Ukifuatilia, wengi wa viongozi wanaokemea watu wasiandamane ni kama wanataka raia watulie na kuburuzwa.
Issues zinazolalamikiwa na wananchi hazifanyiwi kazi, watu wanaendelea kutekwa, hofu ya wananchi juu ya maisha yao inazidi kutanda kwani wananchi wanatekwa, wanapotezwa au kuuawa na haijawahi kusikika kiongozi wa juu na mamlaka za husika zikikemea vitendo hivi wazi wazi.
Tangu awe Rais, Samia hatoi kauli thabiti ya kukemea matendo haya ya kikatili dhidi ya maisha ya watu.
Wengi wa wanaotufokea ni wanaotaka vyeo, wenye ukaribu au kunufaika kwa namna moja au nyingine na Serikali iliyo madarakani.
Kuna wizi uliopiliza wa mali za umma. Watu wanapambana wapate vyeo ili waitafune nchi huku uwajibikaji ukiwa sifuri kabisa.
Vyombo vilivyopewa dhamana badala ya kutekeleza wajibu wake vinatumika kuumiza wananchi badala ya kuwatumikia.
Yaani, tumekuwa Taifa la ajabu sana. Tuna watu wanaotuona kama mifugo yao, si wananchi.
Haya mambo yanakwaza sana. Huyu kijana (video) kaeleza vema
Issues zinazolalamikiwa na wananchi hazifanyiwi kazi, watu wanaendelea kutekwa, hofu ya wananchi juu ya maisha yao inazidi kutanda kwani wananchi wanatekwa, wanapotezwa au kuuawa na haijawahi kusikika kiongozi wa juu na mamlaka za husika zikikemea vitendo hivi wazi wazi.
Tangu awe Rais, Samia hatoi kauli thabiti ya kukemea matendo haya ya kikatili dhidi ya maisha ya watu.
Wengi wa wanaotufokea ni wanaotaka vyeo, wenye ukaribu au kunufaika kwa namna moja au nyingine na Serikali iliyo madarakani.
Kuna wizi uliopiliza wa mali za umma. Watu wanapambana wapate vyeo ili waitafune nchi huku uwajibikaji ukiwa sifuri kabisa.
Vyombo vilivyopewa dhamana badala ya kutekeleza wajibu wake vinatumika kuumiza wananchi badala ya kuwatumikia.
Yaani, tumekuwa Taifa la ajabu sana. Tuna watu wanaotuona kama mifugo yao, si wananchi.
Haya mambo yanakwaza sana. Huyu kijana (video) kaeleza vema