kadovela
JF-Expert Member
- Jan 31, 2016
- 471
- 679
Unakuta mwanamke ni mama tu wa nyumbani kaolewa na mumewe na anapendwa sana asubuhi kama ilivyo wajibu anaamka mapema anamuandalia maji ya moto ya kuoga mumewe.
Mumewe anaamshwa anakwenda bafuni kuoga anatoka kuoga anakuta nguo imenyooshwa anavaa anakaribishwa kifungua kinywa na mkewe anapata chai kabla ya kuanza safari ya kwenda kazini anamfuata mkewe kwa tabasamu anamkumbatia na kumbusu kwa huba na kumtakia mkewe abaki salama.
kumbuka haya yote yanafanyika wakati huyu mke alikurupuka asubuhi bila kupiga mswaki,kuoga wala kunawa uso ili amuweke sawa mumewe aende kazini, uwa najiuliza baada ya hapo huyu mwanamke kushinda kujipodoa na kujikoboa full ma make up, na urembo wa gharama kubwa yote anafanya kwa ajili ya nani?
Hivi kufanya usafi wa mwili na kujiweka sawa bila maurembo ya gharama haiwezekani? hayo yote kwa ajili ya nani wakati mumeo hata katika muonekano wa kuamka asubuhi bado anakupenda na kuthamini uwepo wako kwake, nauliza hayo yote kwa ajili ya nani?
Mumewe anaamshwa anakwenda bafuni kuoga anatoka kuoga anakuta nguo imenyooshwa anavaa anakaribishwa kifungua kinywa na mkewe anapata chai kabla ya kuanza safari ya kwenda kazini anamfuata mkewe kwa tabasamu anamkumbatia na kumbusu kwa huba na kumtakia mkewe abaki salama.
kumbuka haya yote yanafanyika wakati huyu mke alikurupuka asubuhi bila kupiga mswaki,kuoga wala kunawa uso ili amuweke sawa mumewe aende kazini, uwa najiuliza baada ya hapo huyu mwanamke kushinda kujipodoa na kujikoboa full ma make up, na urembo wa gharama kubwa yote anafanya kwa ajili ya nani?
Hivi kufanya usafi wa mwili na kujiweka sawa bila maurembo ya gharama haiwezekani? hayo yote kwa ajili ya nani wakati mumeo hata katika muonekano wa kuamka asubuhi bado anakupenda na kuthamini uwepo wako kwake, nauliza hayo yote kwa ajili ya nani?