Hi, all! Kila nikichangia hii mada na wadau sehemu ninazopita huwa najikuta niko peke yangu.
1. Napata mshahara wangu na mke wangu anajua napata kiasi gani. Tunatumia wote kila mmoja kulingana na mahitaji yake.
2. Siwezi na wala sifikirii kumpiga mke wangu maana nampenda sana. Huu ni mwaka wangu wa 5 na sijawahi kumpiga.
3. Kukitokea issue huwa tunaeleweshana na hatugombani na wala hata mtu wa chumba kingine hawezi kujua unless aone tu moods zetu kwani mkielezana kitu na kama mumeelezana kwa kina mtu atakuonekana baridi kwa muda (sku mbili/tatu au wiki) kabla ya kurudia hali ya kawaida.
4. Sina nyumba ndogo na wala sitarajii kuwa nayo maana ni kukosa uaminifu katika ndoa na kunaweza kusababisha maambuzi ya magonjwa ya zinaa na hata kufikwa na mauti. Kukosa uaminifu katika ndoa ni sawa na unafiki maana ni lazima uwe mwongo. Ukichelewa huko kwa nyumba ndogo utasema "ulikuwa na safari ya kikazi". Uwongo wa namna hii ni mbaya sana maana nilimsikia mmoja akimdanganya mwenzake wa ndoa kwa simu kuwa "ndio wanakaribia Morogoro" wakati alikuwa Mbagala Rangi 3. Sikuamini!
5. Kuoa siyo kununua mke/mwenza hata kama umetoa mahari. Mke/mwenza wa ndoa siyo mali/kitu cha kuhifadhi kwenye mfuko na unaweza kukitumia unavyopenda. Wengine hata wanadiriki kumtia mke/mwenza wao kilema na hata kumwua kwa kisingizio cha "wivu wa mapenzi." Na mara nyingi wanaofanya haya siyo waaminifu wao wenyewe.
6. Nasema haya kwa sababu leo nimeshuhudia jamaa akimtwanga mke wake mangumi. Kisa? Mke wake alienda kumchukua baa waende nyumbani baada ya kuona muda umepita bila kufika na jamaa huyu anakunywa kila siku na sijui kama ana "any future"!
7. Kama mtu unampenda huwezi kumpiga, kumwumiza, kuwa na wasiwasi naye na wala kumwua! Kama wewe ni mmojawapo wa haya mataahira badilika kuanzia muda huu! Jifunze kuwa non-violent na inawezekana!
1. Napata mshahara wangu na mke wangu anajua napata kiasi gani. Tunatumia wote kila mmoja kulingana na mahitaji yake.
2. Siwezi na wala sifikirii kumpiga mke wangu maana nampenda sana. Huu ni mwaka wangu wa 5 na sijawahi kumpiga.
3. Kukitokea issue huwa tunaeleweshana na hatugombani na wala hata mtu wa chumba kingine hawezi kujua unless aone tu moods zetu kwani mkielezana kitu na kama mumeelezana kwa kina mtu atakuonekana baridi kwa muda (sku mbili/tatu au wiki) kabla ya kurudia hali ya kawaida.
4. Sina nyumba ndogo na wala sitarajii kuwa nayo maana ni kukosa uaminifu katika ndoa na kunaweza kusababisha maambuzi ya magonjwa ya zinaa na hata kufikwa na mauti. Kukosa uaminifu katika ndoa ni sawa na unafiki maana ni lazima uwe mwongo. Ukichelewa huko kwa nyumba ndogo utasema "ulikuwa na safari ya kikazi". Uwongo wa namna hii ni mbaya sana maana nilimsikia mmoja akimdanganya mwenzake wa ndoa kwa simu kuwa "ndio wanakaribia Morogoro" wakati alikuwa Mbagala Rangi 3. Sikuamini!
5. Kuoa siyo kununua mke/mwenza hata kama umetoa mahari. Mke/mwenza wa ndoa siyo mali/kitu cha kuhifadhi kwenye mfuko na unaweza kukitumia unavyopenda. Wengine hata wanadiriki kumtia mke/mwenza wao kilema na hata kumwua kwa kisingizio cha "wivu wa mapenzi." Na mara nyingi wanaofanya haya siyo waaminifu wao wenyewe.
6. Nasema haya kwa sababu leo nimeshuhudia jamaa akimtwanga mke wake mangumi. Kisa? Mke wake alienda kumchukua baa waende nyumbani baada ya kuona muda umepita bila kufika na jamaa huyu anakunywa kila siku na sijui kama ana "any future"!
7. Kama mtu unampenda huwezi kumpiga, kumwumiza, kuwa na wasiwasi naye na wala kumwua! Kama wewe ni mmojawapo wa haya mataahira badilika kuanzia muda huu! Jifunze kuwa non-violent na inawezekana!