Wanawake mnijibu

Wanawake mnijibu

ytara jr.

Member
Joined
Feb 6, 2014
Posts
61
Reaction score
22
Kuna binti nilimuomba awe Girlfriend wangu akakataa, alidai hataki mahusiano ya kawaida labda kama ni uchumba.

Nilimjibu siko tayari.

Niliamua kumpotezea, tunaonana mtaani, wakati mwingine tangu hapo ni miaka miwili sasa.

Cha ajabu wakati mwingne hunipigia simu na kuniomba hela, nishamtumiaga mara moja kiasi kidogo, ila juzi tena kaniomba hela, so simuelewi huyu binti ana nia gani?

Msaada mabinti.
 
Kama amekuomba msaada mpe kama anashida msaidie kama mtu mwingine yeyeto
Kama utaki mwambie siwezi kukusaidia,kama basi unampenda ongea naye saa nyingine Ni utoto Tu huwa wanasumbua au maigizo Tu
 
Muulize huyo binti anania gani hapa hakuna ajuaye nia ya bint huyo zaid ni kukisia tu ni vema ukimuuliza yeye.
 
hamuwezi kuwa wachumba bila kuanza wapenzi ni sawa uanze shule darasa la saba moja kwa moja
pili kama anaomba hela kwako kwani wewe ndo baba ake mzazi????na we ulifanya kosa kubwa sana kumtumia japo kidogo maaana ulishamuonjesha asali sasa anataka achonge mzinga.
 
Aaaaaaaa jamani we msaidie tu kiaina au kisa kakuweka kapuni?
Wee mtoe binti uyoo akiwa na shida kama unaona waweza kumsaidia
 
 
Last edited by a moderator:
Kwahiyo umeshindwa kumuuliza mwenyewe, sie ndo tumsemee huyo binti!!!!
Face her....
 
Mpe tu sioni tatizo kumsaidia....... binti kakuweka wa akiba
 
Umekosea sana kuuliza suala lako hili kwa wanawake....
 
mwambie njoo nyumbani uchukue....
akija na wew unamwambia unachotaka then mambo yanaenda sawia kabisaa
 
Back
Top Bottom