Habari za leo,
Latest news, Mwanaume rijali Rombo ni dili.
Wanaume Wilaya ya Rombo wameathirika na ulevi wa pombe za kienyeji kama vile gongo, vimorali, raha leo, vimondo, vimbuli na vipombe vingine vyenye majina ya ajabu. Matokeo yake wanaume wamepoteza ule uwezo wa kuhudumia ndoa zao na hatimaye wamekuwa wakiwakimbia wake zao.
Tatizo hili ni kubwa sana kiasi kwamba hata mwanamke akienda kwa jirani kuomba msaada kwenye tuta anakuta nafuu ya mume wake. Si akina mama, si mabinti, wote wamebaki wapweke yani no huduma ya za wanaume.
Kwa hali hiyo wanawake wa Rombo wamwonapo mwanaume aliyetoka mjini ie DSM, Arusha, DDM, Moro n.k. wanamvizia kama mwanaume amviziavyo mtoto wa kike...
Na wanaume sasa, akikuona umeenda kusabahi Rombo hawana shida ya bia wala mbege! Siku hizi wanakuomba jero tu na ukimpa baada ya nusu saa anarudi yupo safi, amependeza yani kalewa!
Hali ya Rombo ni tete kigenaration kwani shule nyingi za msingi kwa darasa la kwanza zimebaki na madawati tupu. Kama pombe hizi hazitotokomezwa, basi kuna hatari miaka 3 hadi 5 ijayo shule hizi zikakosa wanafunzi kabisa.
Kujua hali ilivyo mbaya, angalia ITV, Jumanne saa tatu na nusu usiku kipindi cha Ripoti Maalum toka Romba, ni mwendelezo wa jinsi wanaume wa Rombo walivyoathirika na ulevi wa pombe za kienyeji.
Mpo wababa? Kuna haja ya kupigana kuokoa Rombo yetu.