Wanataka uajiriwe ili wakuombe hela

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,891
Kwema Wakuu,

Uchunguzi wangu unaonyesha kuwa kumuomba hela mtu aliyeajiriwa ni rahisi tofauti na aliyejiajiri. Yaani hata Kama Aliyeajiriwa analipwa pesa ndogo Mfano laki tatu, wataona ni Kheri kwani wanajua fika ifikapp mwisho wa mwezi utakuwa na laki 3.

Wakati ukijiajiri hawajui mapato yako, sio ajabu wazazi, ndugu, jamaa na marafiki wakawa wanakupigia kelele uajiriwe, ni kwa sababu wanataka uhakika wa kuomba hela kwako.

Waliojiajiri ni rahisi kukimbia misumari na vibomu vya waombaji na wengi husema mambo ni magumu sana, waombaji huelewa.

Hata kutembelewa na ndugu, ni rahisi ndugu kumtembelea ndugu aliyeajiriwa kuliko anayefanya ujasiriamali, hata Kama mjasiriamali anapata pesa nyingi kuliko muajiriwa, Siri ni kuwa Aliyejiajiri mapato yake hayafahamiki.

Sio ajabu ukiajiriwa halafu ukatangaza kuoa mapema unaweza zua balaa kubwaπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€ ndugu kukuzingua, huku wengine wakimpa taabu Mke/mume wakoπŸ˜€πŸ˜€πŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈ

Nawasilisha
 
Ndugu: Ncha Kali ushaajiriwa?

Mimi: Bado, nimetuma maombi nasikilizia.

Ndugu: Sasa mjini unaishije?

Mimi: Kuna mishe fulani, naunga-unga maisha yanaenda.

Ndugu: Pole sana, basi nilikuwa nakusalimia tu.

Mimi:


πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€

Unaweza fikiri wanakuonea huruma kumbe wanaseti upinde wakuchape mshale Kama umeajiriwa.

Wajue umeajiriwa alafu wasikie unataka kuoaπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€ wanaweza wasionyeshe hasira zao Ila amini watakasirika moyoni.

Ukipata Ajira watakuambia subiri ujijenge Kwanza ndio uoe. Hii ni nafasi kwao mgawane Mshahara.

Usipokuwa na Ajira watakuambia Mbona huoi umri unaenda, badala ya kukuambia usioe utamlisha niniπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Hiyo ndio point ya Msingi Boss.

Wewe unafikiri wanakushauri uajiriwe ili ufanikiwe na uanzishe familia yako?

Ndio maana ukiajiriwa alafu ukaoa mapema wakati mwingine unaweza zua migogoro baina yako na Familia au ndugu zako
Wengine mpaka husema mke anafaidi wakati tumemsomesha sie, sasa sijui hawataki aoe awe anadanga!
 
Kwema Wakuu,

Uchunguzi wangu unaonyesha kuwa kumuomba hela mtu aliyeajiriwa ni rahisi tofauti na aliyejiajiri. Yaani hata Kama Aliyeajiriwa analipwa pesa ndogo Mfano laki tatu, wataona ni Kheri kwani wanajua fika ifikapp mwisho wa mwezi utakuwa na laki 3.

Wakati ukijiajiri hawajui mapato yako, sio ajabu wazazi, ndugu, jamaa na marafiki wakawa wanakupigia kelele uajiriwe, ni kwa sababu wanataka uhakika wa kuomba hela kwako.

Waliojiajiri ni rahisi kukimbia misumari na vibomu vya waombaji na wengi husema mambo ni magumu sana, waombaji huelewa.

Hata kutembelewa na ndugu, ni rahisi ndugu kumtembelea ndugu aliyeajiriwa kuliko anayefanya ujasiriamali, hata Kama mjasiriamali anapata pesa nyingi kuliko muajiriwa, Siri ni kuwa Aliyejiajiri mapato yake hayafahamiki.

Sio ajabu ukiajiriwa alafu ukatangaza kuoa mapema unaweza zua balsa kubwaπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€ ndugu kukuzingua, huku wengine wakimpa taabu Mke/mume wakoπŸ˜€πŸ˜€πŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈ

Nawasilisha
Pesa haijifichi ndugu yangu.
 
Noma haswaa, na kijana akianza labda kapata kijiwanja huko alipo utasikia anza nyumbani, mkeo kakukalia, wanawake hubeba lawama hata zisizo wahusu.


πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€

Binadamu Wabinafsi Sana.

Wakati kila mtu anamajukumu yake.

Jukumu la mume ni kumtunza mke wake na Watoto.
Wakikua asiwasumbue Bali anatakiwa awe alishawaandalia Urithi lakini kikwetu kwetu(Afrika)
Mtoto bado anapewa kazi ya Kulea wazazi Jambo ambalo sio jukumu lake, na hapa ndipo ugomvi unapotokea
 
Unanisema kbs nahusika na hii maada kwa asilimia zote...nilivokuwa mtaani waliniambie nioe kwani Kuna madhara ya kuchelewa kuoa na kupata mtoto.chupuchupu ilibaki kidogo nioe sema mwali alizingua baada ya mwaka nimepata kazi Sasa hivi Wanasema jitahidi ujenge kanyumba chako ndipo uoe sijui ujipange usomeshe Mtoto shule nzuri blah blah kibao.....Mimi Kama Mimi kwa misimamo yangu naona Bora nioe TU MAANA napoteza pesa nyingi Sana kwenye kula mahotelini
 
Back
Top Bottom