Wanaopinga uwepo wa Mungu ni wakaidi

Wanaopinga uwepo wa Mungu ni wakaidi

Msonjo

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2019
Posts
1,378
Reaction score
2,394
Wanaokana mungu huwa wanahoja mbalimbali katika kupinga uwepo wa mungu, pia huwa wanakosoa mafunzo ya dini ili kutilia mkazo zaidi katika hilo.

Lakini ukweli ni kwamba, sio kama hoja zao zinathibitisha kutokuwepo kwa mungu, hapana.
Bali hoja zao zinathibitisha kuwa wao ni wapingaji, hivyo hakuna andiko wala muujiza utakao wafanya waamini, sembuse hizi hoja ambazo huwa wanarumbana na watu Kila kukicha.

Na hivi ndivyo walivyo tangu enzi na enzi, hoja zao ni zilezile, na hata katika Quran, imeelezwa jinsi hawa watu walivyowakaidi.

Walipoonyeshwa miujiza waliita uchawi, maneno ya Mwenyezi Mungu waliyaita hadhithi za kutunga, mitume waliwaita wachawi, machizi n.k.(rejea; Quran 6:7,10:2,15:6, 46:17, 44:14, 40:56).

Na katika kudhihirisha zaidi ukaidi wao, walifikia hadi kusema kumwambia Mwenyezi Mungu, eti kama kweli hii (yaani yale aliyokujanayo mtume) ni haki kutoka kwako basi tuteremshie mawe kutoka mbinguni, au ututeremshie adhabu yenye kuumiza.(rejea; Quran 8:32).

Hii inaonyesha ni kiasi gani hawa watu ni wakaidi maana wangetaka kujua, wangeomba kuongozwa ila kwakuwa ni wakaidi wakaomba kuangamizwa.

Atakwambia thibitisha kama mungu yupo.

Sasa kama dalili alizoziweka mungu mwenyewe kuthibitisha uwepo wake hazijakukinaisha kuamini, unadhani hoja gani itakayokukinaisha.

Muktadha wa kupinga kwao ni kwamba mungu hayupo, hivyo hoja za kuthibitisha uwepo wake zote ni batili, lakini hata kama mungu yupo na hizi ndizo dalili alizoziweka kuthibitisha uwepo wake, basi ndio tayari wameshazipinga, maana hawakubalianinazo, hivyo ni wapingaji.

Kwahiyo tatizo sio ubora wa dawa ya sikio katika kutibu, bali tatizo ni kuwa hili ni sikio la kufa, hivyo halisikii dawa.

Muendelezo


 
Kuna vitu ukifikiria hupati majibu kabisa mfano kumu judge Mungu
Hauna haja ya kumjua Mungu kabsa wakati ata wewe mwenyewe haujijui Ni Nan ,! Ulikua wap kabla ya kuzaliwa , upo apa kwa dhumuni gani ! Unaenda wap baada ya haya maisha , unataka kumjua Mungu wakati wewe haujijui
 
Kuna Miungu ipatayo zaidi ya 5,000 inayoabudiwa hapa duniani

Wasioamini Mungu hawakubaliani na hiyo Miungu yote

Ila wewe unakubaliana na Mungu mmoja na kupinga Miungu 4,999

For the same reason umekuwa mkaidi kwa hiyo miungu na huwezi kuthibitisho hiyo miungu uliyoipinga kuwa haipo

Umesema wasioamini Mungu wanapinga mafundisho ya dini, well kauli hii itakuwa valid pale muislamu atapotuambia ni kiasi gani anakubalina na habari za roho mtakatifu, Mungu katika utatu, Yesu kuwa ndio njia ya pekee na uzima, Yesu kubatizwa nk. ambazo zimeelezwa kwenye dini ya kikristo

Kama nyinyi kwa nyinyi mnaoamini Mungu mnapinga mafundisho ya dini zingine, kwanini jambo hilo hilo likifanywa na mtu asiyeamini Mungu lichukuliwe katika uzito mkubwa?

Nimeona umenukuu aya za Quran hapo kua ndio uthibitisho wa kile ulichokiita muujiza, lakini kuna madai mangapi ya kimuujiza kwenye biblia unayapinga?

