uzoefu unaonyesha kuwa ndoa ambayo mke ana pato kubwa kuliko mume haidumu na ikidumu inakuwa na migogoro mingi kwani kwa pato mke atataka amiliki nyumba na awe mwamuzi mkuu.
1. Mwanaume kuongozwa na mwanaumke nyumbani lazima una matatizo (Mwanaume atamtawala Mkewe - Refer Eden)
2. Kwenye jamii yetu hii mwenye pesa ndio ana maamuzi - Hekima ya masikini haisikilizwi -Refer Proverbs.
3. Aliye nacho Huongezewa, na asiye nacho hata kile kidogo alichodhani kuwa anacho... atanyang'anywa.. Ajitahidi KUWANACHO
4. Mwanamke akikuzidi kila kitu, Hio imekula kwako (akuzidi hela, elimu, akili, sijui nini hio imekula) Pride at it peak
5. Mwanaume ndio kichwa cha Nyumba.. Ukiangalia tu kirahisi hatuna taifa lolote masikini duniani lenye sauti ila yenye hela ndio yana sauti... Sasa wewe mkeo ndio kashikilia usukani unategemea sauti uitoe wapi?
6. Mtaji wake, kila kitu chake... Bila aibu unalaghaika unaenda kumkuzia mtaji... ona yatokanayo... hujaongeza hapo hata shs tano unasema biashara yetu... wewe na nani? Unawafahamu akina hawa au unawasikia? With all due respect I have enough back ups..... One or two among 20 ndio wanaweza kuwa na uwezo kifedha juu ya mwanaume bado wakajishusha... otherwise Money corrupts
7. Mwanaume always ni wajanja... huyu alilala.
So what is your suggestion, conclusion and the way forward?uzoefu unaonyesha kuwa ndoa ambayo mke ana pato kubwa kuliko mume haidumu na ikidumu inakuwa na migogoro mingi kwani kwa pato mke atataka amiliki nyumba na awe mwamuzi mkuu.
Tatizo sio ubabe ila wanaume wengi siku hizi wanapenda kulelewa, mwanaume mzima na akili timamu utaongozwaje na akili ya mwanamke na umeambiwa wewe ni kichwa cha nyumba? Mnatakiwa kuwa strong kweli kweli kuongoza akili ya mwanamke wa sasa. Bila hivo mtaishia kulialia kila siku.
Hakuna mwanaume mwenye uwezo wa kumuongoza mwanamke, wanawake wana hekima, ujanja na ulaghai. Mwanamke mara nyingi huamua kujishusha ili maisha yaende. Wanaume ni JASIRI uwanja wa vita lakini si ktk uwanja wa mapenzi.Kumbuka ya Samsoni na Delila au ya Adam na Eva na tunda la katikati.
Hakuna mwanaume mwenye uwezo wa kumuongoza mwanamke, wanawake wana hekima, ujanja na ulaghai. Mwanamke mara nyingi huamua kujishusha ili maisha yaende. Wanaume ni JASIRI uwanja wa vita lakini si ktk uwanja wa mapenzi.Kumbuka ya Samsoni na Delila au ya Adam na Eva na tunda la katikati.
Hayo maandiko yamewekwa ili ujifunze. Hadithi inatolewa unaulizwa umejifunza nini, siyo muhusika alifanya makosa basi wewe ukafanye tena yale makosa.
Kuwa kichwa cha nyumba ni pamoja na kuongoza familia yako. Kama ingekuwa haiwezekani basi maandiko yangesema mwanamke ni kichwa cha nyumba.
Kuwa kichwa cha familia hakutufanyi kuwa ndio ALFA NA OMEGA. Mwanaume anao wajibu wa kuunganisha Maono ya wanafamilia ili yaweze kuwa na matokeo chanya na katika hili kushauriana ni jambo la msingi. Kina mama sio viumbe DHAIFU, PENGINE DHANA hii ilitumika ili kuleta amani na maelewano kwani wahenga walisema, ''Mafahali 2 hawakai zizi 1''.
Sasa wewe umetoa details nyingi kiasi kwamba inakuwa rahisi sana kumjua huyo jamaa yako kama mtu akiamua kufuatilia. Jifunze kuficha ficha details.
Kuna rafiki yangu niliyemaliza nae chuo kikuu cha ardhi mwaka 2010, mimi na yeye wote tulikuwa tunasoma architecture baada ya kuhitimu rafiki yangu(jina lake naliifadhi) alifanikiwa kupata kazi katika kampuni moja hapa D'salaam, na muda haukupita sana kwani mwaka 2011 kwenye mwezi oktoba alifunga ndoa na mwanamke aliyempenda(jina naliifadhi).
Yule mwanamke aliyemuoa alisomaga mambo ya biashara na hata baada ya kuingia kwenye ndoa alikuwa akijishughulisha na mambo ya biashara wakati mume wake akiwa ameajiriwa, mambo ya biashara kwa yule mwanamke yalimuendea vizuri sana na akawa anapata pesa nyingi sana akamshauri na mume wake aache kazi wafanye wote biashara na yule mume kwa kufikiria kipato alichokuwa anakipata mke wake kutoka kwenye biashara akaamua aache kazi na wafanye wote biashara.
Haukupita mda mrefu sana ndoa yao iliyumba sana kiasi cha kwamba mwanamke akamwambia mume wake mimi na wewe basi, kuanzia leo tusijuane. Mwanaume(rafiki yangu hakuamini) akaamua kumpigia simu mama mkwe wake naye alijibu hivi alichosema mtoto wangu ndo hicho hicho na mimi nipo huko huko, kumbe ata nyumba waliyokuwa wakiishi ilikuwa ya mwanamke kwa hiyo jamaa ilibidi aondoke pale na arudishe mpira kwa goli kipa( aende nyumbani kwa wazazi wake).
Amerudi nyumbani kwa wazazi wake akiwa hana kazi na akiwa hajui pakuanzia.Ndoa ikawa imevunjika baada ya kudumu kwa miaka mitatu tu.
Mhhh ... Hakika wanawake tuna sheeeda. Tumeoana wewe umeajiriwa mm nafanya biashara baada ya 2 years biashara imependeza imekuwa maradufu kumbe inakuwa imekula kwako Tized dahhhh sasa ulitaka nikifanya biashara isifanikiwe au? Kuna vitu vinakuwa judged in a very wrong way....