Wanawake tuna maneno

Dejane

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2014
Posts
51,003
Reaction score
72,292
Hivi sisi hatuwezi kuwa marafiki mpaka tusemane vibaya, yani usipomsema mwenzio unaona siku haiendi au inakuwaje, unakuta unakuwa na rafiki mnasaidiana kwa hali na mali lakini au akiwa na shida unamsaidia tena vya kwake mchoyo kweli, unajitoa kwa kila kitu lakini utakuta linakusema vibaya sijui ni wivu, chuki hata sielewi aisee!

Hii tabia tunayo sana wanawake tubadilike jamani, maisha yashakuwa magumu maneno ya nini, mimi nishaamua sasa niwe mwenyewe tu sitaki marafiki maana ukigeuza tu mgongo wauaji, halafu ukitaka kukumbuka kitu ambacho umemuudhi huoni au ukimuuliza anasema hakuna kitu yaishe tu nisamehe.

Au wengine bila kusema wenzao siku haziendi vizuri "lazima tuji control "
Yaani nishaamua toka mwaka jana hakuna rafiki yeyote kushika simu yangu, wala kujua password, misele yangu napiga kimya kimya, sitambulishi mpenzi wangu tuonane wenyewe tu. Maana maneno mengi mpaka unachoka.

Wanawake sisi ni kibokooo
 
Wewe ndo unashtuka saiviii poleeee!!!
Mie sinaga rafiki wa kike kabisaa wala sitaki, ukiwa na shida nitakusaidia nawe nikiwa na tatizo nisaidie lakini sio ushost wa kupeana sijui simu, pochi, nguo urafiki wa hivyo siutaki kabisaa kila mtu afanye yake, hayo mengine ni unafiki tuuu
 
Mchumba unae lkn?!...
 
Mkuu umechelewa,mimi sina rafiki nina watu niliozoeana nao tu!
 
Wanawake wengi field yao ipo limited sana, hawapo sana kwenye mambo ya mpira, pombe, muziki, kazi na pia kuongea 'hard topics' kama elimu, siasa, sera mbalimbali sio sana, so ndio maana mada nyingi (sio zote) zinakuwa ni kuhusu mahusiano tu, yawe kifamilia, kimapenzi yaani umbea in general , na mazungumzo hayahusu kusemana vibaya tu, kumsema kupo mara nyingi sababu kumsema mtu vibaya kisaikolojia huwa kunaleta faraja flani hivi hasa ukiwa na matatizo....
 
Kuna wengine unakuta mpaka kuvaa wanavaa sare na usiombe siku watibuane watatoleana siri zao zote mpaka za ndani.
 
Haya kwakuwa hamtakani urafiki nyie kwa nyie njooni kwangu tuwe marafiki na mgegedo lazima Maana hakuna kilio pasipo machoziπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Dinazarde umeongea ukweli haswaa
Hakuna watu wabaya km marafiki feki hasa wanawake sijui katuloga nani mi mwaka jana nilipiga chini wote. Sababu izo izo wanakuchekea wakigeuka wanakuchoma mishale... Bora uwe na marafiki wakiume 10 klk kuwa na rfk mnafiki wa kike mmoja.....
Pole sana.
 
Kuna wengine unakuta mpaka kuvaa wanavaa sare na usiombe siku watibuane watatoleana siri zao zote mpaka za ndani.
Hamna ushost mbaya kama huo, wanawake bwanaaa sie wenyewe kwa wenyewe hatupendani ni wachache saaana wenye urafiki wa kweli.
Rafiki yako wa karibu ndo muuaji wako wa siri, kwa ninayoyaona kwa wenzangu ushost upite tu mbali na mie
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…