Wanawake hii kutaka Uhuru au ni Uchoyo tu ?

Wanawake hii kutaka Uhuru au ni Uchoyo tu ?

Macbook pro

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2020
Posts
752
Reaction score
1,105
Habari zenu wadau.!

Niende kwenye maada moja kwa Moja. Kuna simulizi kaza wa kaza zimekua zikiletwa hapa Jamvini wanaume wakilalamikia wake zao kutokufurahishwa na uwepo wa Ndugu wa Mwanaume pale nyumbani.

Mwanzo atakua kama amefurahi baadae visa na mikasa inaanzishwa na Visirani visivyokuwa na kichwa wala miguu. Siku moja nilikaa na mdada mmoja pale kazini. Aliomgea mengi lakini dhana yake kubwa ilijikita kwenye Uhuru wa Kuishi na Mumewe Nyumbani kwamba uwepo wa ndugu unamfanya ashindwe kufurahia penzi la mumewe

Kwani wakiwepo ndugu hawezi kudeka na hata ile kutenbea na kanga moja kumtega mumewe. Na hii dhana inasambaa sana hasa kwa mabinti wa kileo, Hawapendi kuona ndugu wa mume kuishi nao pale Nyumbani..mwanaume ukilazimisha anakubali kishingo upande na baadae kuanza kuleta maneno na visa chonganishi ili mradi tu hawa ndugu waondoke.

Ni Uhuru tu kweli au ni kauchoyo kamejificha ??
 
Mbona hukumuuliza kama ndugu wa upande wake huwa hawamnyimi huo uhuru wa kutembea na kanga moja kumtega mumewe ili tujue hili anaendana nalo kivipi?
Unakuta nyumba ina ndugu wa mwanamke wa jinsia ME lakini husikii malalamiko kama hayo, hawa watu wana asili ya uchoyo hayo mengine ni maelezo ya ziada tu.
 
Kwa uzoefu wangu wanawake ni wabinafisi sana hasa linapokuja swala la ndg wa mme wake.

Utafiti kidogo tu ujio wa ugeni

Haijarishi hao ndg wamekuja na kuondoka mapokezi ya ndg zake na ndg wa mme wake ni vitu viwili tofauti.

Amini usiamini wanarudi kwao hao ndg zake kama una uwezo kama sukari huwa una nunua mfuko mzima watabebeshwa hadi na nguo zako usizozivaa mara kwa mara! Bado watapewa na hela wewe ndg zako wataambiwa mtafika salama karibu tena!!

Narudi kwenye mada yako huyo mwanamke uliye kaa nae kazini na akaanza kukueleza kuwa hapati uhuru nk ni hivi huyo ana roho mbaya.

Unataka kuniambia akiwa na watoto wake atavaa kanga moja kumtega mme wake? Atajibebisha mbele ya watoto?

Desturi zetu haziko hivyo la sivyo muishi wawili tu kama njiwa ndo mtafanya hayo yote.

Mbona sisi wanaume hatulalamiki kuishi na shemeji zetu (kaka /wadogo zao )?

Wanawake sampli hiyo wana roho mbaya tu kati ya familia kumi sita hadi saba zinaishi na ndg wa mke
Familia 4 kati ya 10 ndo zinaishi na ndg wa mwanaume.

Familia 2-3 kati ya 10 zinaishi na ndg wa pande zote yaani wa mme na mwanamke.

Hii nimeipata kwenye sensa ya ukoo wetu huwa tuna kawaida ya kuorodhesha watu wanaoishi kwa kila familia ya mwana ukoo kuna kuwa na category kama

Mfanyakazi (hana upande)
Mtoto
Ndg wa upande ME/KE

Sensa hii hutuwezesha kujua wanaukoo waliosoma hadi level fulani ya Elimu ni wangapi je wanaongezeka?
 
Back
Top Bottom