Wapi nitapata koboko hapa Tanzania

Anakimbia hadi 16kph

Anaweza kusimama na kifikia 1.5m

Anaweza "kugonga" zaidi ya mara 20 kwa wakati mmoja

Ana sumu kali, akikugonga usipopata tiba ndani ya dakika 30 unafariki

Hufukuza magari na kujishikiza kwalo, ili ukisimama na kushuka tu, unaye!

Hukaa pia juu ya miti na kuvizia wapitao na kuwarukia kuwagonga utosini.

Nenda Katavi, njia ya sStalike - Kibaoni, waone wale wahifadhi, watakupeleka kwenye "kambi" ya koboko

Kila la heri.
 
Sawa kabisa ndio huyu nae muhitaji Mimi asante sana kwa maelekezo mazuri

#road to financial fredom
 
Hiyo ni nyara ya see serikali inaweza kukupeleka jela miaka 30 na faini juu
Mbona nyoka wanauliwa tu kawaida hata chatu kuna watu wanawamiliki wale wa ngoma za asili lakini hakuna polisi anawasumbua tena hadharani kabisa
 
Snake experts wanasema siku zote ukiona nyoka ana mdomo mweusi huyo ana sumu Kali sana na usimchezee akikugonga ni ndani ya dakika kadhaa unakata roho maana sumu yake inasababisha moyo kusimamia.

Huyu koboko ndio anaitwa black mamba watu wengi huwa wakiona nyoka mweusi ndio wanahisi black mamba, huyu ni hatari zaidi ya wote anakua Hadi mita tatu, akikupiga sumu hesabu sio zaidi ya nusu saa umekata roho. Very dangerous snake.
 
Habari wana jamvi

Natafuta koboko au hata ngozi yake nchi 6 x9 na kuendelea kama unaye au unayo bei isizidi laki tano kwa koboko mzima au laki mbili kwa ngozi ndefu na safi
Daah
Mkuu huyu mdudu huwa hawindwi bali watu hupambana naye asiishi karibu nao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…