Wanasema maneno huumba

Habari yako Samiya.
 
Mimi niliamin hii baada ya kujaribu kujiua ingawaje nilipona

Ila hapo kabla nilipenda sana kusema na kuwazia jambo la kukatisha uhai,kweli bhana siku moja nikafanya hicho kitendo mpaka leo huwa sielew niliponaje wakat nilikunywa sumu ambayo iliwah uwa watu wengine
 
Ujachelewa mzee, mafanikio hayana umri. DHAMIRA + VITENDO.
 
Bora umebaini hilo. Ni kweli, maneno ni VITU!

Hata Mary Todd alipokuwa angalia binti, alimwambia baba yake kuwa ni lazima siku moja aje kuwa mke wa Rais wa Marekani. Na kweli, baadaye alipompata mchumba aliyekuwa mwanasiasa, baba yake alipata matumaini kuwa huenda ndoto za bintiye kuwa first lady wa USA zitakuja kutimia. Lakini huo uchumba haukudumu. Ulipovunjika, mzee alikata tamaa ya kumpata mkwe mwenye ndoto ya Urais.

Maisha yaliendelea, na Mary akaolewa na kijana wa kawaida tu, Abraham Lincoln. Kipindi hicho haikutarajiiwa kuwa angekuja kuwa Rais wa Marekani. Lakini kwa kuwa Mary Todd Lincoln alikuwa amejinenea kuwa atakuja kuwa FIRST LADY wa USA, maneno yake yaliishia kuwa utabiri wake binafsi.

Ni kweli! Maneno yanaumba! Kuwa makini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…