Waoga wanavyoharibu nchi

Waoga wanavyoharibu nchi

mapesa yamejaa

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2021
Posts
1,404
Reaction score
3,420
Vijana wa sasa wamekuwa waoga sana wa kudai haki zao tofauti na kizazi kile cha wapigania uhuru kama kina Nyerere, Obote Kenyatta Kamuzu Banda, Mugabe nk.walitetea haki kwa nguvu zao zote waziwazi hadi wakawatoa wakoloni wakarudi makwao.

Cha ajabu hiki kizazi kilichozaliwa kuanzia miaka ya 70s hadi90s(nguvu kazi) ni kizazi cha waoga sana.hawajali hata wakinyimwa haki zao.Mfano tozo za simu tuliahidiwa ifanyike kwa mwaka mmoja lakini imekuwa endelevu na hakuna hata mmoja wa kuhoji

Mikataba ya kilaghai inaumiza wananchi.Mfano gesi ya mtwara tuliambiwa ingepunguza bei ya umeme nchini lakini imekuwa kinyume chake.Hivyo hivyo na huu mradi wa uchakataji na usindikaji wa gesi (LNG)na wenyewe tutapigwa tu.Mkataba wa kujadiliana na watu wawili hapo si ndo kupigwa kwenyewe.

Pamoja na hivyo, hamna hata mmoja amehoji.wasaidizi ni kusifu tu.uoga umezidi sana tofauti na wakina nyerere walipinga hadharani hii mikataba ya kilaghai pamoja na kodi za kihuni kama hizi. watawala waliojifanya wagumu cha moto walikiona.hawakuogopa cha policcm wa enzi hizo wala chombo chochote cha dola.

Kwa sasa huduma zote za umma ukianzia hospitali,shule nk.zote niza kusuasua.watawala wao hawaziboreshi kwa kuwa haziwahusu.Wao hutumia kodi zetu kwenda nje pamoja na watoto wao kupata huduma hata ambazo hazisitahili(malaria kwenda kutibiwa ulaya).yote haya yamesababishwa na aina ya jamii yetu kuwa ya waoga sana tofauti na jamii ya enzi za nyerere

Wewe mdau karibu tushauliane tufanye nini ili tuwe na watu jasiri na wazalendo kama wa enzi za wapigania uhuru?Maana kwa kizazi cha sasa ni cha kusifia tu hata pale pasiposifika.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa sasa uoga umezidi sana tofauti na kipindi hicho cha wapigania uhuru.kwa sasa ni kusifu tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani kipindi kile hakukua na uoga??
Ingekua hivyo tz tusingekua hapa ndgu yangu.

Hii serikali toka enzi hizo imewajengea uoga wananchi wake, ndio maana hata historia za serikali ya mwalimu ni nzuri nzuri tu, mpaka unashangaa kama mwalimu aliku vizuri namna hiyo ilikuaje nchi ikawa maskini kiasi hiki!!

Ndipo unakuja kujua kua ni uoga wa wanachi kuogopa kuhoji, mtawala anaandikwa vile atakavyo yeye na sio muonavyo nyie waandishi.
 
Wanaojiita wapigania uhuru wa Kiafrika wengi walikuwa tu wanataka Mzungu aondoke ili wawageuze waafrika wenzao watumwa.

Ona ANC ya S.A kimeguka chama cha ufisadi wanaojiita wapigania uhuru wanautafuna S.A, kule zimbabwe yake yale, hapa TZ labda JKN tu ndiye aliondoka akiwa na mali za kawaida na wala hakuwaacha watoto wake kwenye system,
 
Vijana wa sasa wamekuwa waoga sana wa kudai haki zao tofauti na kizazi kile cha wapigania uhuru kama kina Nyerere, Obote Kenyatta Kamuzu Banda, Mugabe nk.walitetea haki kwa nguvu zao zote waziwazi hadi wakawatoa wakoloni wakarudi makwao.

Cha ajabu hiki kizazi kilichozaliwa kuanzia miaka ya 70s hadi90s(nguvu kazi) ni kizazi cha waoga sana.hawajali hata wakinyimwa haki zao.Mfano tozo za simu tuliahidiwa ifanyike kwa mwaka mmoja lakini imekuwa endelevu na hakuna hata mmoja wa kuhoji

Mikataba ya kilaghai inaumiza wananchi.Mfano gesi ya mtwara tuliambiwa ingepunguza bei ya umeme nchini lakini imekuwa kinyume chake.Hivyo hivyo na huu mradi wa uchakataji na usindikaji wa gesi (LNG)na wenyewe tutapigwa tu.Mkataba wa kujadiliana na watu wawili hapo si ndo kupigwa kwenyewe.

Pamoja na hivyo, hamna hata mmoja amehoji.wasaidizi ni kusifu tu.uoga umezidi sana tofauti na wakina nyerere walipinga hadharani hii mikataba ya kilaghai pamoja na kodi za kihuni kama hizi. watawala waliojifanya wagumu cha moto walikiona.hawakuogopa cha policcm wa enzi hizo wala chombo chochote cha dola.

