Wanawake na kaburi la mapema....

loh afadhali madhara hayakuwa makubwa...........

kama ulivyosema ni utegemezi wa hisia, ila pia kuna uoga wa kujitegemea, baadhi ya wanawake hata wawe na kazi nzuri, mishahara mizuri bado wanaogopa kujitegemea anahisi hatoweza kumudu gharama za maisha peke yake hivyo huwakuta wakivumilia matusi, kuna wanaume wanabaka hadi ndugu za mke lakini mke hachukui hatua, anaogopa mume akimuacha hataweza leo/tunza familia, ingawa unaweza kukuta huyo mumewe hachangii hata sukari....

Nimewahi kuzungumza na baadhi ya wanawake wanaoishi kwenye ndoa ngumu, wengi sababu wanazozitoa, ni kichekesho......
Kuna mmoja alidai kwamba, aliwahi kuonywa na wazazi pamoja na ndugu zake juu ya huyo mumewe kwamba sio mume mzuri, nadhani waligundua kasoro zake mapema, lakini yeye aling'ang'ania hadi akaolewa, ni kweli hata yeye aliziona hizo kasoro, lakini alijipa moyo kwamba huenda atabadilika (wenyewe husema akikua ataacha) lakini alipoolewa na mume yule hali ilizidi kuwa mbaya. Sasa anajiuliza, Je akienda kuwaeleza wazazi na ndugu zake kwamba ndoa imemshinda watamuonaje, anahisi watamshambulia na kumdhihaki

Mwingine naye alinieleza kwamba, alipompata huyo mumewe, alijikweza sana kwa marafiki zake kwa sababu mumewe alikuwa na hali nzuri sana kifedha, alidekezwa sana na alijiweka mbali na rafiki zake akihofia kuporwa mumewe, lakini baada ya kufunga ndoa, alifurahia ndoa yake kwa miaka mitano tu, baada ya hapo hali ilibadilika. Mume amekuwa malaya, amekuwa mlevi, na kila akirudi nyumbani lazima wagombane na kuishia kupigwa.............kwa ujumla ndoa yake imekuwa ni ya vurugu kila siku.
Na yeye anadai hawezi kudai talaka kwa sababu anaogopa kujidhalilisha, Je ndugu na marafiki zake watamuonaje?

Kwa hiyo kama ulivyosema, wapo wanawake wanakubali kufa huku wakiona kwa kuogopa kwamba jamii iliyo wazunguka itawaonaje pale watakapoachana na waume zao...................!

Kwa kweli zipo sababu nyingi sana na nyingine ni za kijinga kabisa.................
 
kwa sasa sijajua umri wako
naweza sema haya tu
kuishi kwingi kuona mengi

pole kwa mafuriko.....

:focus:

hivi kwani kuishi kwenye hizo ndoa za mashaka ni lazima? kama mapenzi yameisha si basi?
kwa nini uishi kwa hofu? hata ukiachwa utakua wa kwanza?
siku zote mapenzi ni furaha (ingawa misuguano na mitihani ya "kiasi" ruksa kuwepo) lakini penzi linapoisha hisia zikiondoka nini kinakukataza kutafuta ustaarabu wako? wanawake watasingizia watoto...
ndo upigwe, utishiwe kuachwa wengine waletewe nyumba ndogo kisa?
ndoa haya sasa mtambuzi anasema wanajichongea kifo? loh
 
@Mtambuzi:Baba basi basi nimefuta usemi jaman lol!nipe mda nitakuletea mkweo soon nipe miezi kadhaa utapewa chako kwa kunizaa,kunisomesha na kunipa malezi bora!
 
Ngoja nikupe kisa kimoja:
Kuna mfalme alihitaji mtabiri wa kumtabiria maisha yake, akaletwa mtabiri aliyesifika sana kwa tabiri zake zenye kulenga hasa..........Yule mtabiri akamwambia kwa mujibu wa nyota yake, inaonekana kuwa watoto wake wote na wake zake watakufa na kumwacha peke yake............. yule Mfalme akataharuki na kuamuru yule Mtabiri akatwe kichwa.................

Akaletwa Mtabiri wa pili, yeye akatabiri kwa kumwambia kwamba, kutokana na nyota yake, inaonekana atakuwa na umri mrefu kuliko watoto wake na wake zake........... Mfalme akafurahi sana akaagiza yule mtabiri apewe Fedha na Dhahabu nyingi sana kwa utabiri wake uliotukuka......................
Je tofauti ya mtabiri wa kwanza na huyu wa pili iko wapi?

Ukipata jibu, basi utagundua kwamba hata Heading yangu haikuwa na kasoro, bali tafsiri yako ilikuelekeza vibaya.............

Nimegundua kuwa woote walimaanisha ki2 kimoja ila kila moja wao aliielezea kwa namna tofaut! lol nimekupata nw mtambuz!
 
hivi adha yote hii ni ya nini! kwanini watu walioko kwenye mahusiano kila mtu kwa nafasi yake wasiamue kuwa waaminifu (a.k.a Kuacha mipango ya kando) coz to me nafikiri hii ndo challenge kubwa ktk mahusiano mengi. Mzee Mtambuzi umesahau wale wanaokasirika kufikia kiasi cha kujiua au wakati mwingine kuteketeza familia nzima kwa sababu ya haya maradhi yaliko kwenye ndoa.
 
Back
Top Bottom