Wanaume ni dhaifu kuliko wanawake! Nani anabisha?

Mie sijasema yeyote ni dhaifu, mie naona watu wana-excersize haki zao za kudinyana tu.

Kama mtu anacheat ama nyumba ndogo ni sambi sake mwenyewe.

Soma hiyo post yangu ya juu hapo...kwa mantiki hiyo "wanawake ndio dhaifu, maana tungelikuwa dhaifu basi mngelisema kwa udhaifu wetu twalibakwa"
 
Mie sijasema yeyote ni dhaifu, mie naona watu wana-excersize haki zao za kudinyana tu.

Kama mtu anacheat ama nyumba ndogo ni sambi sake mwenyewe.

Oooh nadhani wewe na mimi iko dugu moya na iko na aina moya ya mawazo na hili ndilo najaribu kumuelewesha huyu bi mkubwa hapa...
 
naomba nikujibu hoja zako kama ifuatavyo,moja umeongozwa na hisia sana,alafu pia umefanya generalization ya sampling ya wanaume wacahche wenye tabia hizo kwamba wote ndio tupo hivyo nikianzia katika hoja ya kwanza,mwanaume kuwa na nyumba ndogo binafsi sikubaliani na hilo swala lakini pia inaweza pakawa na sababu zilizomfanya huyo kuwa na nyumba ndogo rejea post ya Zeddicusaliyekaa mwaka mmoja bila ya kupewa uyumba na mkewe,
katika hoja yakoya pili ya wanaume kutumia mabavu sio wote wako hivyo ukija na hoja nzuri yenye mantiki lazima mumeoa au mwanaume wako aikubali akiikataa basi atakauwa sio mwerevu,ila pia kuna makabila mengine yanataka mwanaume awe juuu na ni haramu kwa manamke kutoa ushauuri napingana nayo,
mwisho hiyo ya uwezo wa kuvumilia matatizo hapa na mfano wako ulioutoa wa kumlea mtoto wanawake wangapi umesikia wanatupa watoto chooni au jalalani au hhujasikia habari hizo,lakini pia mko influenced sana na kuishi namtoto kwa shida na raha kutokana na uchingu mnaoupata wakati wa kujifungua na kubeba ujauzito na hiyo ni gender ole ipo hivyo kutoka kwa muumba,nimalizie usifikiri kutongoza jamba rahisi kumdanganya mkubwa mwenzio mpk akupe papuchi si jambo la kitoto,`wengine hutumia msemo wa kusema ni sawa na kuteka kambi ya jeshi`,refer kwa wanoenda kununua malaya hawana midomo ya kutongozea??
 
Last edited by a moderator:
Mbona wakiachiwa usukani wanaweseseka,na kuhaha namna ya kusimamia miradi na maendeleo ya familia.Chezea mwanaume weye.
 
Hapo nadhani unamaanisha:

"UJUNGA NI BARAKA"

Au?

Hata cheche ndogo tu sehemu penye giza totoro huonekana kuwaka sana.

Rais wa wabeba box kasema watu wengine wanadanganyika na Kiingereza kama cha Kiranga, cha kujifunzia ukubwani.

Nilitaka kusema tu, si kwa sababu Kiranga ni kipanga sana wa ungwini, labda kwa sababu wanaomshangaa wako totoro kuliko msitu wa Tororo.

Aidha

Kiingereza ni lugha isiyo mfumo wa sheria wala matamshi unaoeleweka kwa ujamali. Kwa hiyo sijawahi kuelewa kwa nini kujua Kiingereza kuwe ni sifa ya ustadi, zaidi ya sifa ya kuweza kuongea na wengi.
 
kirk.jpg


Ninaamini hivyo kwa sababu kuna mambo kadhaa ambayo yamenipa ushahidi kwamba, mwanaume hata akijidai kwamba ana ubavu wa kiwango gani, lakini bado kiufahamu ni mtumwa wa mwanamke. Kuna mambo makuu kama matatu ambayo yananifanya nifikiri hivyo.

Kwanza kwa mada yako hii umeonesha namna usivyofikiria sawasawa!

Kwanza ni ile hali ya mwanaume kuweza kutawaliwa na mwanamke wa nje (aka nyumba ndogo) na kukubali kuacha familia yake na hata kuvunja heshima yake. Kuna wakati najiuliza kama kweli mwanaume mbele ya mwanamke huwa anaweza kutumia akili yoyote. Unakuta mwanaume anakutana na mwanamke barabarani na kumtongoza na akikubaliwa anamgeuza huyo mwanamke kuwa nyumba ndogo yake, lakini usidhani kwamba nyumbani kwa huyo mwanaume kuna matatizo ya ndoa. Hapana, hakuna tatizo lolote ila mwanaume huyo kaendeshwa na tamaa yake ya mwili na akashindwa kuidhibiti. Matokeo yake anajikuta analowea huko kwa nyumba ndogo yake, hadi anaharibikiwa. Hajali watoto, hajali mkewe, hajali heshima yake wala chochote.

