GE2025 Wangapi Tarehe 29 October 2025, Tutaandamana Mtandaoni au Moyoni

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

GenuineMan

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2017
Posts
7,068
Reaction score
16,380
Wale ambao tunaona mambo hayaendi sawa.

Tunatamani kuandamana ila bado hatuko tayari kutoka barabarani, tunaogopa kupingwa na polisi, tunaogopa familia zetu tutaziachaje.

Tunaogopa kuumizw au kufa.

Uwanja ni wetu, tujuane keyboards warriors, tusione haya kukiri kuwa sisi ni waandamanaji wa mtandaoni au wa kimoyomoyo.

Kama unamjua keyboards warrior mwenzio mtaje.
 
Hakuna mtanganyika atakayeandamana in field, wote tutaandamana online.

Kwenye mapambano huwezi kusema nasubiri ifike 29 ndo nipambane wakati adui anakupiga kila dakika.
 
Mimi nakupongeza kwa kua mkweli, kiuhalisia Jf hii iliyojaa Nyumbu waoga hamna atakae toka hata mmoja, nyumbu hata zikiwa elfu 10 zinaweza kukimbizwa na kitoto cha simba na zote zikatawanyika kwa uoga, siku zote usiwaamini nyumbu kwa umoja wao unaouona kwa macho zinaweza kukuingiza mkenge.

Hizi nyumbu zilishawahi kumuingiza mkenge Mbowe akaandamana peke yake, zimemuingiza mkenge Lissu leo yuko mahabusu miezi 6 hata kuandamana haziwezi.

Hizi nyumbu ndo zilikua zinajaza comments kwa Mdude, soka na wengine ila leo hii nyumbu zimejificha zinachungulia kwa mbali bila msaada wowote.
 
Binafsi natamani maandamano kama yale ya Gen Z ya wakenya, au kilichofanyika kwenye mwendokasi hapo Magomeni.

Maandamano ambayo ni ya wananchi wenyewe kuamua baada ya kuchoshwa na upumbavu wa serikali bila kusukumwa na chama chochote cha siasa, maandamano kama haya nayaunga mkono 100% na mimi lazima utanikuta kwenye hayo maandamano.

Ila maandamano ambayo kuna chama cha siasa kinayapigia debe mana wanajua wao pia watanufaika kupitia hayo maandamano, huwezi kunikuta kwenye huo upumbavu.
 
Kwa vyovyote vile hata yawe maandamano ya wananchi kuchoshwa bado wapo watu binafsi na vyama vya siasa vitanufuika nayo. Hata hao Genz wa Kenya walipo andamana wapo watu na vyama vilifaidika.
 
Kwani kuandamana moyoni na mtandaoni lazima kungoja October 29?! Si mnaweza kuandamana kila siku na usiku wake au kwa sasa hamna sababu za kuandamana hadi October 29?!
Lisu yuko ndani, chama chenu kimefutiwa ruzuku na kuzuiwa kufanya shughuli za kisiasa , KWANINI HAMUANDAMANI?!
 
Kwa vyovyote vile hata yawe maandamano ya wananchi kuchoshwa bado wapo watu binafsi na vyama vya siasa vitanufuika nayo. Hata hao Genz wa Kenya walipo andamana wapo watu na vyama vilifaidika.
Ile ishu ya mwendokasi, chama gn cha siasa kilichonufaika nayo?

Point yangu n sitaki chama chcht kuhusika wala kuunga mkono bali ni yawe maandamano ya wananchi kuamua wenyewe.
 
Maandamano ambayo ni ya wananchi wenyewe kuamua baada ya kuchoshwa na upumbavu wa serikali bila kusukumwa na chama chochote cha siasa, maandamano kama haya nayaunga mkono 100% na mimi lazima utanikuta kwenye hayo maandamano.
Aione Lucha ambaye akisikia neno maandamano, akili yake finyu inakimbilia chadema na kuona yeye na mboga mboga wenzake hayawahusu.
Mtanzania yeyote bila kujali chama,dini wala kabila tunapaswa kutafuta haki na kusimama nayo..
 
Nimekwambia tutoke mimi na wewe leo tuandamane sema mwenyewe tunaanzia barabara ipi
 
Ile ishu ya mwendokasi, chama gn cha siasa kilichonufaika nayo?

Point yangu n sitaki chama chcht kuhusika wala kuunga mkono bali ni yawe maandamano ya wananchi kuamua wenyewe.
Kwahiyo mkianzisha na chama cha siasa kikasapoti mnaachana nayo? 🤭

although, I think ni vizuri kwa wananchi kuwa msitari wa mbele kwa ujumla wao, ni vigumu kuwaondoa wanasiasa kwa maana nao ni victim wa mambo yanayodaiwa..
 
Kwahiyo mkianzisha na chama cha siasa kikasapoti mnaachana nayo? 🤭

although, I think ni vizuri kwa wananchi kuwa msitari wa mbele kwa ujumla wao, ni vigumu kuwaondoa wanasiasa kwa maana nao ni victim wa mambo yanayodaiwa..
Mkuu, hv unaelewa nachoandika?
 
Labda wakenya ndo wataandamana ila sio hawa ng’ombe wa Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…