Hii haihitaji moyo, inahitaji mapenzi kutoka pande zote mbili. Mwanaume yeyote anaejitambua, mwenye akili, mwenye mapenzi na alie na mtazamo chanya wa maisha anapendeka tu.
Hii haihitaji moyo, inahitaji mapenzi kutoka pande zote mbili. Mwanaume yeyote anaejitambua, mwenye akili, mwenye mapenzi na alie na mtazamo chanya wa maisha anapendeka tu.
Hapana, mimi binafsi nimeshashuhudia watu wameoa na kuolewa na walemavu. Unamkumbuka yule msanii (Jembe?) wa ze comedy? Mkewe mlemavu, simkumbuki jina? Hudhani kama jamaa angekuwa na mwanamke mrembo si ajabu angemuacha kitandani akawahi wazee wa mjini?
Shida ya ulemavu ni kumpata mwenye kujiamini na asietumia ulemavu wake kama sababu ya kushindwa maisha. wasiokuwa walemavu wanafulia kiuchumi, wanaugua, wanakuwa cheated, wanapoteza kazi etc. ulemavu ni limitation tu ya baadhi ya mambo, na sio kikwazo!
Japokuwa mimi si mwanamke lakini naamini wapo wanawake wengi tu wenye moyo huo. Nimeshapata kuwafahamu wanaume kadhaa wenye ulemavu lakini wana wake zao ambao ni wakamilifu wa viungo.