Kwanini uyapinge wakati yameitwa ni miujiza? So kumbe kitu kuitwa miujiza sio kigezo cha kyafanya yawe kweli au kukubaika, kwa fact hiyo kumbe hata wewe inawezekana hayo madai yako yakawa ya kizushi vile vile otherwise uje na vivid evidence inayopimika
 
Kuna Miungu ipatayo zaidi ya 5,000 inayoabudiwa hapa duniani

Wasioamini Mungu hawakubaliani na hiyo Miungu yote

Ila wewe unakubaliana na Mungu mmoja na kupinga Miungu 4,999

For the same reason umekuwa mkaidi kwa hiyo miungu na huwezi kuthibitisho hiyo miungu uliyoipinga kuwa haipo

Umesema wasioamini Mungu wanapinga mafundisho ya dini, well kauli hii itakuwa valid pale muislamu atapotuambia ni kiasi gani anakubalina na habari za roho mtakatifu, Mungu katika utatu, Yesu kuwa ndio njia ya pekee na uzima, Yesu kubatizwa nk. ambazo zimeelezwa kwenye dini ya kikristo

Kama nyinyi kwa nyinyi mnaoamini Mungu mnapinga mafundisho ya dini zingine, kwanini jambo hilo hilo likifanywa na mtu asiyeamini Mungu lichukuliwe katika uzito mkubwa?

Nimeona umenukuu aya za Quran hapo kua ndio uthibitisho wa kile ulichokiita muujiza, lakini kuna madai mangapi ya kimuujiza kwenye biblia unayapinga?

Kwanini uyapinge wakati yameitwa ni miujiza? So kumbe kitu kuitwa miujiza sio kigezo cha kyafanya yawe kweli au kukubaika, kwa fact hiyo kumbe hata wewe inawezekana hayo madai yako yakawa ya kizushi vile vile otherwise uje na vivid evidence inayopimika
Haya Mambo ya kidini sio ya ukwel ndomaana yatakuja kupotea tu ukwel ujulikane
 
And when Our Verses (of the Quran) are recited to them, they say: "We have heard this (the Quran); if we wish we can say the like of this. This is nothing but the tales of the ancients."(8:31)

Hii nayo ni miongoni mwa hoja zao, lakini tangu Quran imeteremshwa mpaka leo hawajawahi kuleta mfano wake.
 
Kama mdau wa Dunia nimeona sometimes ni heri kuishi na wapagani kuliko watu wanaodhani / wanaojiona wameona the light hence kuwa judgmental....

Pili wale wanaotaka kuchanganya Sayansi na mambo ya kiimani huwa siwaelewi sababu wanataka kubadilisha kitu ambacho kimejengwa katika misingi ya facts na proof..., Kwa kufanya hivyo ni kutokuitendea haki Sayansi.

Kuamini waamini tu wala wasiingiliwe ila wasilete doctrines zao kama sayansi
 
Wanaokana mungu huwa wanahoja mbalimbali katika kupinga uwepo wa mungu, pia huwa wanakosoa mafunzo ya dini ili kutilia mkazo zaidi katika hilo.

Lakini ukweli ni kwamba, sio kama hoja zao zinathibitisha kutokuwepo kwa mungu, hapana.
Bali hoja zao zinathibitisha kuwa wao ni wapingaji, hivyo hakuna andiko wala muujiza utakao wafanya waamini, sembuse hizi hoja ambazo huwa wanarumbana na watu Kila kukicha.

Na hivi ndivyo walivyo tangu enzi na enzi, hoja zao ni zilezile, na hata katika Quran, imeelezwa jinsi hawa watu walivyowakaidi.

Walipoonyeshwa miujiza waliita uchawi, maneno ya Mwenyezi Mungu waliyaita hadhithi za kutunga, mitume waliwaita wachawi, machizi n.k.(rejea; Quran 6:7,10:2,15:6, 46:17, 44:14, 40:56).

Na katika kudhihirisha zaidi ukaidi wao, walifikia hadi kusema kumwambia Mwenyezi Mungu, eti kama kweli hii (yaani yale aliyokujanayo mtume) ni haki kutoka kwako basi tuteremshie mawe kutoka mbinguni, au ututeremshie adhabu yenye kuumiza.(rejea; Quran 8:32).

Hii inaonyesha ni kiasi gani hawa watu ni wakaidi maana wangetaka kujua, wangeomba kuongozwa ila kwakuwa ni wakaidi wakaomba kuangamizwa.

Atakwambia thibitisha kama mungu yupo.

Sasa kama dalili alizoziweka mungu mwenyewe kuthibitisha uwepo wake hazijakukinaisha kuamini, unadhani hoja gani itakayokukinaisha.

Muktadha wa kupinga kwao ni kwamba mungu hayupo, hivyo hoja za kuthibitisha uwepo wake zote ni batili, lakini hata kama mungu yupo na hizi ndizo dalili alizoziweka kuthibitisha uwepo wake, basi ndio tayari wameshazipinga, maana hawakubalianinazo, hivyo ni wapingaji.

