Husninyo
Platinum Member
- Oct 24, 2010
- 24,167
- 10,226
sisalimii maana maneno yatakuwa mengi! lol
wapenzi wa mmu, leo naomba tujadili ni wapi tunakosea katika mahusiano. watu wengi wamekuwa hawafurahii mahusiano, wakati wanaume wanatuona wanawake tupo kama mafisi tunajali maslahi zaidi na sie tunawaona wao kama manyani kudandia kila mwanamke. tunakosea wapi? binafsi naona kuna mambo tunakosea katika kuanzisha na kuendeleza mahusiano.
1. tunakosea katika kuchagua mpenzi sahihi.
ni ukweli ulio wazi kuwa kila mtu ana vigezo vya mpenzi anaependa awe nae. inapotokea mtu amekuwa single muda mrefu hujikuta ameanzisha mahusiano na mtu hata kama hana vigezo alivyokuwa anaviwaza awali. wakati upo kwenye mahusiano sasa antokea mtu mwenye vigezo vyote ulivyovitaka na hapo ndipo usaliti huanza. a nashauri utulie na utampata yule umfikiriae hata kama itakuwa muda mrefu kiasi gani, jitulize na epuka kufanya hili kosa.
2.kosa katika hatua ya awali kabisa. wengi huwa hatujadili aina gani ya uhusiano tunaoutaka. wakati mwingine anafikiria mambo ya "mpaka kifo kitutenganishe" kumbe mwenza wake anafikiria kula bata tu. ni vizuri kujadili mapema kuhusu aina ya mahusiano yenu.
3. tunakosea tunapotaka wenzi ambao wapo perfect katika kila kitu wakati tunajua hakuna mkamilfu. unapokuwa katika mahusiano ni vizuri kuyakubali na kuyavumilia mapungufu ya mwenzi wako badala ya kufikiria kumbadilisha kuendana na unavyotaka awe maana ni ngumu mno..
4.tunaposhindwa kuwa na muda na wapenzi wetu pia tunakosea.si ajabu kuona mtu anaspend muda mwingi na marafiki kuliko mpenzi wake ambae ni mtu wake wa karibu zaidi. waweza kuona ni kawaida lakini kadri tunavyojiweka mbali na wenzi wetu tunazidi kuchujisha penzi.
hayo ni baadhi ya tunayoyakosea, nakaribisha wana mmu tujadili wapi pengine tunakosea kwa pande zote mbili ke na me.
ushauri wa bure:
ruhusu moyo wako kupenda bila kujali umetendwa mara ngapi maana katika kila mahusiano unayoumizwa ni changamoto ya kukufanya uwe imara katika mahusiano yako yajayo.
wapenzi wa mmu, leo naomba tujadili ni wapi tunakosea katika mahusiano. watu wengi wamekuwa hawafurahii mahusiano, wakati wanaume wanatuona wanawake tupo kama mafisi tunajali maslahi zaidi na sie tunawaona wao kama manyani kudandia kila mwanamke. tunakosea wapi? binafsi naona kuna mambo tunakosea katika kuanzisha na kuendeleza mahusiano.
1. tunakosea katika kuchagua mpenzi sahihi.
ni ukweli ulio wazi kuwa kila mtu ana vigezo vya mpenzi anaependa awe nae. inapotokea mtu amekuwa single muda mrefu hujikuta ameanzisha mahusiano na mtu hata kama hana vigezo alivyokuwa anaviwaza awali. wakati upo kwenye mahusiano sasa antokea mtu mwenye vigezo vyote ulivyovitaka na hapo ndipo usaliti huanza. a nashauri utulie na utampata yule umfikiriae hata kama itakuwa muda mrefu kiasi gani, jitulize na epuka kufanya hili kosa.
2.kosa katika hatua ya awali kabisa. wengi huwa hatujadili aina gani ya uhusiano tunaoutaka. wakati mwingine anafikiria mambo ya "mpaka kifo kitutenganishe" kumbe mwenza wake anafikiria kula bata tu. ni vizuri kujadili mapema kuhusu aina ya mahusiano yenu.
3. tunakosea tunapotaka wenzi ambao wapo perfect katika kila kitu wakati tunajua hakuna mkamilfu. unapokuwa katika mahusiano ni vizuri kuyakubali na kuyavumilia mapungufu ya mwenzi wako badala ya kufikiria kumbadilisha kuendana na unavyotaka awe maana ni ngumu mno..
4.tunaposhindwa kuwa na muda na wapenzi wetu pia tunakosea.si ajabu kuona mtu anaspend muda mwingi na marafiki kuliko mpenzi wake ambae ni mtu wake wa karibu zaidi. waweza kuona ni kawaida lakini kadri tunavyojiweka mbali na wenzi wetu tunazidi kuchujisha penzi.
hayo ni baadhi ya tunayoyakosea, nakaribisha wana mmu tujadili wapi pengine tunakosea kwa pande zote mbili ke na me.
ushauri wa bure:
ruhusu moyo wako kupenda bila kujali umetendwa mara ngapi maana katika kila mahusiano unayoumizwa ni changamoto ya kukufanya uwe imara katika mahusiano yako yajayo.