Wanasheria msaidieni Mwalimu huyu

mwambunnyara

JF-Expert Member
Sep 25, 2013
518
206
Ni mke wa kaka yangu amekuwa akifundisha shule ya sekondari Mgulasi,iliyopo manispaa ya Morogoro.

Shemeji yangu huyu pamoja na kuwa wako 2 tu wanaofundisha fizikia shuleni kwao,lakini Mkuu wake wa shule amemfanyia zengwe za ajabu kwa sababu tu alihoji mapato na matumizi ya shule kwenye kikao.

Matokeo yake,shemeji yangu huyu aliuguliwa na mtoto,usiku(ilikuwa ghafla) akalazimika kumpeleka mtoto hospital, asubuhi akaandika barua ya kuomba ruhusa akiwa hospital,akampatia madam mwenzake ampelekee kwa Mkuu wake wa shule.

Mkuu wake alipokea barua na kuificha bila kuweka kwenye file,na akaanza kumuandikia "NO ANY INFORMATION" kwenye daftari ya mahudhurio,zilipotimia siku tano,akapeleka taarifa kwa afisa elimu,ilipofika tarehe 01/03/2016 akaletewa barua tatu na Mkuu wa shule,barua hizo zilikuwa...

1.TUHUMA ZA UTORO KAZINI
2.BARUA YA KUJIELEZA KWANINI ASICHUKULIWE HATUA
3.BARUA YA KULIMWA MSHAHARA WAKE,(NUSU MISHAHARA)

Barua zote tatu,zimeandikwa siku moja,01/03/2016.Baada ya kupokea barua hizo alienda kwa afisa elimu wake kutafuta ufafanuzi wa jambo hilo akamtimua,alipoenda kwa mkurugenzi kutafuta haki yake hakupata fursa hiyo,aliambiwa mkurugenzi yupo busy sana.

(kwa zaidi ya mwezi wiki mbili hakupata msaada wowote) Hatimaye mwisho wa mwezi wa tatu mshahara wake ukafyekwa,akakuta kuna nusu mshahara,akaamua KUACHA KAZI.

MPAKA SASA MGULASI SEKONDARI ILIYOPO MOROGORO MANISPAA YENYE WANAFUNZI 1034 INA MWALIMU MMOJA TU WA FIZIKIA,ETI KISA MWALIMU KUHOJI MAPATO NA MATUMIZI YA SHULE, KWA MWENDO HUU TUTAFIKA?

Kwa hiyo situation hapo wakuu,mnamsaidiaje shemeji yangu huyu kisheria imekaaje!?
 
Aliamua kuacha kwenda kazini kwa sababu ya hasira,ila kazi bado anataka,afuate hatua gani kudhibiti uharamia huu aliofanyiwa na kwenda kuhakikisha anaendelea na kazi yake!!!!
 
Mwambie aache hasira aendelee na kazi (Kama hajaandika barua rasmi ya kuacha kazi) wakati akiendelea kufuatilia hiyo issue yake. Mshahara wake utarudishwa mambo yakiwa poa but issue ya msingi ni kutafuta mwanasheria au aende akaripoti kwa chama cha walimu (CWT) maana kumlipa mwanasheria kwa mshahara wa ualimu itakuwa ni issue nyingine. Hope CWT wataweza kumsaidia.
 
Hilo jipu ni baya mno hapa morogoro mjini, yanayotukuta huko maofisini siri yetu, hawa wakuu wa shule wana figisu nyingi sana na hata yuke afisa elimu sidhani kama ana maadili ya kazi, pole sana ndugu. nami nipo njiani kuachia ngazi wafundishe wao, tumechoka kuburuzwa.
 
Umeandika uwongo mtupu..mkuu wa shule sio mpuuzi kiasi hicho..nyie walimu wavaa milegezo mnashida..hakika huyo mkuu hapendi upuuzi...
Hongera kwa mawazo yako mufilisi,nyie ndo mnaokurupuka tu kujibu kitu pasipo kutumia hata chembe ya ubongo,hamna tofauti na NGURUWE
 
Hilo jipu ni baya mno hapa morogoro mjini, yanayotukuta huko maofisini siri yetu, hawa wakuu wa shule wana figisu nyingi sana na hata yuke afisa elimu sidhani kama ana maadili ya kazi, pole sana ndugu. nami nipo njiani kuachia ngazi wafundishe wao, tumechoka kuburuzwa.
Imeniuma sana kwa hii issue ya shemeji yangu,coz kiukweli ni mtu anayejituma sana,kosa lake kubwa eti ni kuhoji namna pesa zinavyotumika shule,jitu limejenga roho ya hasira,mpaka kero.
Walimu walio wengi wamejaa unafiki na uzandiki,hawajielewi hata kidogo,eti kauli mbiu ni JIFANYE MJINGA SIKU IPITE,hopeless!!!
 
Mwambie aache hasira aendelee na kazi (Kama hajaandika barua rasmi ya kuacha kazi) wakati akiendelea kufuatilia hiyo issue yake. Mshahara wake utarudishwa mambo yakiwa poa but issue ya msingi ni kutafuta mwanasheria au aende akaripoti kwa chama cha walimu (CWT) maana kumlipa mwanasheria kwa mshahara wa ualimu itakuwa ni issue nyingine. Hope CWT wataweza kumsaidia.
Ahsante Mkuu,ushauri wa Kujenga kabisa
 
Asijitoe kirahisi sana CWT itambeba tu na huyo mkuu ataaga mashindano na afsa elimu pia.na Je anayo nakala?? Akiona anaogopa aende idara ya usalama Taifa hapo wilayani aeleze huko issue yake itafuatiliwa na haki ataipata.
 
Asijitoe kirahisi sana CWT itambeba tu na huyo mkuu ataaga mashindano na afsa elimu pia.na Je anayo nakala?? Akiona anaogopa aende idara ya usalama Taifa hapo wilayani aeleze huko issue yake itafuatiliwa na haki ataipata.
Ahsante sana Mkuu nitajitahidi sana kumpa ushauri huu,kwani nimekuwa namtia moyo kuwa asikate tamaa kirahisi hivyo!!
 
Nakala za nyaraka zake zote anazo,kuanzia barua yake ya ruhusa,nyaraka za matibabu ya mtoto wake na barua zake za adhabu!!!
 
sheria hapo mbona rahisi siku aliyompeleka mtoto kama ana stakabazi za daktari na barua copy aliyo andika au kuwa na moja na shaidi aende kwenye maadili ya watumishi kulalamika
 
mwambie aje tubadilishane mie nije moro yeye aje tukuyu huku hatuna mambo hayo ya kubaniana
 
Back
Top Bottom