Wanawake mbona mnatunyima raha tukitaka kusafisha macho?

Complex

JF-Expert Member
Mar 20, 2013
4,113
4,741
Katika mojawapo ya raha azipatazo mwanamume rijali (walio wengi), mojawapo ni kumuangalia mwanamke mrembo kwa viwango vyake. Kwani hata wanawake mnajiremba ili kupata attention hii kutoka kwetu sisi wanaume.

Ila imekuwa ni kawaida mwanaume akiongozana ama akiwa mahali na mpenzi wake wa jinsia ya kike na ikatokea mwanaume akataka kusafisha macho kwa kumuangalia mrembo anayepita ama aliyevutiwa naye katika eneo hilo, huzuliwa nongwa kubwa sana toka kwa mkewe.

Wanawake wengi huwa mnachukulia kama mmedharauliwa ama mmedhihakiwa. La hasha, hili la kusafisha macho wanaume huwa tunafanya katika kujiburudisha na kutimiza majukumu tuu (refer kuwa mnajiremba ili mpate kuangaliwa kwa attention, na waangaliaji wenyewe ni sisi wanaume).

Hamuwezi kuturekebisha katika hili la kuwaangalia wanawake warembo ( Nazungumzia kuangalia, na siyo kutongoza ama vinginevyo) kwani inatupa starehe isiyo kifani na pia ni asili/nature ipo hivyo.

Katika mifano miwili mikubwa ni hii iliyowakumba waliopata kuwa most influential humans katika dunia yetu ya sasa. Nao ni Obama na Clinton, Katika nyakati tofauti wamepatwa kumbwa na rungu la wake zao wakiwa katika harakati za kuosha macho ama kuzoza(kama anavyopenda kusema JK) na waliovutiwa nao.

Obama, katika mazishi ya Nelson Mandela nchini Afrika ya Kusini, kamera ziliwanasa David Cameron, Barack Obama na Waziri Mkuu wa Denmark kipindi hicho Bi Helle Thorning-Schmidt wakichukua selfie. Jambo hili lilimkwaza sana mke wa Obama na kumtoa katika mood kabisa, sura yake ilikuwa inaonesha kabisa amechukizwa na kitendo kile.

1A298BCA00000578-0-image-a-9_1420993239941.jpg


Katikati ya sherehe ile, kuna muda Obama alinyanyuka akatoka. Guess what, Michelle akaenda kukaa katika siti ya mumewe na kufanya chattings baina ya mumewe na Waziri Mkuu yule Denmark ikomee hapo wakati mumewe aliporejea. Hii kama ni katika mpira wa miguu tungeweza sema Michele aliweka upaja kwa mumewe.

131211131234-obama-mandela-memorial-swap-horizontal-large-gallery.jpg


Bill Clinton.

Mwanaume mwenzetu huyu juzi katika uapisho wa Donald Trump yeye alikuwa anasafisha macho kama tunavyofanyaga wanaume asilimia kubwa. Ila yeye alionekana kuvutiwa na si mwengine, but Melania Trump, mke wa rais wa 45 wa Marekani.

Hamad kugeuka, akakutana na macho ya mkewe Bi Hillary yakimuangalia. nimsifu tuu alijikaza kiume na kuonesha msimamo kwani aliendelea na shughuli aliyokuwa anaifanya ya kusafisha macho licha ya kuona akiangaliwa na mkewe.

promo309219783.jpg




Kwa niaba ya wanaume marijali (tulio wengi) natoa rai katika hili la kusafisha macho, wanawake muwe mnatuvumilia tuu, na muendelee kutuvumilia, kwani hili hufanya nafsi zetu zisuuzike sana.
 

Attachments

  • Hillary BUSTS Bill Clinton STARING At Melania TRUMP! (2017 Inauguration) - YouTube.MP4
    3.8 MB · Views: 49
Vizuriiiii bora umewaambia mkuu

Hawajui tuu kuwa tupo tofauti sana na wao, kwani kuna kuna simulizi zinajaribu kubainisha hili kwa kusema "women are from venus men are from mars" yote hii katika kujaribu kuelezea kuwa tupo tofauti
 
Nimepata picha unaona mbele yako anapita Emmyta kwa maringo utaachaje kuangalia msambwanda....

Ila mkuu kama umeongozana na mke inabidi uuangalie msambwanda kwa makini. Unaweza shtukia kelbu ya uso kama mkeo si mstaarabu. Kwa wale wake ambao ni wastaarabu, hapohapo hutoona reaction yake. Ila subiri ufike nyumbani, Unaweza lala njaa siku hiyo. Heheheeheee
 
Hawajui tuu kuwa tupo tofauti sana na wao, kwani kuna kuna simulizi zinajaribu kubainisha hili kwa kusema "women are from venus men are from mars" yote hii katika kujaribu kuelezea kuwa tupo tofauti
yeah tupo tofaut sana na hawa watu japo nao ni dynamic sana
 
Katika mojawapo ya raha azipatazo mwanamume rijali (Walio wengi), mojawapo ni kumuangalia mwanamke mrembo kwa viwango vyake. Kwani hata wanawake mnajiremba ili kupata attention hii kutoka kwetu sisi wanaume.

