Wanaoujiunga CCM wanatoka CHADEMA peke yake?

Wanaoujiunga CCM wanatoka CHADEMA peke yake?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,799
Reaction score
50,383
Hivi wanaojiunga na CCM ni kutoka CHADEMA peke yake watu wa kutoka vyama vingine hakuna. Ama hii ni dalili kwamba CCM inatishika na CHADEMA na ndiyo maana kwenye mikutano yao wanaona ni fahari sana kupokea wanachama toka CHADEMA?
 
CCM hawalali kwasabb ya chadema. Mwenyekiti wao akienda sehemu yoyote badala ya kuwaza awafanyie nn wananchi anawza awahujumu vipi chadema. Rubbish!!
 
Hivi wanaojiunga na CCM ni kutoka CHADEMA peke yake watu wa kutoka vyama vingine hakuna. Ama hii ni dalili kwamba CCM inatishika na CHADEMA na ndiyo maana kwenye mikutano yao wanaona ni fahari sana kupokea wanachama toka CHADEMA?
Huwa ni ccm wanageuzwa chadema halafu wajiondoe kurudi ccm mbinu za masaburi za kuvesha kundi la wahuni nguo za chadema halafu wakajifanya wamefunga tawi la cdm nonesense
 
Hivi wanaojiunga na CCM ni kutoka CHADEMA peke yake watu wa kutoka vyama vingine hakuna. Ama hii ni dalili kwamba CCM inatishika na CHADEMA na ndiyo maana kwenye mikutano yao wanaona ni fahari sana kupokea wanachama toka CHADEMA?
Hivi wanaojiunga na CCM ni kutoka CHADEMA peke yake watu wa kutoka vyama vingine hakuna. Ama hii ni dalili kwamba CCM inatishika na CHADEMA na ndiyo maana kwenye mikutano yao wanaona ni fahari sana kupokea wanachama toka CHADEMA?
Mkuu kama ulikuwa hujui CCM wanaiogopa zaidi CDM kuliko mungu
 
Hivi kumbe yule Mwigamba ametoka CHADEMA na kuhamia CCM??
na hivi kumbe wanaohamia CHADEMA wanatoka tuu CCM,vyama vingine hakuna??
 
Hivi kumbe yule Mwigamba ametoka CHADEMA na kuhamia CCM??
Hata huyo waliompokea wanakuza zaidi uenyekiti wake wa CHADEMA Arusha kuliko u-ACT wake. Wewe unadhani Mwigamba kapokewa kwa shamrashamra kama wale madiwani ambao Polepole aliwaita "Vigogo" wa CHADEMA?
 
Hivi wanaojiunga na CCM ni kutoka CHADEMA peke yake watu wa kutoka vyama vingine hakuna. Ama hii ni dalili kwamba CCM inatishika na CHADEMA na ndiyo maana kwenye mikutano yao wanaona ni fahari sana kupokea wanachama toka CHADEMA?
Kuna kipindi walikuwa wakitoka CUF tu. Kisha hawaishi yaonyesha hivi vyama vina wanachama wengi sana hawamaliziki.
 
Kuna kipindi walikuwa wakitoka CUF tu. Kisha hawaishi yaonyesha hivi vyama vina wanachama wengi sana hawamaliziki.
Ajabu ni hiyo. Wakati wa NCCR-Mageuzi ile ya Kina Mrema na Marando ilikuwa ni kutoka NCCR, ilipokuja CUF kuwa na nguvu mambo yakawa ni hivyo hivyo.

Halafu hoja nyingine ni hiyo ya kwako. Sehemu haina hata uongozi wa CHADEMA utasikia wanachama 400 wa CHADEMA wajiunga CCM na wawili wachukua kadi kwa niaba yao!!
 
Back
Top Bottom