Kwa sasa huduma zote za umma ukianzia hospitali,shule nk.zote niza kusuasua.watawala wao hawaziboreshi kwa kuwa haziwahusu.Wao hutumia kodi zetu kwenda nje pamoja na watoto wao kupata huduma hata ambazo hazisitahili(malaria kwenda kutibiwa ulaya).yote haya yamesababishwa na aina ya jamii yetu kuwa ya waoga sana tofauti na jamii ya enzi za nyerere

Wewe mdau karibu tushauliane tufanye nini ili tuwe na watu jasiri na wazalendo kama wa enzi za wapigania uhuru?Maana kwa kizazi cha sasa ni cha kusifia tu hata pale pasiposifika.


Sent using Jamii Forums mobile app
VIJANA WAJINGA, WAPENDA NGONO, WALEVI , WARAHIBU WA MADAWA YA KULEVYA , VIJANA WASIO NA MAARIFA , HEKIMA NA AKILI, VIJANA WASIO JUA HISTORIA YA TAIFA HILI LIMETOKA WAPI NA LINAKWENDA WAPI, VIJANA WASIO NA ELIMU , VIJANA WASIOTAMBUA HAKI ZAO NI ZIPI, VIJANA MALAYA MALAYA, VIJANA MACHAWA WA VIONGOZI WAPUMBAVU, VIJANA WALAMBA MAKALIO YA VIONGOZI WAPUMBAVU, VIJANA WAPUMBAVU AINA HII YA VIJANA IMEJAZANA SANA KATIKA TAIFA LETU LA TANZANIA KWA HIYO USITEGEMEE VIJANA WA NAMNA HII KUFANYA UKOMBOZI WA PILI WA TAIFA LETU LA TANZANIA HAWA VIJANA WA NAMNA HII WANAHITAJIKA ZAIDI KUWANYIWA UKOMBOZI WA KIFIKRA KABLA YA YOTE.
 
Chadema wanaamini Mbowe ndie mtu asiye muoga lakini mbele ya asali Mbowe ni nani aache utaaam
 
..sikuwahi kusikia Nyerere kachezea kichapo toka kwa jeshi la polisi la muingereza.

..pia sikuwahi kusikia kama wakati wa ukoloni wa Muingereza, wakati wa kudai uhuru, kulikuwa na kundi la "wasiojulikana" linaloteka na kutesa wanaharakati wa Tanu.
Exactly
 
Uoga unaouona unatokana na hofu.

Sio kwamba Tanzania watu ni waoga ila hofu imetanda vichwani mwao, hofu ya kupoteza maisha ama kupata ulemavu wa viungo, hofu ya kuacha familia zikitaabika, hofu ya kubambikiwa kesi na kuswekwa jela.

Shida kubwa ni utawala wa chuma uliopo kwa muda mrefu ambao umefanya watu waone kudai haki zao ni kama kufanya jinai. Anzia mashuleni huko, mwalimu anaweza akakufanyia ndivyo sivyo ila ukilalamika utaonekana mtukutu. Wanaku
expel na katika hilo tayari inajenga impression kwa wengine kuwa kulalamikia uonevu ni kosa unaweza ukafukuzwa, hivyo watoto wanavumilia humiliation wakipewa moyo kuwa hawatadumu milele hapo shuleni.

Ukichunguza trend utaona hata wanafunzi wa shule kama Azania, Jitegemee za miaka ya 98-O3.. Ni tofauti sana na watoto wa kileo. Tofauti kubwa ni kujitambua mapema na kuelewa haki zao na kuzisimamia. Watoto wa zama hizi wanafundishwa kuvumilia uonevu kwa kigezo ati kuwa ni nidhamu matokeo yake hata kujieleza ni ngumu kwa kuwa anaogopa ataonekana mtukutu na watukutu huadhibiwa na kufurushwa.

Hili limeenda deep zaidi na kufikia uraiani ambako raia tunazuiwa kupinga udhalimu kupitia sheria ambazo zimewekwa mahususi kabisa kugandamiza raia. Unaambiwa iko haki ya raia kufanya maandamano ya amani ila haki hio ni lazima iwe approved na kibali maalum cha polisi ambao hao
polisi wenyewe hawawezi kukupeni kibali ikiwa lengo ni kuilalamikia serikali. Hilo linagusa maslahi yao kwahio lazma watagoma kuwapa na mkilazimisha haki yenu watakuja kuwafumua mabomu na maji ya kuwasha.

Kwa minajili hio hofu hujengeka na kuzaa uoga. Uoga ukizidi sana huzaa utii wa kinafiki ambao ndio stage tuliopo sasa. Deepdown hakuna anayeridhika na hali hii ila hakuna aliyetayari kusimama imara na kuanzisha movement sababu ataumizwa. Unafiki ndio umezaa machawa na keyboard warriors.
 
..sikuwahi kusikia Nyerere kachezea kichapo toka kwa jeshi la polisi la muingereza.

..pia sikuwahi kusikia kama wakati wa ukoloni wa Muingereza, wakati wa kudai uhuru, kulikuwa na kundi la "wasiojulikana" linaloteka na kutesa wanaharakati wa Tanu.
Shida inaanziaga hapa na jeshi la polisi liko tayari kufanya uhuni huo wa kuumiza raia kwa sababu yeyote ile na kigezo common watasingizia mnalengo la kuleta taharuki.

Kifup nchi haiongozwi na katiba hii ila maslahi ya watawala na daraja kati ya watawala na raia ni hao
askari. Hivyo askari wakiulizwa mnalipwa na nani? CCM...Haya fanyeni kazi yenu. 😂
 
Back
Top Bottom