Kwahiyo tatizo sio ubora wa dawa ya sikio katika kutibu, bali tatizo ni kuwa hili ni sikio la kufa, hivyo halisikii dawa.
Shida wote nyie mnaamini Mungu, vichekesho sasa kila kundi lina Mungu wake hapo ndio taabu inapo kuja
 
Kuna Miungu ipatayo zaidi ya 5,000 inayoabudiwa hapa duniani

Wasioamini Mungu hawakubaliani na hiyo Miungu yote

Ila wewe unakubaliana na Mungu mmoja na kupinga Miungu 4,999

For the same reason umekuwa mkaidi kwa hiyo miungu na huwezi kuthibitisho hiyo miungu uliyoipinga kuwa haipo

Umesema wasioamini Mungu wanapinga mafundisho ya dini, well kauli hii itakuwa valid pale muislamu atapotuambia ni kiasi gani anakubalina na habari za roho mtakatifu, Mungu katika utatu, Yesu kuwa ndio njia ya pekee na uzima, Yesu kubatizwa nk. ambazo zimeelezwa kwenye dini ya kikristo

Kama nyinyi kwa nyinyi mnaoamini Mungu mnapinga mafundisho ya dini zingine, kwanini jambo hilo hilo likifanywa na mtu asiyeamini Mungu lichukuliwe katika uzito mkubwa?

Nimeona umenukuu aya za Quran hapo kua ndio uthibitisho wa kile ulichokiita muujiza, lakini kuna madai mangapi ya kimuujiza kwenye biblia unayapinga?

Kwanini uyapinge wakati yameitwa ni miujiza? So kumbe kitu kuitwa miujiza sio kigezo cha kyafanya yawe kweli au kukubaika, kwa fact hiyo kumbe hata wewe inawezekana hayo madai yako yakawa ya kizushi vile vile otherwise uje na vivid evidence inayopimika
Ok, japo mimi sijasema kuwa kunamiungu 5000, ila nakubaliana na wewe 100% kuwa hiyo miungu 4,999 haipo,sasa sijui tunabishana nini hapo.

Au unataka mimi nithibitishe kutokuwepo kwa hao miungu wakati hata wewe unakubali kuwa haipo?

Kuhusu wanayoyaamini wakristo sijui unataka niseme nini wakati mimi ni muislamu na unajua kabisa siyaamini hayo na yamebainishwa katika Quran.

Halafu njoo na hoja zako maana wewe sio mkristo na wala huamini katika hiyo miungu 4999.

Hebu jikite kwenye mada kama huoni kuna hoja ya kujibu, unaweza kuichukua kama somo maana linaelezea watu wa aina yako.
 
Kuna Miungu ipatayo zaidi ya 5,000 inayoabudiwa hapa duniani

Wasioamini Mungu hawakubaliani na hiyo Miungu yote

Ila wewe unakubaliana na Mungu mmoja na kupinga Miungu 4,999

For the same reason umekuwa mkaidi kwa hiyo miungu na huwezi kuthibitisho hiyo miungu uliyoipinga kuwa haipo

Umesema wasioamini Mungu wanapinga mafundisho ya dini, well kauli hii itakuwa valid pale muislamu atapotuambia ni kiasi gani anakubalina na habari za roho mtakatifu, Mungu katika utatu, Yesu kuwa ndio njia ya pekee na uzima, Yesu kubatizwa nk. ambazo zimeelezwa kwenye dini ya kikristo

Kama nyinyi kwa nyinyi mnaoamini Mungu mnapinga mafundisho ya dini zingine, kwanini jambo hilo hilo likifanywa na mtu asiyeamini Mungu lichukuliwe katika uzito mkubwa?

Nimeona umenukuu aya za Quran hapo kua ndio uthibitisho wa kile ulichokiita muujiza, lakini kuna madai mangapi ya kimuujiza kwenye biblia unayapinga?

Kwanini uyapinge wakati yameitwa ni miujiza? So kumbe kitu kuitwa miujiza sio kigezo cha kyafanya yawe kweli au kukubaika, kwa fact hiyo kumbe hata wewe inawezekana hayo madai yako yakawa ya kizushi vile vile otherwise uje na vivid evidence inayopimika
Mkuu, haijalishi kuhusu idadi ya miungu, imani ya mtu kuamini kuwa Mungu Muumbaji yupo ama hayupo, ama hata juu utofauti wa imani za watu za kidini kuhusu miungu wanayoiamini na kuitumikia, bali kinachojalisha ni jina lako kuandikwa katika kitabu cha uzima.

