani atapigia nyanya kura??
unaweka maoni ya ccm na wenye chuki ya maendeleo..
utaangushwa kaka kaa pembeni na siasa mkuuu umeshindwa weee
zero brain labda ndo watakupa kura
 
Huu ujtafiti unatilia mashaka makubwa sana maana kwa point uliyoandika kuwa tayari ameshachangisha 61millioni kununulia gari huoni kama huo ni mwanzo mzuri?Je, pamoja na mambo mengine kama mbunge ya maendeleo jimboni linaloonekana ameshindwa ni hilo tu la uchafu wa mji?

Katika maelezo yako nukuu ""Wakizungumza l;eo kwa nyakati tofauti wananchi wa jimbo la Iringa mjini walisem mji wa Iringa umeendelea kuzidiwa na uchafu "" Je ulifanikiwa kuwahoji wenyeji wangapi au uliitisha kikao?

maswahi hayo yananitilia shaka kubwa na makala yako na mwisho inaonekana kama kuna kampeni ya siri kuanza kumtambulisha Chilisosi kwa mbali

Jaribu kujibu hayo maswali ili sisi wananchi wa Iringa tujue ukweli uko wapi
 
Huyu ni Msigwa na anaonekani yupo karibu na wanakijiji Je amewaona wabunge wa CCM popote pale wakiwa wanajishughulisha na shughuli za kawaida wa wapiga kura??

"Ninajua kero ya maji na barabara ndizo zinazowatesa wakazi wa kijiji hiki hususani wakina mama, lakini niseme tu kwamba suala la maji, nimefurahi kuna mfuko mnaendelea kuuchangia deni lililobaki ninalimalizia sasa na kuhusu barabara tayari nimeshaleta greda nitahakikisha barabara hii inatengenezwa, nisipotimiza ahadi hizi msinipigie kura mwaka 2015,"


MBUNGE wa Jimbo la Iringa ,Mchungaji Peter Msigwa amewataka wakazi wa Kijiji cha Kigonzile, katika Manispaa ya Iringa kutomchagua katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ikiwa hatatimiza ahadi ya kuwapelekea maji na barabara katika kipindi hiki cha uongozi wake.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kigonzile juzi, Msigwa alisema amepania kuwafikishia maji na barabara wakazi wa kijiji hicho ili kuwapunguzia kero ya kutafuta maji na adha ya usafiri.

"Ninajua kero ya maji na barabara ndizo zinazowatesa wakazi wa kijiji hiki hususani wakina mama, lakini niseme tu kwamba suala la maji, nimefurahi kuna mfuko mnaendelea kuuchangia deni lililobaki ninalimalizia sasa na kuhusu barabara tayari nimeshaleta greda nitahakikisha barabara hii inatengenezwa, nisipotimiza ahadi hizi msinipigie kura mwaka 2015,"alisema Msigwa.

Aliwataka wamhukumu kwa ahadi zake kwani atayafanya hayo katika kipindi cha miaka miwili.
Katika mkutano huo, Msigwa alitoa Sh1.06 milioni kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji unaotekelezwa kwa ubia na wananchi pamoja na Serikali kwa msaada kutoka Benki ya Dunia.
Katika mradi huo wananchi walitakiwa kuchanga Sh3 milioni ambapo hadi mbunge anakwenda kufanya mkutano juzi walikuwa wamechanga Sh1.04 milioni .

Mwenyekiti wa kamati ya maji wa kijiji hicho, Emsy Silla alisema fedha zilitakiwa kuchangiwa na wananchi ni Sh3 milioni ambapo zingechanganywa na michango mingine kutoka Benki ya Dunia na Serikali ya Manispaa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo. Katika mkutano huo wakazi wa kijiji hicho walilalamikia kukosekana kwa huduma mbalimbali za kijamii katika kijiji chao ikiwamo huduma za afya na maji safi na salama wakidai hali hiyo inahatarisha maisha yao.

Akijibu hoja hizo mbunge huyo alisema suala la kukosekana kwa huduma ni tatizo la kitaifa na kwamba limekuwa likilalamikiwa katika maeneo yote nchini lakini akasisitiza uchache wa idadi ya wabunge wa chama chake unachangia kupitishwa bajeti isiyokidhi huduma za afya
 
Enyi CCM ni nani aliyewaroga? acheni uvivu na wivu kawatumikieni wananchi. Ndo maana JK aliweka mkeka siku ile alipopanda mti.
 