Kwanza kitendo cha kulinganisha ni ishara ya udhaifu mkubwa ulionao

Hivi wewe unaunganishaje watu wote na ujinga wa mtu au kikundi kimoja cha watu?

Unakuta mwanaume anazuzuliwa na shanga tu, au kitu kingine kidogo sana, labda weupe wa mkorogo au lipstiki na makalio makubwa. Kwa ujumla utaona kabisa kwamba, ufahamu wa mwanaume ni kama ziro kabisa. Halafu kumbuka kwamba, wakati huo hiyo nyumba ndogo inajuwa kabisa kwamba, inalisanifu hilo janamume b.w.e.g.e, au tuite buzi lakini limo tu, kama GEGEREKA.

Kama mwanaume angekuwa na ufahamu kuliko mwanamke, angeweza vipi kushikwa na nyumba ndogo kwa kiwango cha kukatisha tamaa kwa kiasi hicho? Ni wazi mwanamke ndiye ambaye ana uwezo mkubwa zaidi wa kufikiri na kupanga. Kama mwanaume angekuwa na ufahamu wa kutosha, si angeweza basi kung'amua kwamba, anasanifiwa na nyumba ndogo, kwani hapo hakuna kupendwa bali kuchunwa.

Kwanza wewe inaonekana ni kimada au nyumba ndogo

Au mumeo ameshikwa na nyumba ndogo

Yaani wewe unataka kuwajumlisha watu wote kwenye ujinga wa mtu mmoja tu?

Unawajua ni wanaume wangapi wana nyumba ndogo?

Unajua kuwa shanga zinavaliwa na watu gani?

Unajua kuwa wanawake wangapi wanavaa shanga?

Unajua ni wanaume wangapi wanazijua shanga achillia mbali kuzipenda?

Pili ni ile hali ya mwanaume kupenda kutatua mambo yake kwa mabavu badala ya kufikiri. Ukiangalia sana, kwenye matatizo au vurugu nyingi, wanawake huwa ni watu wa hekima zaidi kuliko ubabe, yaani wanatumia vichwa vyao kuliko miili. Siyo kwamba, wanaogopa kutumia miili yao, hapana. Kuna mazingira ambayo unaona kabisa kama mwanamke angeamua kujikaza hapa, hakika angempiga huyu mwanaume. Lakini sisi wanawake tunapenda kuyamaliza mambo kwa hekima na uelewano.

Hii ni hekima ambayo kwa bahati mbaya kwa wanaume wengi sana haipatikani. Kwa hiyo, unaona kabisa kwamba, mwanaume bado yuko kwenye ile hali au kiwango cha chini cha kujifahamu kwa sababu bado yuko kwenye kuamini mabavu yake.

Tatu, mwanamke ni bora zaidi kuliko mwanaume katika suala la kukabiliana na matatizo na vurugu za kimaisha. Unaweza kuona mwanamke ametelekezwa na mume akiwa na watoto, lakini hata siku moja hachukui uamuzi wa kuwakimbia watoto. Ni wanawake wachache sana kwa idadi ambayo hatuwezi kuizingatia, ambao wanaweza kufanya hivyo.

Lakini kila siku magazetini kuna taarifa za ukatili wa wanaume dhidi ya wanawake au wanaume kutelekeza familia zao. Ukiangalia sana utaona wamekimbia familia zao kwa sababu ya nyumba ndogo au kwa sababu ya ugumu wa maisha. Kwa nini msione kwamba, mwanamke bado ni shujaa zaidi ya mwanaume…?


Yaani wewe sijui niseme umetumia kitu gani kufikiri mpaka ukaleta hii mada yako ya hovyo hapa

Wanawake wanatumia akili?
Zipi?

Za kuwalisha sumu watoto wa kambo?
Vipi kila uchao kwenda kwa waganga kutafuta dawa ili wapendwe?

Je ni wanawake hawa hawa unawazungumzia ambao tumeambiwa kwenye maandiko tuishi nao kwa akili?

Kwa mada hii umeendelea kuthibitisha namna ulivyotumia miguu kufikiri!!!!!!!!!!!!

Hovyo kabisa!!!!
 
Back
Top Bottom