Habari za humu ndani,
Baada ya kusherehekea sikukuu ya wanawake duniani ambayo kwa upande wangu sijaona wanawake wenyewe wakishiriki kikamilifu.
Sasa tuendelee na harakati za maisha kama kawa. Mwenzenu kuna jambo linanitatiza au pengine mimi napenda kupewa sifa sana mnishauri niepuke hili kama nimepitiliza.
Au kwa sababu pesa zenyewe nazipata kwa kuunga unga sana, jasho na mchoko wa kufa mtu na wakati mwingine kashifa, fedheha na matusi huyapata katika harakati za kutafuta kipato.
Mara nyinga si mara zote huyu mwenzi wangu hata nimfanyie nini, pesa si nyingi nazompa lakini najitahidi kadiri ya uwezo wangu lakini kwake neno asante baba fulani, au asante kwake ni jambo gumu kwake.
Sasa naanza kukata tamaa kwamba mwenzangu hana shukurani, au mimi ndio napenda sana kushukuriwa.
Je nifanye nini? Au ni tende wema na kwenda zangu? Je kuna wanawake wa aina hii na si kwangu tu.
Waswahili wanasema asante ni kuomba tena, mtu kwangu akiniambia asante nafarijika sana najisikia raha moyoni, naona kile nilichofanya kimeleta impact kwa mtu huyo hata kama asante yake haitoki moyoni mimi sijali.
Karibuni kwa mjadala maoni na michango yenu.
Baada ya kusherehekea sikukuu ya wanawake duniani ambayo kwa upande wangu sijaona wanawake wenyewe wakishiriki kikamilifu.
Sasa tuendelee na harakati za maisha kama kawa. Mwenzenu kuna jambo linanitatiza au pengine mimi napenda kupewa sifa sana mnishauri niepuke hili kama nimepitiliza.
Au kwa sababu pesa zenyewe nazipata kwa kuunga unga sana, jasho na mchoko wa kufa mtu na wakati mwingine kashifa, fedheha na matusi huyapata katika harakati za kutafuta kipato.
Mara nyinga si mara zote huyu mwenzi wangu hata nimfanyie nini, pesa si nyingi nazompa lakini najitahidi kadiri ya uwezo wangu lakini kwake neno asante baba fulani, au asante kwake ni jambo gumu kwake.
Sasa naanza kukata tamaa kwamba mwenzangu hana shukurani, au mimi ndio napenda sana kushukuriwa.
Je nifanye nini? Au ni tende wema na kwenda zangu? Je kuna wanawake wa aina hii na si kwangu tu.
Waswahili wanasema asante ni kuomba tena, mtu kwangu akiniambia asante nafarijika sana najisikia raha moyoni, naona kile nilichofanya kimeleta impact kwa mtu huyo hata kama asante yake haitoki moyoni mimi sijali.
Karibuni kwa mjadala maoni na michango yenu.