Nina mpenzi wangu ambaye nimeridhika naye kwa kuwa ninampenda, na kama mapenzi ya Mola yatatimia ningependa awe mama wa watoto wangu. Ni mwanaume wake wa kwanza.
Ni binti mrembo, anajiheshimu, mpole kidogo, mrefu wa wastani, kwa kifupi ametimiza vigezo muhimu vya mtu anayefaa kuitwa mke wa mwanaume wa kiafrika, ikiwemo age gap ya miaka 4. Kilichonileta hapa jf ni kwamba kwa sasa yuko likizo kwa dada yake aliyeolewa. Mume wa dada yake amekuwa akimtaka kimapenzi huku akimuahidi kumpa pesa nyingi na zawadi kama atakubali kufanya naye mapenzi. Mpenzi wangu amekataa na kutaka kuondoka japo dada alimuomba aendelee kukaa hapo kumsaidia kwa kuwa ana mtoto mdogo.
Huyo bwana kuna siku huingia hadi chumbani kwa huyo binti wakati mkeo akiwa kazini. Jamani mimi huwa nina roho ngumu lakini hapa naumia nahisi kama anaweza kumuingilia kwa nguvu na kwa sasa sina uwezo wa kumuondoa pale. Ila jamani wanaume heshimuni ndoa!!!