Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,712
Leo nilikuta mjadala huu kwenye usafiri wetu wa hiace,walikua wakijadili rangi ya mwanamke na mwanaume namna inavyoweza kuwa dili kwenye mahusiano,wengi walionekana kuisifia rangi nyeupe na kuonekana kuvutiwa nayo na si hao tu kuna baadhi ya makabila ukiwa na mtoto wa kike mweupe wewe ni tajiri,mfano usukumani yani ukiwa na mabint wawili tu umeula.Mijini nako vipodozi vyenye kemiko ya kuchubua ngozi vinauzwa kama pipi!Rangi nyeupe ina nini?Binafsi katika pitapita yangu sijawahi kuwa na uhusiano na binti mweupe,so sijajua kama mwanamke anapokuwa mweupe anakua na kitu cha ziada,hebu niambieni mliowahi kuwa na hawa watu wana nini mpaka wawe gumzo kiasi hicho!. . . .Wanawake nao ndani ya hiace ile walisema hata mwanaume akiwa mweupe anavutia!!Hii inaonesha weupe hata kwa mwanaume ni dili,wanawake hebu niambieni mwanaume anapokuwa mweupe anakua na nini?Inaonekana ndo maana vijana wa siku hizi wamekua ni wateja wazuri wa karolaiti!Au huu ni utumwa wa fikra?