Nilipopata hiyo sms wala sikusumbuka.
Nili-edit sms ya M-pesa niliyokuwa nimetumiwa pesa, pale kweny kiasi nikaweka 1mil, then nika-edit muda....nikamtumia
Then nikamtumia sms nyngn nikamwambia Samahani Kwa Kukucheleweshea Pesa Yako.
jamaa yangu mmoja alikua anadaiwa na mama mwenye nyumba wake sasa siku akampigiwa na yule mama kwamba lini atampa hela yake jamaa akasema nakutumia sasa hivi...ile kukat simu ikaingia msg km hyo jamaa akatuma bila kuuliza ilikula kwake
Kwangu imeshakuja mara 4 halafu kila mara anamalizia 'fanya haraka nipo kwa wakala' .Siku moja nikatuma sms kumuuliza hela gani hiyo hakujibu .Kwangu huwa inakuja kwa namba ya Tigo
Mi nimemkamulia matusi hadi akakata simu eti anatuma sms rahisi ile pesa tuma kwenye namba hii simu yangu inasumbua mpesa namuuliza pesa ipi anauma maneno kala matusi ya haja hajarudia tena
Mimi juzi nilikumbana na mtu anadai kilimo chake kigumu ...mara anataka vifaa kkoo sijui mara pesa walituma Yaani mtu hasiye eleweka ..mimi nikamwambia nashukuru sana maana nilikuwa natafuta mtu wa kafara maana mganga alisema atakayenipigia simu nimtoe ,nikasikia twitiwitiiiii
Wafanyakazi wengi wa huduma hizi ni matapeli na wana mtandao kama wauza unga
Yaani hakuna haiba ya kazi na heshima siku hizi
Ni kama bank, zamani wafanyakazi wanaheshimika hata chai unaweza kumkaribisha lakini siku hizi unawapita tu maana wamekuwa watu wa kudondosha elfu kumi chini
Yaani millennium imekuja na mambo ya ajabu sana kila sekta ni wizi tu aaaghhh