MGAWARIZIKI
JF-Expert Member
- Dec 16, 2010
- 305
- 47
Wananchi wa kijiji cha segese wilayani Kahama wamechimba barabara iendayo Kakola ili kuzuia mawasiliano ya barabara wakimtaka mbunge wao atekeleze ahadi alizowaahidi kwenye kampeni zake za uchaguzi wa mwaka 2005 na 2011, wamedai mbunge wao amekuwa akiwaahidi umeme na maji kwa awamu zote mbili za uchaguzi bila mafanikio yoyote. Hii nafikiri inaweza kuwa changamoto kwa viongozi wengine wanaodanganya wananchi na kutoa ahadi za uongo.Wana JF mnalionaje hilo?