Huu ujtafiti unatilia mashaka makubwa sana maana kwa point uliyoandika kuwa tayari ameshachangisha 61millioni kununulia gari huoni kama huo ni mwanzo mzuri?Je, pamoja na mambo mengine kama mbunge ya maendeleo jimboni linaloonekana ameshindwa ni hilo tu la uchafu wa mji?

Katika maelezo yako nukuu ""Wakizungumza l;eo kwa nyakati tofauti wananchi wa jimbo la Iringa mjini walisem mji wa Iringa umeendelea kuzidiwa na uchafu "" Je ulifanikiwa kuwahoji wenyeji wangapi au uliitisha kikao?

maswahi hayo yananitilia shaka kubwa na makala yako na mwisho inaonekana kama kuna kampeni ya siri kuanza kumtambulisha Chilisosi kwa mbali

Jaribu kujibu hayo maswali ili sisi wananchi wa Iringa tujue ukweli uko wapi
Boss,
Iringa ni mji mkubwa sio kijiji OK?
Gari moja haliwezi kuzoa taka.
Siwezi kukuambia chilisosi ana mpango gani lakini haya ndio yatakuwa majibu yangu na sio moja na sitachangisha mtu
600

600

na kuna kitu kinaitwa wheel bins.
Let's see what happens next
YOU DONT NEED TO BE A GENIUS TO KNOW WHAT PEOPLE WANTS!
 
Boss,
Iringa ni mji mkubwa sio kijiji OK?
Gari moja haliwezi kuzoa taka.
Siwezi kukuambia chilisosi ana mpango gani lakini haya ndio yatakuwa majibu yangu na sio moja na sitachangisha mtu
600

600

na kuna kitu kinaitwa wheel bins.
Let's see what happens next
YOU DONT NEED TO BE A GENIUS TO KNOW WHAT PEOPLE WANTS!
Mmmh,, utakuwa umemuonea mchungaji. lakini nina wasi wasi asije akawa anatumia sadaka za watu kuzolea taka kinyume na kanisa
 
Je unafahamu kuwa Halmashauri ya mji wa Iringa ina magari mangapi ya usafi wa mji na kama unafahamu unajua yapo wapi kwa sasa??

Ni vizuri sana tena nakupa hongera kujitokeza kugombea nafasi yeyote lakini lazima uanze kwa kuweka kila kitu wazi ili iwe changamoto kwa wote wapiga kura na wewe utapata njia nyepesi ya kupita na tutakuamini sasa kwa mada hii utamshawishi nini mpiga kura??

Je ungekuwa wewe ndiye mbunge ungefanya nini zaidi ? maana msigwa miaka miwili tayari gari moja huoni akiendelea hivyo miaka kumi tutakuwa na magari ya kutosha?
 
Boss,
Iringa ni mji mkubwa sio kijiji OK?
Gari moja haliwezi kuzoa taka.
Siwezi kukuambia chilisosi ana mpango gani lakini haya ndio yatakuwa majibu yangu na sio moja na sitachangisha mtu
600

600

na kuna kitu kinaitwa wheel bins.
Let's see what happens next
YOU DONT NEED TO BE A GENIUS TO KNOW WHAT PEOPLE WANTS!
sioni welevu wako kwa kuweka magari ya taka ya miji ya uingereza, unaonesha ujuha wako. Taka za toka majumbani uingereza zinakusanywa na watu binafsi na kutiwa katika makasha meusi na kisha kuwekwa katika maghala hifadhi makubwa ambayo gari kama hiyo ulioionesha huja kuchukua, TANZANIA hatujafika hapo hoja zako ni za hovyo, Mhe MSIGWA aungwe mkono kwa alichokianzisha, ni jambo jema kwa maendeleo na hali yetu ya kitekenolojia.
 
