Wanawake na kuwafokea waume zao

Wanawake na kuwafokea waume zao

Mwagitho

Senior Member
Joined
Oct 11, 2013
Posts
111
Reaction score
38
Hivi huwa mnajisikiaje unapomfokea mume wako kama mtoto mdogo tena mbele za watu? halafu utakuta mwanaume kanywea kama kalowa maji, inasikitisha sana ndoa za sasa hivi hazina tena mwanamke kumuheshimu mume.
 
nampa kibano hajawahi kuona,fedheha na zarau ndio ktu huwa sitaki na ntaifight at any cost
 
sasa wee unataka mke hakuheshimu wakati yeye na wewe mlishindwa heshimu miili yenu wakati wa uchumba kwa kugegedana.

tuwe makini lakini tunapochagua wake
 
Huyo mwanamke hana adabu

Sawa sisi binadamu hatujakamilika na ni vigumu sana kucontrol hasira zako,

Lakini mwanamke mwenye busara ni yule anaejua umuhimu wa kufunga mdomo wake Tena zaidi wakiwa mbele za watu

Utamfokeaje mmeo or mpenzi wako kama mtoto mdogo??

Huko ni kukosa adabu
 
KUNYA ANYE KUKU AKINYA BATA KAHARA!!!!!!!!!!? Mbona nyie mnatufokea? Na wewe mwanaume kwanini ufanye JEURI na KIBURI hadi ufokewe??????????? Mnaboa saa zingine!

Ila mwanaume tafuta PESA sanaaa! Money cant buy you happines but it can spare you the drama and unecesary shame like this. Ukizingatia uko broke unamtegemea mkeo! Haloooooooo! Uapigwa hadi makonzi nini kufokewa!
 
Hata mwanaume kumfokea mke wake mbele za watu siyo busara.Muhimu ni kujaribu kudhitibi hasira mpaka mtakapokuwa wenyewe ili muyamalize.
 
Pole zao hao 'wavulana' wanaofokewa na wake zao...nijuavyo mimi mwanaume huwa hafoki wala kufokewa...

Fall in Love - D'Banj naudediketi wimbo huu kwa mai waifu wangu mai switi poteto mai shuga banana Mrs Nanilihuu...
 
ImageUploadedByJamiiForums1389387712.600840.jpg
 
Labda kalishwaa limbwata ya nyama ya kondooo

Mwanaume wa hovyo hovyo na mzinifu ndiyo huwa anafokewa maana Mke kajua udhaifu wake!

Mme anayetimiza majukumu yake ndani ya ndoa;mme kichwa cha familia na ambaye frequently hukaa chini na Mke wake kupanga issues zao HAWEZI fokewa wala fokea!
 
Mi mwenyewe jana yamenikuta kisa nilimuhuliza kwanin kanisave k.k kwenye simu yake alifoka mpaka nikahamua kutoka ndani na kwenda kwa washikaji kupiga story 2tatu
 
Mi huwa nasema Wanawake wazuri wote walishaolewa yamebaki Manungayembe yanahangaika tu. Mjini hapa yaliyobakia ni makahaba wapenda pesa tuu kwa sasa, na ukioa mmoja wapo haya lazima yakukute. Sio ndoa za sasa majanga, Wanawake wa sasa majanga.
 
Hivi huwa mnajisikiaje unapomfokea mume wako kama mtoto mdogo tena mbele za watu? halafu utakuta mwanaume kanywea kama kalowa maji, inasikitisha sana ndoa za sasa hivi hazina tena mwanamke kumuheshimu mume.

Ukiona mwanaume anafokewa na mkewe mbele za watu na katulia tuli, ujue tayari amepoteza heshima yake na haki yake ya kuwa kichwa ndani ya nyumba! Hakuna kitu kinachonikera kama mwanaume kushindwa kujitambua kwa kujua wajibu wake ndani ya nyumba ya kuwa yeye ndiye mkuu wa familia na anapaswa kuiongoza, kuihudumia na kuitunza familia yake.

Baadhi ya vijana wa sasa wamepoteza sifa hii muhimu, na kujikuta wameacha suala la kuitunza familia na kuilinda kubaki kwa akina mama, na hivyo wamama waliochoshwa ambao pia hawajui waume zao wana nafasi gani ndani ya familia kuamua kuwadharau na kuwaweke waume zao level moja sawa na watoto wao.

Nakerwa na hizo tabia za hao wanaume, nakerwa pia na wanawake wenye hizo tabia za kuwafokea waume zao mbele za watu!
 
Mwanaume wa hovyo hovyo na mzinifu ndiyo huwa anafokewa maana Mke kajua udhaifu wake!

Mme anayetimiza majukumu yake ndani ya ndoa;mme kichwa cha familia na ambaye frequently hukaa chini na Mke wake kupanga issues zao HAWEZI fokewa wala fokea!

Kweli kabisaa
 
Back
Top Bottom