Wanaume kuogopa wanawake wenye pesa

Wanaume kuogopa wanawake wenye pesa

umukagame

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2014
Posts
1,044
Reaction score
675
Habari wakuu,

Kwa mazingira ya kawaida na uzoefu wangu huwa naona wanawake wenye uwezo wanaogopwa na wanaume.

Ni kwa nini vijana wanawaogopa au kuwanyanyapaa wanawake wenye pesa/wanaojiweza kimaisha?

Huwa mnaogopa nini wakuu?

Semeni ya moyoni kama hao wanawake wenye mihela wapo huku wajue kabisa
 
Mambo yafuatayo

1. Ana changamoto chache za kimaisha kwa hiyo weak point zinakuwa chache

2.Overconfidence( hili ni tatizo kubwa la wanawake wenye uwezo wa kumudu mahitaji yao)

3. Kuwa wachaguzi sana.
 
Wanaume wanapenda kuwa juu in everthing(inaboost ego yao) na inamfanya ajiamini zaidi na awe na controll.
Anapokuwa na mwanamke alomzidi iwe kiuchumi, kielimu nk huwa kujiamini kunashuka as anahisi hatukuwa na controll anayopaswa kuwa nayo kwa mwanamke.
 
Huo ni mtazamo wako.

Hata kama wapo wanaoogopa lakini sio wote.

Pia hiyo nadharia ni mbaya katika jamii
 
Hatugopi wanawake wenye hela tunaogopa hulka zao ni za kidhalilishaji heshima huwa ndogo sana,atataka yeye ndio awe msemaji mkuu na wa mwisho na mbaya zaid kila mtu atajua kuwa yeye ndio kila kitu pale nyumban.! Ni asilimia kubwa wapo hivyo but wapo wenye hela na bado wanaisha kama wanawake wa kawaida hata mama samia Suluhu ju kasema pamoja ni makamu wa rais kwa mume wake anapiga goti.!
 
Huwa wanajeuri Sana ukitaka mgegedo anakupa pale anapokua anataka yeye
 
Kitu amabcho nimekigundua kwa wanawake wenye pesa, yaani wanakuwa too possessive.
Na ikitokea unajiweza kifedha yaani hutegemei, basi atafanya kila njia kutaka kukurubuni, usipokuwa makini hata kazi unaweza acha, ama ukaacha kufanya shughuli za kukuingizia kipato.

Commenting from experience
 
Ilishanitokea nilikuwa na sister mmoja mwenye pesa zake kwa muda mfupi nilimiliki macheni ya gold na simu kila aina ila duu akikwambia Leo usitoke ukatoka mbona shida nikaamua kuachana na umarioo
 
Back
Top Bottom