wapi tunakosea? turekebishe vipi?

Husninyo

Platinum Member
Joined
Oct 24, 2010
Posts
24,167
Reaction score
10,226
sisalimii maana maneno yatakuwa mengi! lol

wapenzi wa mmu, leo naomba tujadili ni wapi tunakosea katika mahusiano. watu wengi wamekuwa hawafurahii mahusiano, wakati wanaume wanatuona wanawake tupo kama mafisi tunajali maslahi zaidi na sie tunawaona wao kama manyani kudandia kila mwanamke. tunakosea wapi? binafsi naona kuna mambo tunakosea katika kuanzisha na kuendeleza mahusiano.

1. tunakosea katika kuchagua mpenzi sahihi.
ni ukweli ulio wazi kuwa kila mtu ana vigezo vya mpenzi anaependa awe nae. inapotokea mtu amekuwa single muda mrefu hujikuta ameanzisha mahusiano na mtu hata kama hana vigezo alivyokuwa anaviwaza awali. wakati upo kwenye mahusiano sasa antokea mtu mwenye vigezo vyote ulivyovitaka na hapo ndipo usaliti huanza. a nashauri utulie na utampata yule umfikiriae hata kama itakuwa muda mrefu kiasi gani, jitulize na epuka kufanya hili kosa.

2.kosa katika hatua ya awali kabisa. wengi huwa hatujadili aina gani ya uhusiano tunaoutaka. wakati mwingine anafikiria mambo ya "mpaka kifo kitutenganishe" kumbe mwenza wake anafikiria kula bata tu. ni vizuri kujadili mapema kuhusu aina ya mahusiano yenu.

3. tunakosea tunapotaka wenzi ambao wapo perfect katika kila kitu wakati tunajua hakuna mkamilfu. unapokuwa katika mahusiano ni vizuri kuyakubali na kuyavumilia mapungufu ya mwenzi wako badala ya kufikiria kumbadilisha kuendana na unavyotaka awe maana ni ngumu mno..


4.tunaposhindwa kuwa na muda na wapenzi wetu pia tunakosea.si ajabu kuona mtu anaspend muda mwingi na marafiki kuliko mpenzi wake ambae ni mtu wake wa karibu zaidi. waweza kuona ni kawaida lakini kadri tunavyojiweka mbali na wenzi wetu tunazidi kuchujisha penzi.

hayo ni baadhi ya tunayoyakosea, nakaribisha wana mmu tujadili wapi pengine tunakosea kwa pande zote mbili ke na me.

ushauri wa bure:
ruhusu moyo wako kupenda bila kujali umetendwa mara ngapi maana katika kila mahusiano unayoumizwa ni changamoto ya kukufanya uwe imara katika mahusiano yako yajayo.
 
WE SHOULDN'T GET IT TWISTED LOVE IS A BEAUTIFUL THING INDEED!!!!!!!!!!!!

Mi naona Fates and Privileges are entirely to blame!!!!!!!! YES! 100%

Watu vichecheee wanapataga watu waliotulia!!!!!!!! Mtu kavuruga jiji zima, anakuja kuolewa na mtu decent mpaka mnashangaaa! Mxiuuuuuuuuuu!

Unajituliza wewe,gundu la mibomu halikuishi! Hahahaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!! Yote maisha lakini!!!!!!!!!!!

But there is the men myth!!!!!! A man is not how you found him, rather how you mold him to your liking!!!!!!! Sasa hii hardwork ya turning Bozo's to good loving and ofcourse generous men we all like ndo wengi wetu mimi no 1 hatuipendi kabisaaaaaaa! Kuhonga amfundishe mwingine, kuchuna tuchune sie! Si Majangaa hayo!
 
sasa mtu mmekutana ukbwani utawezea wapi kummold?. siku zote mabadiliko huanzia ndani ya mtu mwenyewe labda kupiga goti sana mungu ambadilishe vingevyo ni kuyakubali tu madhaifu yake na ili maisha yasonge mbele vinginevyo uchape lapa umuachie majeraha ya moyo.
 
Njaa na maisha magumu inatibua sana maisha ya ndoa za kibongo na kiafrika kwa ujumla.
Scale ya njaa ninayoizungumzia ni ile hali ya kukosa kitu katika muda muafaka kutokana na ufinyu wa bajeti.
Mfano;unakuta mtu anatamani kuwa na pic nik na mwenzie ila ndo vile hela hamna,au miaka inakatika mpz hajawahi kumnunulia zawadi ambayo inaweza ki activate mapenz lakini wapi so mwisho wa siku image ya mpenzi inaanza kubadirika kichwani kwako kutoka cute baby to nyani.
Lingine ni swala la kujiringanisha maisha na wapendanao wengine kunafany mjione nyie mnaigiza wale ndo wanayaishi mapenzi hapa napo vurugu za kimpenzi hutokea.
Na mwisho ni kwamba ILI MAPENZI YAWE MATAMU AKILI ZA LAZIMA IWEKEZWE KWENYE PENZI LA SIVYO KILA SIKU WABONGO TUTAKUA TUNALIZWA N MAPENZI BILA KUMJUA MCHAWI WETU.
 


Ha ha ha tatizo waliotulia ni lack of opportunity,,, vicheche wanakuwa na sifa za ziada za kumfanya decent man aingie line...
 

Not necessarily! LOVE IS POWERFUL!!!!!!!!! Mambo mangapi umefanya jst because you love somebody, other wise in your right senses usingefanya??

Ukiyakubali madhaifu ni just for the time being, huweki kurizika na madhaifu ya mtu, unajizulumu! Afterall kama hujamwambia huyo mwenzio in a sense that it gets to his head kuwa hujarizika na mambo yake, How will he know?

