Wanywaji wa bia na wavutaji wa sigara, mnapaswa msusie, ili kushinikiza wapunguze bei!

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Imekuwa kawaida ya serikali hii ya magamba kila wakati wa kutangaza bajeti eneo peke yake wanalolionea kulikamua ni kwa wanywaji bia na wavutaji wa sigara, nadhani ni vyema tukawaambia magamba kuwa tumeonewa kiasi cha kutosha.

Hii serikali badala ya kuchukua kodi kwenye migodi ambao wanatuibia kwa kutuachia shilingi 4 tu katika kila 100, sasa wao wametung'ang"ania wanywaji bia na wavuta sigara, ni vyema tukaiga mfano wa wanywaji wa Kibuku kitu ambacho waliwahi kukifanya mwanzoni mwa miaka ya 90, ambapo hatimaye serikali ilisalimu amri kwa kushusha bei ya kibuku!

Mkakati ni rahisi tu ni vyema zikatumika simu zetu za mkononi na kuwa-sms wale mnaowaona ni mashabiki wa bottle na kwa kuwa hata wabunge wengi wamekerwa sana na mtindo huu wa serikali yetu kujiendesha kwa pesa ya wanywaji wa bia na wavuta sigara tu naamini watapoona bia hazitoki watasalimu amri kwa kushusha bei ya vileo!!
 
Hapana bwana hapo ndio pakukusanyia kodi me nadhani wangepukunguza kwenye vitu vya msingi sio ulivyovitaja
 
Mystery, wewe huwapendi wafanyakazi. Usiwe mchochezi. Inakumbusha miaka fulani mabpo wanywaji wa kibuku waligoma na serikali inanywea na kupunguza bei ya kinwaji hicho. Lakini bia ni babu kubwa watakaogoma ni sawa na wahujumu uchumi kwa sababu kila kitu kitasimama.
 
Serekali wanakosea sana kwenye hili suala, wanadhani wanawakomoa wanywaji na wavutaji ila ukweli ni kwamba wanakomoa na kutesa familia nyumbani, mnywaji hata siku moja hatabadili au kupunguza kiasi cha kinywaji au fegi, kinachotokea ni ku adjust budget ya home ili unywaji uendelee, maisha yanakuwa magumu zaidi na zaidi manyumbani kama serekali haijui.
 
Back
Top Bottom