AU UNAWEZA KUWANUNULIA HAYA MKUU, MBONA BEI POA SANA HAYO HUKO KWENU?
600
 
Boss,
Iringa ni mji mkubwa sio kijiji OK?
Gari moja haliwezi kuzoa taka.
Siwezi kukuambia chilisosi ana mpango gani lakini haya ndio yatakuwa majibu yangu na sio moja na sitachangisha mtu
600

600

na kuna kitu kinaitwa wheel bins.
Let's see what happens next
YOU DONT NEED TO BE A GENIUS TO KNOW WHAT PEOPLE WANTS!
heee chilisosi hayo ni magari ya kuzoea taka UK?? sio kwamba linazoa taka njiani hapana... bali kila nyumba inakuwa na dust bin yake siku ya kuzoa dustbin zinawekwa njee kisha gari lina pita mtaa baada ya mtaaa... sasa wewe wataka kutuambia kuleta hilo gari lina tukuwa solution tosha kwa shida walizo nazo wananchii wa iringa... kweli ukiwa ccm na akili zako zinakuwa finya kama ulivyo wewe.... kadanganye watu wa ccm sio watoto wa digital chadema
 
sioni welevu wako kwa kuweka magari ya taka ya miji ya uingereza, unaonesha ujuha wako. Taka za toka majumbani uingereza zinakusanywa na watu binafsi na kutiwa katika makasha meusi na kisha kuwekwa katika maghala hifadhi makubwa ambayo gari kama hiyo ulioionesha huja kuchukua, TANZANIA hatujafika hapo hoja zako ni za hovyo, Mhe MSIGWA aungwe mkono kwa alichokianzisha, ni jambo jema kwa maendeleo na hali yetu ya kitekenolojia.
Una uhakika na unayosema,
Hizi gari zinabeba uchafu wa aina zote na zina u compress ili ziweze kubeba mwingi, suala la mifuko ni chaguo lako lakini kama uchafu ukiwekwqa kwenye ma binss maalumu hili gari linazoa lenyewe na sio bei sana kama shangingi la mbunge, shangingi moja unanunua haya matatu, na mie nitafanya hili kwa mfano
 
heee chilisosi hayo ni magari ya kuzoea taka UK?? sio kwamba linazoa taka njiani hapana... bali kila nyumba inakuwa na dust bin yake siku ya kuzoa dustbin zinawekwa njee kisha gari lina pita mtaa baada ya mtaaa... sasa wewe wataka kutuambia kuleta hilo gari lina tukuwa solution tosha kwa shida walizo nazo wananchii wa iringa... kweli ukiwa ccm na akili zako zinakuwa finya kama ulivyo wewe.... kadanganye watu wa ccm sio watoto wa digital chadema
Na ukikutana nayo pale kitanzini, mshindo miyomboni utasemaje?
Tena utayaona kabla hata ya mwisho wa huu mwaka
 
Na ukikutana nayo pale kitanzini, mshindo miyomboni utasemaje?
Tena utayaona kabla hata ya mwisho wa huu mwaka
haya mkuu sipingi maendeleo ila hakika..kuna rafu itakuwa imechezwa sehemu... una tenda na riz1 nini na ndo maana ukatukimbia chadema UK??
 
Hautachangisha mtu kw sababu kuna mahali utakwapua eeh? Usije ukatuuzia twiga wetu wa ruaha na change kutununulia gari ya kuzoa taka.

Boss,
Iringa ni mji mkubwa sio kijiji OK?
Gari moja haliwezi kuzoa taka.
Siwezi kukuambia chilisosi ana mpango gani lakini haya ndio yatakuwa majibu yangu na sio moja na sitachangisha mtu
600

600

na kuna kitu kinaitwa wheel bins.
Let's see what happens next
YOU DONT NEED TO BE A GENIUS TO KNOW WHAT PEOPLE WANTS!
 
WAPIGA KURA JIMBO LA IRINGA MJINI WAMSHANGAA MBUNGE WAO



WAKATI mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (pichani )na viongozi wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) leo walijitolea kufanya usafi katika eneo la kitanzani mjini Iringa kama njia ya kuhamasisha usafi, wapiga kura wa jimbo hilo wameonyesha kutofautiana na uamuzi huo wa mbunge kufanya usafi huku baadhi yao wakidai kuwa jimbo hilo limemsinda kuongoza na ndio sababu ya uchafu kuzagaa kila kona ya mji .


