Nyakati tulizo nazo sasa ni za kilimo cha kisasa. Kilimo cha technology. Nyakati hizi ni za kutumia viuatilifu na teknolojia zingine.
Hebu jiulize, ni vijana wangapi wanaweza gharama hii? Yaani 500,000/= kwa mafunzo ya siku 3 ya viuatilifu? Na hapo ujitegemee chakula na malazi! Mafunzo haya yanafanywa na taasisi ya Serikali. Hawa wanalipwa mishahara na kodi zetu.
Hivi wameshindwa namna ya kuwafikia waTanzania kwa gharama nafuu? Mbona kuna semina na training kubwa zinafanyika, tena mpaka walengwa wanalipwa posho. Kwa hili Bashe kakwama wapi? Serikali inashindwa wapi?
Ukiangalia gharama ya mafunzo ni mtaji tosha. Kwa anayeweza kulima mahindi ekari moja, ni gharama tosha mpaka kuvuna. Kwa anaelima nyanya, gharama hiyo ni sawa na robo eka. Kweli tutafika?
Hivi Serikali imeshindwa kuyawekea ruzuku mafunzo haya ili Watanzania wafaidike wengi?
Hebu jiulize, ni vijana wangapi wanaweza gharama hii? Yaani 500,000/= kwa mafunzo ya siku 3 ya viuatilifu? Na hapo ujitegemee chakula na malazi! Mafunzo haya yanafanywa na taasisi ya Serikali. Hawa wanalipwa mishahara na kodi zetu.
Hivi wameshindwa namna ya kuwafikia waTanzania kwa gharama nafuu? Mbona kuna semina na training kubwa zinafanyika, tena mpaka walengwa wanalipwa posho. Kwa hili Bashe kakwama wapi? Serikali inashindwa wapi?
Ukiangalia gharama ya mafunzo ni mtaji tosha. Kwa anayeweza kulima mahindi ekari moja, ni gharama tosha mpaka kuvuna. Kwa anaelima nyanya, gharama hiyo ni sawa na robo eka. Kweli tutafika?
Hivi Serikali imeshindwa kuyawekea ruzuku mafunzo haya ili Watanzania wafaidike wengi?