Ila imekuwa ni kawaida mwanaume akiongozana ama akiwa mahali na mpenzi wake wa jinsia ya kike na ikatokea mwanaume akataka kusafisha macho kwa kumuangalia mrembo anayepita ama aliyevutiwa naye katika eneo hilo, huzuliwa nongwa kubwa sana toka kwa mkewe.

Wanawake wengi huwa mnachukulia kama mmedharauliwa ama mmedhihakiwa. La hasha, hili la kusafisha macho wanaume huwa tunafanya katika kujiburudisha na kutimiza majukumu tuu ( Refer kuwa mnajiremba ili mpate kuangaliwa kwa attention, Na waangaliaji wenyewe ni sisi wanaume).

Hamuwezi kuturekebisha katika hili la kuwaangalia wanawake warembo ( Nazungumzia kuangalia, na siyo kutongoza ama vinginevyo) kwani inatupa starehe isiyo kifani na pia ni asili/Nature ipo hivyo.

Katika Mifano miwili mikubwa ni hii iliyowakumba waliopata kuwa most influential humans katika dunia yetu ya sasa. Nao ni Obama na Clinton, Katika nyakati tofauti wamepatwa kumbwa na rungu la wake zao wakiwa katika harakati za kuosha macho ama Kuzoza(kama anavyopenda kusema JK) na waliovutiwa nao.

Obama, Katika mazishi ya Nelson Mandela nchini afrika ya kusini, kamera ziliwanasa David Cameron, Barack Obama na waziri mkuu wa Denmark kipindi hicho Bi Helle Thorning-Schmidt Wakichukua selfie. Jambo hili lilimkwaza sana Mke wa Obama na kumtoa katika mood kabisa, Sura yake ilikuwa inaonesha kabisa amechukizwa na kitendo kile.

View attachment 463052

Katikati ya sherehe ile, Kuna muda obama alinyanyuka akatoka. Guess what, Michelle akaenda kukaa katika siti ya Mmewe na kufanya chattings baina ya Mmewe na Waziri mkuu yule Denmark ikomee hapo wakati mmewe aliporejea. Hii kama ni katika mpira wa miguu tungeweza sema Michele aliweka upaja kwa mmewe.

View attachment 463053

Bill Clinton.

Mwanaume mwenzetu huyu juzi katika uapisho wa Donald Trump yeye alikuwa anasafisha macho kama tunavyofanyaga wanaume asilimia kubwa. Ila yeye alionekana kuvutiwa na si mwengine, but Melania Trump, Mke wa raisi wa 45 wa marekani.

Hamad kugeuka, akakutana na macho ya mkewe Bi Hillary yakimuangalia. Nimsifu tuu alijikaza kiume na kuonesha msimamo kwani aliendelea na shughuli aliyokuwa anaifanya ya kusafisha macho licha ya kuona akiangaliwa na mkewe.

View attachment 463055



Kwa niaba ya wanaume marijali (tulio wengi) natoa rai katika hili la kusafisha macho, Wanawake muwe mnatuvumilia tuu, na muendelee kutuvumilia, kwani hili hufanya nafsi zetu zisuuzike sanaaaaaa.

Ni kutokujiamini tu, Na wivu ukipitiliza na ukiwa hauko nae unauhakika hawaangalii mpe mtu uhuru km anakuheshimu na kukupenda kwa dhati JIAMINI.
 
Ila mkuu kama umeongozana na mke inabidi uuangalie msambwanda kwa makini. Unaweza shtukia kelbu ya uso kama mkeo si mstaarabu. Kwa wale wake ambao ni wastaarabu, hapohapo hutoona reaction yake. Ila subiri ufike nyumbani, Unaweza lala njaa siku hiyo. Heheheeheee
 
hawa viumbe wameubwa katika hali ya tofauti tofauti na huwezi choka kuwaangalia hata wakipita mia sema mm huwa naangalia hadi watu wananishtukia, Ila kwa kweli wameumbwa na wanajua kuvaa.
 
Kuna tofauti kubwa kati ya kuona na kutazama, kuona ni nature ya binadamu tu kwamba macho yanafanya kazi lazima yaone. Kutazama ni choice hivo co lazima utazame kila kitu unachokiona. Kuwatazama wanawake wazuri ni utumwa wa ngono tubadilike tuwe tunawaona tu ila,tusiwatazame
 
Back
Top Bottom