Wanaume na vijitabia vyao

Wanaume na vijitabia vyao

Wanaume wapo wengi Sana wa hivyooo
Mwanaume ni yule akitoka kutafuta hurudi kujiandaa kwa ajili ya kwenda kutafuta kesho tena..sasa hyo anaekuja kukaa na wewe jikoni hyo sio mwanaume bali ni mwenzako!
 
Mmh. Hivi wanaume wa kuhesabu vitoweo bado wapo kweli? Kama wapo nawapa pole aiseee.

Hao wabahili na wenye gubu huwa ni kumuomba tu M'mungu usikumbane nao sababu hawaepukiki na ukibahatika kuwapata wa hivyo ni wewe mwenyewe kujua namna ya kuishi nao tu sababu ni tabia ya mtu hiyo huwezi mbadilisha zaidi ya kuipunguza isizidi kipimo.
 
Ukiolewa na kimeo unakuwa unajitahidi kujifariji kwa kauli za eti wote wako hivi hivi.
 
Dada usione mwanaume kavaa suruali mkanda kachomekea nadhifu ana vichenji vikakuzuzua mchunguze kiundani kabla ya kuolewa nae .

Zijue Tabia zao zisizopendeza na kama zipo unazozijua ongezea hapa.

*wabahili hawa akishakuoa anachojua kukuhudumia chakula tu wengine wanafika mbali wanakuweka kama pambo hatahuduma hakupi

*Gubu.huyu akianza kusema haeshi siku nzima anasemaa tu akitoka ndio unapumzika.

*kuhesabu vitoweo.Mara nyingi huyu anakupangia mboga iwe siku tatu tatu hata wakija wageni utajijua mwenyewe.

*wachoyo.hapendi ndugu zako mwanamke wake au usaidie kwenu
hiyo ya nne ndio yangu,nikileta nyama naikatakata nahesabu finyango naweka kwenye vimfuko,kilo mbili zinaweza kukaa hata mwezi maana nyama nakata kama vijimiskaki viduchuviduchu
 
Back
Top Bottom