" Mbunge wetu leo anajitolea kufanya usafi siku zote alikuwa wapi hadi uchafu unazangaa kiasi hiki mitaani .....tunamtaka Msigwa kufanya kazi kama wabunge wengine na kuachana na siasa za kuunga unga na kutafuta umaarufu kwa watu "


Wakizungumza l;eo kwa nyakati tofauti wananchi wa jimbo la Iringa mjini walisema kuwa mji wa Iringa umeendelea kuzidiwa na uchafu na kuwa mbali ya mbunge kujitolea kufanya usafi pamoja na wanachama wa Chadema ila bado hatua hiyo haiwezi kutatua tatizo la uchafu na badala yake uchafu wa Manispaa ya Iringa utaendelea kuwepo .


Juma Husein mkazi wa Kitanzini katika Manispaa ya Iringa alisema kuwa mbunge wao anatafuta umaarufu wa kisiasa na kusahau kuwa yeye ni mbunge wa jimbo la Iringa mjini na mwakilishi wa wananchi hao bungeni hivyo alipaswa kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa uchafu katika jimbo lake badala ya kufanya usafi kwa misingi ya kisiasa huku akitambua kufanya hivyo ni kujichongea mwenyewe kwa wananchi kuwa kumbe ameonyesha kushindwa kuongoza jimbo hilo na ndio sababu ya taka kuzagaa kila kona.


Husein alisema ni vema mbunge Msigwa kwenda kujifunza katika jimbo la Moshi mjini ambalo pia linaongozwa na mbunge wa Chadema na kuona kama mbunge huyo ametumia mbinu kama hiyo kusafisha mji ama kuna mbinu nyingine inatumika badala ya hiyo ya zima moto inayotumiwa na mbunge Msigwa sasa ya kukodi magari ya usafi.


Aidha alisema kuwa kwa kuwa Manispaa ya Iringa inakabiliwa na tatizo la magari ya kusomba takataka na uhaba wa vyombo vya kuhifadhia takataka mbunge Msigwa kwa kutumia mfuko wa jimbo alipaswa kuanza kushughulikia kero hiyo badala ya kukodi magari kwa siku moja ili kutaka kuonekana kuwa ni mchapakazi wakati siku zote yupo mjini Iringa na uchafu huo upo.


Kwa upande wake mbunge Msigwa alipoulizwa na mwandishi wa habari hizi kuhusiana na utaratibu huo alisema kuwa kazi ya mfuko wa jimbo si kwa ajili ya kusafisha mji na kuwa yeye ataendelea kusafisha mji kwa muda wa siku mbili hizi kabla ya kwenda bungeni .


Msigwa alisema kuwa kupitia ofisi yake tayari amekwisha changisha kiasi cha shilingi milioni 16 kwa ajili ya kununua gari ya kubeba taka katika Manispaa ya Iringa ili kupunguza tatizo la uchafu katika mji huo.


Afisa afya wa Manispaa ya Iringa Severin Tarimo alipotafutwa na mwandishi wa habari hizi ili kueleza mikakati ya Manispaa ya Iringa juu ya hali ya uchafu inayoendelea kuukumba mji huo alidai kuwa kwa sasa yupo likizo hivyo anayeweza kujibia hilo ni yule aliyemwachia ofisi.


"Nazungumza na nani ....sasa mimi nipo likizo bwana naomba uongee na mtu mwingine" alikata simu


MWISHO
Source FRANCIS GODWIN BLOG

My take,
Msigwa kuna mtu anaitwa Chilisosi anakuja hapo hivyo jiandae vyema
CHILISOSI FOR IRINGA 2015


Chilisosi unaonekana umechanganyikiwa. Wewe na magamba wenzako mnaoona Tanzania imeendelea, hamuwezi kuleta suluhisho lolote kwa maisha ya Tanzania. Retarded minds!
 
My take'

  1. Hii habari nayo ni ya kuungaunga tu
  2. Eti wapiga kura wa iRINGA UKISOMA ALIYEHOJIWA NI Hussein tu
  3. Tatizo limejulikana hapa kumbe mji umekua mchafu sababu AFISA MANISPAA YUKO LIKIZO... fool stop
 
Dar is stinkinkly filfthy despite all MP's, Ministers, Permanent Secretaries ana Presidents staying here
 
hee nani atapigia nyanya kura??
unaweka maoni ya ccm na wenye chuki ya maendeleo..
utaangushwa kaka kaa pembeni na siasa mkuuu umeshindwa weee
zero brain labda ndo watakupa kura
CDM dies in 2015 if you do not agree wait you will see
 
Back
Top Bottom