Wanao ogopa mabadiliko ni wanyonyaji

Wanao ogopa mabadiliko ni wanyonyaji

Magufuli 05

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2023
Posts
1,990
Reaction score
3,821
Ukweli ni kwamba tunahitaji mabadiliko ya kanuni na sheria za uchaguzi. Hatuwezi kuwa conservative. Kwanini hawa jamaa hawataki mabadiliko?

Hivi kweli unaweza ukawa na mfumo kama huu ukasema una uchaguzi huru na haki?
Chadema mlichelewa sana kuamua jambo hili. Lakini siyo mbaya kwasasa mmeonyesha kuwa chama chenu kina watu wenye akili zinazofanya kazi. Najua walioko madarakani watashupaza shingo kwasasa kujaribu kutikisa lakini hawana muda mrefu watakubali wenyewe. Uchaguzi ujao ambao sijui utafanyika lini utakuwa mgumu sana.

Baada ya chadema kususia zoezi la ujazaji wa form za maadili mmeonyesha ukomavu lakini vyama 17 shindani wa CCM vilivyokubali kujaza wametuonyesha watanzania kwamba wale ni njaa na si vyama shindani. Kumbe tuna utitiri wa vyama kwa ajili ya business tu. Wao ruzuku ni mhimu kuliko maslahi ya nchi.

Mliopo madarakani someni nyakati. Kiburi kinakwenda kuwaponza hivi punde. Mmewachezea watanzania kwa muda mrefu sana lakini kwasasa nature imekataa. Narudia nature imekataa. Nyinyi ni wanyonyaji kama kupe. Kwanini hamtaki mabadiliko? Mnaogopa kuangushwa.

Peter Mutharika na Edgar chagwa Rungu walikuwa wagumu na kiburi kama chenu lakini waliangushwa licha ya kutumia Dola. Nature iliamua na hatimae Lazarus chakwela na Hakainde Hichilema wakatangazwa mtawalia.
Chagueni kukubali mabadiliko au kuangushwa kwa aibu.

"Unaweza ukawadanganya watu kwa nyakati tofauti lakini hutaweza kuwadanganya watu wote kwa wakati mmoja"
 
Ahsante mtoa mada chadema hii ni asili ni halisi wengine ni wafanyabiashara.
 
Asante sana ndugu.. Kenge huwa hasikii hadi damu imtoke masikioni.. ccm ni kenge, sikio la kufa.. watanzania wamefanywa ndondocha kwa muda mrefu sana.. sote tuseme SASA BASI.. ubaya ubwela
#NOREFORMSNOELECTION
 
CCM wanajua kukubali mabadiliko ya sheria za uchaguzi ni kujichimbia kaburi lao wenyewe.

wanajua chaguzi zote hawajawahi kushinda.
 
Back
Top Bottom