Afu tabia ya kukaa na mtu hujarizika nae, iko sanaa kwa wadada sijui kwanini? Mwanaume akikaa na mdada hajarizika nae LAZIMA awe na wapembeni wa kufidia machungu yake. Ama there is an angle for him, labda mdada yuko loded na nini. Ila mwanaume kukaa na mdada out of GRATITUDE, CHARITY au GOODWILL ni mara chahce sanaaa!!!!!

PARDON ME BECAUSE I ALWAYS THINK LIKE A MAN, ACT AS A WOMAN!!!!!!!!!!
 

Hapa wengi sana wamekamatwa...na wengi wataendelea kukamatwa...nimemaliza
 
Ha ha ha tatizo waliotulia ni lack of opportunity,,, vicheche wanakuwa na sifa za ziada za kumfanya decent man aingie line...

AOUUUUUUUUUUUUUUCHHHHHHHHHHHHH!!!!!!!!!! YOU JUST DIDNT SAY THAT!!!!!!!!!!! MOST ESPECIALLY THIS JF, THE UNITED REPUBLIC OF GOOD, PERFECT, MOST RESPECTABLE, HOLLY, WELL MANNERED, DECENT, AND MOST SACRED WOMEN AND LADIES OF ALL TIMES!!!!!!!!!!!!!!


Though as much as i am tempted to disagree and deny but what you said IS THE BITTER TRUTH!!!!!!!!!!!!

Logically thinking Msichana hawezi tu kulala na wanaume wengi unless hao wanaume wengi wawe wamemtaka!!!!!!!! Though kutakwa is one thing, quality ya hao wanaokutaka ni another thing and kukubali is another, mimi namlaumu Wema kiluzi sanaa japo only God knows ningetakwa na wanaume wa Wema wanahonga Audi Q7 kama starlet maybe ningekuwa kicheche zaidi ya wema!!!!!! LOL! In the meantime wakati nawakataa wapiga debe na mibozo yangu, Wema is dispeakable and she should actually be ashamed of herself! Mbona mimi natakwa(japo wapiga debe ila natakwa vilevile) nakataaa! LOLEST!

We should see things from more than one perspective!
 

nakubaliana nawe 1oo%
ni viziri kujua mipaka ya mapenzi yenu kama ni kula bata au till death do us apart lasivyo nikuchezeana hisia,
pia kukubaliana na mapungufu ya mwenzio yeyote yatakayojitokeza safari ya mapenzi ina chamgamoto nyingi yaitaji uvumilizu busara na akili ilokomaa
 
ujue tatitop watu sio wavumilivu ....hata mbuyu ulianza kama mchicha..sasa sisi tunaanza tu kuwa wapenzi hata kabla ya kujuana vema...sasa katikati unajikuta upo na bomu ambalo dakika za kulipuka ndo zinakaribia....na pa kukimbilia huna,,unabaki hapo unachanika vipandevipande hufai tena...
mi naona kabla ya kuingia kwenye mahusiano tuwe at least marafiki wa kawaida tusomane...hii itasaidia maana wengine tunatofautiana saaaaaaana.....
mambo ya kudandia daladala ya mbezi mwenge wakati ulikuwa unasubiri kwenda kimara tuache...daladala ni nyingi sana mwenge ata za kimara zipo so tusubiri bila kuchoka
nawasilisha
 
Jamani mapenzi ni matamu acheni mchezo, unahisi kama unaishi peponi si peponi, kama hutakaa ufe vile.

Ila cha muhimu ni kuchagua mwenza mnayeona mambo katika mwanga mmoja, na si kwamba hamgombani. Mnagombana hadi mnarushiana mashati nje, lakini raha mnayopena inakuwa kubwa kuliko maumivu mnayopeana.

Kama watu mna mitizamo tofauti saaana ya maisha hata kubadilishana inashindikana, kwanza inatia uvivu.
Unamwambia mtu A wakati yeye yuko Q, haelewi haelewi, bora ujikalie kimya tu.
 
Hivi unadhani unakubali mapungufu ya mtu ti from no where?


Kuna watu ni worthy accepting their mapungufu jamani, the effort kwenye relationsjip huwa iko so comforting. Unamuona mtu anajitahidi kuonesha upendo wake kwa maneno na vitendo, why not accept mapungufu yake? Afterall hata wewe labda una yako.

 
Hiyo point 1 ndo muhimu zaidi ya zote. Kama unavyosema Husniyo, hamna mtu aliye perfect. Kwa upande wangu mimi naona mtu mtu awe na vigezo vyake ambavyo prospective mpenzi lazima zwe navyo, hivi ni vile ambavyo asipokua navyo hataweza kuvumilia. Pia awe na vingine ambavyo ni bonus, Hivi ni vile ambavyo mpenzi wake asipokua navyo anaweza akamvumilia. Mfano prospective mpenzi lazima awe mwenye hofu ya Mungu, lakini uzuri wa sura, mwili na utajiri ni bonus, kwamba awe navyo asiwe navyo still nitaweza kuvumiliana nae.
TATIZO NI VIGEZO VIPI TUNAVIPA UZITO ZAIDI?? NA JE WEWE MWENYEWE UNAJITAMBUA VIZURI KWAMBA HIKI NAWEZA KUKIVUMILIA NA HIKI SIWEZI??
 

kujilinganisha na kutaka muishi kama kina flani na lenyewe ni kosa, muhimu ni kuishi muwezavyo na kufanyiana yale yaliyopo ndani ya uwezo.
 
umeona eeeh kuna mtu mwingine chemistry yenu inamatch kitandani na moyoni tu huko kwingine hakuna kwako red yeye ni black whiye ni green yaani ......bora tu upige kimya mshare kilichowezekana period!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…