Ni lazima ukweli ujulikane wazi kuwa mtu yeyote yule ambaye jina lake halijaandikwa katika kitabu cha uzima atakutana na hasara yake mwenyewe, kwa kuwa hukumu yake itakuwa ni ya aibu ya mauti ya milele. Nukuu ifuatayo ya maandiko inaweza kututafakarisha zaidi;

UFUNUO 13

8 Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu (Shetani), kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa, tangu kuwekwa misingi ya dunia.
9 Mtu akiwa na sikio na asikie.

Kwa hiyo basi, maandiko hayaangalii wala kubagua kuhusu imani ama dini ya mtu. Maandiko yatuasa kuwa na mahusiano mema watu wengine, na pia yule aliyekuumba. Nukuu ya maandiko hutupa picha kuhusu jambo hili;

UFUNUO 6

9 Kisha, Mwanakondoo akavunja mhuri wa tano. Nikaona pale chini ya madhabahu ya kufukizia ubani roho za wale waliouawa kwa sababu ya ujumbe wa Mungu, na kwa sababu ya ushuhuda waliokuwa nao.

Kwa muktadha huo basi,
1. Wale wenye ujumbe wa Mungu ni wale wanaoamini na kuishika kwa dhati pamoja na kuitii imani yake ya kweli aliyowajalia kuitambua

2. Wale wenye ushuhuda ni wale ambao matendo na dhamiri zao zitawafanya wahesabiwe kuwa ni wenye haki.
 
Ok, japo mimi sijasema kuwa kunamiungu 5000, ila nakubaliana na wewe 100% kuwa hiyo miungu 4,999 haipo,sasa sijui tunabishana nini hapo.

Au unataka mimi nithibitishe kutokuwepo kwa hao miungu wakati hata wewe unakubali kuwa haipo?

Kuhusu wanayoyaamini wakristo sijui unataka niseme nini wakati mimi ni muislamu na unajua kabisa siyaamini hayo na yamebainishwa katika Quran.

Halafu njoo na hoja zako maana wewe sio mkristo na wala huamini katika hiyo miungu 4999.

Hebu jikite kwenye mada kama huoni kuna hoja ya kujibu, unaweza kuichukua kama somo maana linaelezea watu wa aina yako.
Hakuna ubishi

Kama Miungu hiyo haipo na wewe unakubali na huwezi kuthibitisha haipo for the same principle hata mimi nasema Mungu wako hayupo
 
Mkuu, haijalishi kuhusu idadi ya miungu, imani ya mtu kuamini kuwa Mungu Muumbaji yupo ama hayupo, ama hata juu utofauti wa imani za watu za kidini kuhusu miungu wanayoiamini na kuitumikia, bali kinachojalisha ni jina lako kuandikwa katika kitabu cha uzima.

Ni lazima ukweli ujulikane wazi kuwa mtu yeyote yule ambaye jina lake halijaandikwa katika kitabu cha uzima atakutana na hasara yake mwenyewe, kwa kuwa hukumu yake itakuwa ni ya aibu ya mauti ya milele. Nukuu ifuatayo ya maandiko inaweza kututafakarisha zaidi;

UFUNUO 13

8 Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu (Shetani), kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa, tangu kuwekwa misingi ya dunia.
9 Mtu akiwa na sikio na asikie.

Kwa hiyo basi, maandiko hayaangalii wala kubagua kuhusu imani ama dini ya mtu. Maandiko yatuasa kuwa na mahusiano mema watu wengine, na pia yule aliyekuumba. Nukuu ya maandiko hutupa picha kuhusu jambo hili;

UFUNUO 6

9 Kisha, Mwanakondoo akavunja mhuri wa tano. Nikaona pale chini ya madhabahu ya kufukizia ubani roho za wale waliouawa kwa sababu ya ujumbe wa Mungu, na kwa sababu ya ushuhuda waliokuwa nao.

Kwa muktadha huo basi,
1. Wale wenye ujumbe wa Mungu ni wale wanaoamini na kuishika kwa dhati pamoja na kuitii imani yake ya kweli aliyowajalia kuitambua

2. Wale wenye ushuhuda ni wale ambao matendo na dhamiri zao zitawafanya wahesabiwe kuwa ni wenye haki.
Usinipe nukuu za kwenye biblia wakati huna uhakika na authenticity ya hicho kitabu

Biblia ni madai sio uthibitisho, ni kama muislamu anayetaka kuku convice kuwa muhammad alipaa mbingu ya saba na mnyama mwenye muonekano wa farasi ambaye ana mabawa, sitegemei kuona utakubali maelezo hayo licha ya kwamba kayatoa kwenye Quran
 
Ni jambo jema sana na kiungwana kukubaliana kutokukubaliana kwa mambo kama haya yahusuyo dini, imani na hata mambo ya uungu.
 
Back
Top Bottom